Tukubali kutokubaliana na uteuzi wa Mnyeti

leonaldo

JF-Expert Member
Oct 26, 2014
2,585
3,179
Nilishituka sana niliposikia Rais Magufuli amemteua mkuu wa wilaya ya Arumeru kuwa mkuu wa mkoa na jambo hili likanifanya nikumbuke maswahibu yaliyo mpata
rais Trunp wa Marekani hivi karibuni alipogubikwa na lawama kutoka kila kona ya nchi ya Marekani, kisa alishindwa kuonyesha heshima alipopiga simu kumpa pole mke wa mwanajeshi wa marekani aliefia afrika kwenye kikosi cha kurinda amani cha UN.

Tunajifunza nini sisi watanzania kutokana na mkasa huo:-
  1. Wamarekani hawamkopeshi Rais wala hawamuonei haya kumwambia ukweli anapomkosea hata raia mmoja tu wa marekani.
  2. Vyombo vyote vya habari duniani vililipoti taarifa hii vikiwemo vya serikari kama VOA bila kujificha nyuma ya unafki ili kulinda hadhi na heshima ya taifa la Marekani.
  3. Dhamana ya urais wa USA haiko juu ya haki za raia wa marekani.
  4. Heshima, haki na utu wa raia wa marekani hauwezi kutwezwa au kuingiliwa na taasisi au mtu yeyote yule.
  5. Hakuna mtu ama taasisi iliyomtetea rais katika hili ilimbidi ajitetee binafsi kama Trump.
  6. Wanajua kutenganisha baina ya taasisi ya urais na mtu binafsi kama Trump tofauti na Tanzania ambapo hakuna tofauti kati ya taasisi ya urais na Magufuli kama mtu binafsi.
Kitendo cha rais kuteua mkuu wa wilaya ya Arumeru kuwa mkuu wa mkoa ambae yuko chini ya uchunguzi dhidi ya tuhuma za rushwa,hii inaweza kutafsiliwa kama:-

  • kitendo cha kuizuia taasisi ya kupambana rushwa kuendelea na uchunguzi dhidi ya mtuhumiwa.
  • Kumwepusha mtuhumiwa na adhabu inayoweza kumkabili endapo tuhuma dhidi yake zitathibitishwa.
  • Kujaribu kufifisha uzito wa makosa ya mtuhumiwa.
  • Kukiri kwa mtuhumiwa kujihusisha na alichokiita kununua wapinza na kuwa bado ataendelea kufanya hivyo ni kujaribu kufifisha kosa la rushwa lakini pia ni ujumbe wa dharau dhidi ya raia wa Tanzania.
  • Dalili ya wazi kutangazwa kwa tabaka la raia wasioguswa na sheria.
Hili ni tatizo kubwa na la wazi kushinda hilo la wamarekani pamoja na kuwa wamarekani walisimama pamoja kupinga kudharirishwa kwa taasisi ya urais na hadhi ya nchi yao, tukubali kuwa hili ni tatizo na linatukabili kama taifa kwa sasa, cha kushangaza ni kuwa hakuna taasisi ya kiraia,dini,watu mashuhuri, Maaskofu, Mashehe ukiachilia mbali wananchi wa kawaida mitandaoni waliojitokeza walau kukemea kitendo hiki.
Hakika watanzania hatutaiepuka dhambi ya unafki uliotukuka.

Tumeiacha hadhi na heshima ya nchi kutwezwa huku tukijificha nyuma ya kichaka cha unafiki wa kuiheshimu taasisi ya rais, vyama vya siasa na chuki binafsi,na sio ajabu tukaona watu wanatetea tendo hili.
 
Tatizo umegawanyika. Wengi wanaona ufa mkubwa wa taifa hili, lakini wanaleta hoja binafsi za chuki. Mama ntilie anfurahi mwanamke mwenzake aliyekuwa mfanyakazi katumbuliwa, wamekuwa sawa!

Kijana anafurahi kijana mwenzake amefukuzwa /ametumbuliwa wamekuwa sawa wote hawana ajira rasmi. Udikiteita wa "Mungu" ni faraja kwa wengine mradi mkono wao unakwenda kinywani!
 
Tatizo letu hatuna upinzani makini.
Mnaona upande wapili,hivi mtu mliemuita fisadi kwa miaka nane mkamfanya mgombea urais ndani ya dakika 30 tu,nani atawasamehe wasanii kama nyinyi?mnapata wapi kuona uchafu wa serikali wakati ya kwenu mnayafutika chini ya uvungu na kuwafanya watanzania mafala
 
Ulitaka tufanyeje ikiwa kitendo cha KUNUNUA MADIWANI kimeratibiwa na HQ CCM lumumba chini ya Mwenyekiti wake akisaidiana na Polepole Humphrey??

Unataka watanzania tufanyeje ikiwa PCCB haina meno ya kung'ata wateuliwa wa RAIS na hao wako juu ya sheria hata wakiua watu wataitwa 'WASIOJULIKANA" kama kuna mtanzania mwenye akili timamu kama hadi leo anaamini ati serikali ya Awamu ya 5 inapiga vita RUSHWA na UFISADI basi aende hospitali akapimwe hayuko sawa
 
Tatizo letu hatuna upinzani makini.
Mnaona upande wapili,hivi mtu mliemuita fisadi kwa miaka nane mkamfanya mgombea urais ndani ya dakika 30 tu,nani atawasamehe wasanii kama nyinyi?mnapata wapi kuona uchafu wa serikali wakati ya kwenu mnayafutika chini ya uvungu na kuwafanya watanzania mafala

Issue ni RUSHWA ambayo RAIS amesema anapiga vita lakini anaikumbatia issue za Lowassa zimekuwa zilipendwa.Tugange yaliyopo.Kila siku Lowassa Lowassa Mnyeti alitumwa na Lowassa kutoa RUSHWA kwa madiwani??

Kijana Tanzania ni ya watanzania siyo ya CCM au ya Magufuli.
 
Tatizo umegawanyika. Wengi wanaona ufa mkubwa wa taifa hili, lakini wanaleta hoja binafsi za chuki. Mama ntilie anfurahi mwanamke mwenzake aliyekuwa mfanyakazi katumbuliwa, wamekuwa sawa! Kijana anafurahi kijana mwenzake amefukuzwa /ametumbuliwa wamekuwa sawa wote hawana ajira rasmi. Udikiteita wa "Mungu" ni faraja kwa wengine mradi mkono wao unakwenda kinywani!
Ni kweli ksbisa nakubaliana wewe ndio maana hata humu JF utakutana na mtu kajibu hoja za mtu mwingine kwa kusema "Ngoja yakomeshwe" bila hata kutoa sababu kwa nini anaotaka wakomeshwe wanastahili kukomeshwa, haya yote yanatokana na chuki binafsi,husda,chuki xa kisiasa na ushabiki wa kijinga tu ambso huwa ni faida kwa wanasisa kwa gharama ya umoja wa kitaifa
 
Na huo ni ujumbe wanatumiwa DCs wote kuwa mkuu wao anakunwa na hayo mambo waongeze juhudi. Tunahoji makusanyo yanakwenda wapi kumbe "msema ukweli" ameyawekeza kujenga kiwanda cha kuua upinzani. Tusubiri kwanza huo "uchumi wa kati" uje ndio tuanze kumbeza yule aliyesema tuna RAIS WA AJABU kupata kutokea.
 
Tatizo letu hatuna upinzani makini.
Mnaona upande wapili,hivi mtu mliemuita fisadi kwa miaka nane mkamfanya mgombea urais ndani ya dakika 30 tu,nani atawasamehe wasanii kama nyinyi?mnapata wapi kuona uchafu wa serikali wakati ya kwenu mnayafutika chini ya uvungu na kuwafanya watanzania mafala
Mwanao akifanya kosa, ww kama mzazi pia inabidi ufanye makosa makusudi, halafu ukiulizwa unasema mbona mtt wangu nae alikosea hamjamsema.
 
Issue ni RUSHWA ambayo RAIS amesema anapiga vita lakini anaikumbatia issue za Lowassa zimekuwa zilipendwa.Tugange yaliyopo.Kila siku Lowassa Lowassa Mnyeti alitumwa na Lowassa kutoa RUSHWA kwa madiwani??

Kijana Tanzania ni ya watanzania siyo ya CCM au ya Magufuli.
Acha kuhamisha magoli ili tu ufute kiu yako ya kisiasa.Mlitaka fisadi liingie ikulu saa hizi tungekua wapi?

Hata hivyo tuhuma za mnyeti ni za kutengenezwa tu kisiasa,kama kweli flash ina nguvu waambieni akina kibatala waipeleke tume ya utawala bora,Mbona Boniface alipeleka kesi ya vyeti vya makonda huko?Tatizo lenu mnapenda sana kulia mitandaoni kana kwamba huku kuna wapiga kura
 
Nilishituka sana niliposikia Rais Magufuli amemteua mkuu wa wilaya ya Arumeru kuwa mkuu wa mkoa na jambo hili likanifanya nikumbuke maswahibu yaliyo mpata
rais Trunp wa Marekani hivi karibuni alipogubikwa na lawama kutoka kila kona ya nchi ya Marekani, kisa alishindwa kuonyesha heshima alipopiga simu kumpa pole mke wa mwanajeshi wa marekani aliefia afrika kwenye kikosi cha kurinda amani cha UN.

Tunajifunza nini sisi watanzania kutokana na mkasa huo:-
  1. Wamarekani hawamkopeshi Rais wala hawamuonei haya kumwambia ukweli anapomkosea hata raia mmoja tu wa marekani.
  2. Vyombo vyote vya habari duniani vililipoti taarifa hii vikiwemo vya serikari kama VOA bila kujificha nyuma ya unafki ili kulinda hadhi na heshima ya taifa la Marekani.
  3. Dhamana ya urais wa USA haiko juu ya haki za raia wa marekani.
  4. Heshima, haki na utu wa raia wa marekani hauwezi kuingiliwa na taasisi au mtu yeyote yule.
  5. Hakuna mtu ama taasisi iliyomtetea rais katika hili ilimbidi ajitetee binafsi kama Trump.
  6. Wanajua kutenganisha baina ya taasisi ya urais na mtu binafsi kama Trump tofauti na Tanzania ambapo hakuna tofauti kati ya taasisi ya urais na Magufuli kama mtu binafsi.
Kitendo cha rais kuteua mkuu wa wilaya ya Arumeru kuwa mkuu wa mkoa ambae yuko chini ya uchunguzi dhidi ya tuhuma za rushwa,hii inaweza kutafsiliwa kama:-

  • kitendo cha kuizuia taasisi ya kupambana rushwa kuendelea na uchunguzi dhidi ya mtuhumiwa.
  • Kumwepusha mtuhumiwa na adhabu inayoweza kumkabili endapo tuhuma dhidi yake zitathibitishwa.
  • Kujaribu kufifisha uzito wa makosa ya mtuhumiwa.
  • Kukili kwa mtuhumiwa kujihusisha na alichokiita kununua wapinza na kuwa bado ataendelea kufanya hivyo ni kujaribu kufifisha kosa la rushwa lakini pia ni ujumbe wa dharau dhidi ya raia wa Tanzania.
  • Dalili ya wazi kutangazwa kwa tabaka la raia wasioguswa na sheria.
Hili ni tatizo kubwa na la wazi linalotukabili kama taifa kwa sasa,cha kushangaza ni kuwa hakuna taasisi ya kiraia,dini,watu mashuhuri,Maaskofu,Mashehe ukiachilia mbali wananchi wa kawaida mitandaoni waliojitokeza walau kukemea kitendo hiki.
Hakika watanzania hatutaiepuka dhambi ya unafki uliotukuka.
Tumeiacha hadhi na heshima ya nchi kutwezwa huku tukijificha nyuma ya kichaka cha unafiki wa kuiheshimu taasisi ya rais,vyama vya siasa na chuki binafsi,na sio ajabu tukaona watu wanatetea tendo hili.
Kufananisha America na Tanzania ni kosa kubwa lililokithiri
 
Tatizo letu hatuna upinzani makini.
Mnaona upande wapili,hivi mtu mliemuita fisadi kwa miaka nane mkamfanya mgombea urais ndani ya dakika 30 tu,nani atawasamehe wasanii kama nyinyi?mnapata wapi kuona uchafu wa serikali wakati ya kwenu mnayafutika chini ya uvungu na kuwafanya watanzania mafala

Kwanini mnajitoa akili namna hii?
Who is lowassa ni fisadi au si fissdi,
Let say ni fisadi yes ni fisadi nani anatakiwa ku-deal nae?
Kwanini tunaendekeza uzembe, kama lowassa kama ni fisadi mkamateni akajibu tuhuma zake

Halafu ulivyo katika maada umemuingiza lowassa hahusiki hapa
Kwahiyo kwa kauli yako upinzani ndo wana jukumu la kukosoa
Je huko marekani alikotaja mtoa maada umesikia upinzani ndo wanakosoa
Jikite kwenye maada husika
 
Unaweza kuwa ni mpuuzi wa kiwango cha juu sana. Mwanao akifanya kosa, ww kama mzazi pia inabidi ufanye makosa makusudi, halafu ukiulizwa unasema mbona mtt wangu nae alikosea hamjamsema. STUPID!!
Ujinga mwingine kila ukihoji juu ya serikali unaitwa mpinzani...!! Hivi taifa hili raia wake hawaruhusiwi kuhoji chochote juu ya serikali yao
 
Acha kuhamisha magoli ili tu ufute kiu yako ya kisiasa.Mlitaka fisadi liingie ikulu saa hizi tungekua wapi?
Hata hivyo tuhuma za mnyeti ni za kutengenezwa tu kisiasa,kama kweli flash ina nguvu waambieni akina kibatala waipeleke tume ya utawala bora,Mbona Boniface alipeleka kesi ya vyeti vya makonda huko?Tatizo lenu mnapenda sana kulia mitandaoni kana kwamba huku kuna wapiga kura
Wewe hupigi kura? Hivi kumbe kiwango chako cha ufahamu ni sawa na cha YEHODAYA!!?
 
Issue ni RUSHWA ambayo RAIS amesema anapiga vita lakini anaikumbatia issue za Lowassa zimekuwa zilipendwa.Tugange yaliyopo.Kila siku Lowassa Lowassa Mnyeti alitumwa na Lowassa kutoa RUSHWA kwa madiwani??

Kijana Tanzania ni ya watanzania siyo ya CCM au ya Magufuli.
umepewa mfano hai haiwezekani maamuzi magum tu yatoke kwa dk tano wakati mlizunguka nchi nzima kutuaminisha lowassa fisadi namba moja. toa boliti kwako before ya kibanzi cha kwa mwenzako.
 
Tatizo letu hatuna upinzani makini.
Mnaona upande wapili,hivi mtu mliemuita fisadi kwa miaka nane mkamfanya mgombea urais ndani ya dakika 30 tu,nani atawasamehe wasanii kama nyinyi?mnapata wapi kuona uchafu wa serikali wakati ya kwenu mnayafutika chini ya uvungu na kuwafanya watanzania mafala

Ndugu yangu wakati mwingine acha mzaha kwenye fact. Kuna mahakama ya mafisadi ilioanzishwa kwa mbwembwe kwanini ilikosa watuhumiwa kama mlikuwa na uhakika wa tuhuma dhidi yake?

Haya mnayofanyia ushabiki leo kwa ujira mdogo hamumsaidii Bw Yule wala nchi kwaujumla.

Sisi sote ni Watz na kila mmoja wetu anaona uchumi ulivyoyumbishwa kwa makusudi ili kuwakomoa Watz wanyonge. Nchi inavurugika watu wanapigwa risasi mchana kweupe, amani inachokonolewa kwa nguvu zote halafu mnaleta ushabiki wa kipuuzi hapa.

Hili suala haliwahusu Wapimzani peke yao na kama ndivyo unavyoamini baada ya miezi michache ijayo ako kaujira kako unakopata kwa sasa kwa ushabiki utatoweka. Mark my words, time'll tell.
 
Nilishituka sana niliposikia Rais Magufuli amemteua mkuu wa wilaya ya Arumeru kuwa mkuu wa mkoa na jambo hili likanifanya nikumbuke maswahibu yaliyo mpata
rais Trunp wa Marekani hivi karibuni alipogubikwa na lawama kutoka kila kona ya nchi ya Marekani, kisa alishindwa kuonyesha heshima alipopiga simu kumpa pole mke wa mwanajeshi wa marekani aliefia afrika kwenye kikosi cha kurinda amani cha UN.

Tunajifunza nini sisi watanzania kutokana na mkasa huo:-
  1. Wamarekani hawamkopeshi Rais wala hawamuonei haya kumwambia ukweli anapomkosea hata raia mmoja tu wa marekani.
  2. Vyombo vyote vya habari duniani vililipoti taarifa hii vikiwemo vya serikari kama VOA bila kujificha nyuma ya unafki ili kulinda hadhi na heshima ya taifa la Marekani.
  3. Dhamana ya urais wa USA haiko juu ya haki za raia wa marekani.
  4. Heshima, haki na utu wa raia wa marekani hauwezi kuingiliwa na taasisi au mtu yeyote yule.
  5. Hakuna mtu ama taasisi iliyomtetea rais katika hili ilimbidi ajitetee binafsi kama Trump.
  6. Wanajua kutenganisha baina ya taasisi ya urais na mtu binafsi kama Trump tofauti na Tanzania ambapo hakuna tofauti kati ya taasisi ya urais na Magufuli kama mtu binafsi.
Kitendo cha rais kuteua mkuu wa wilaya ya Arumeru kuwa mkuu wa mkoa ambae yuko chini ya uchunguzi dhidi ya tuhuma za rushwa,hii inaweza kutafsiliwa kama:-

  • kitendo cha kuizuia taasisi ya kupambana rushwa kuendelea na uchunguzi dhidi ya mtuhumiwa.
  • Kumwepusha mtuhumiwa na adhabu inayoweza kumkabili endapo tuhuma dhidi yake zitathibitishwa.
  • Kujaribu kufifisha uzito wa makosa ya mtuhumiwa.
  • Kukili kwa mtuhumiwa kujihusisha na alichokiita kununua wapinza na kuwa bado ataendelea kufanya hivyo ni kujaribu kufifisha kosa la rushwa lakini pia ni ujumbe wa dharau dhidi ya raia wa Tanzania.
  • Dalili ya wazi kutangazwa kwa tabaka la raia wasioguswa na sheria.
Hili ni tatizo kubwa na la wazi kushinda hilo la wamarekani pamoja na kuwa wamarekani walisimama pamoja kupinga kudharirishwa kwa taasisi ya urais na hadhi ya nchi yao,tukubali kuwa hili ni tatizo na linatukabili kama taifa kwa sasa,cha kushangaza ni kuwa hakuna taasisi ya kiraia,dini,watu mashuhuri,Maaskofu,Mashehe ukiachilia mbali wananchi wa kawaida mitandaoni waliojitokeza walau kukemea kitendo hiki.
Hakika watanzania hatutaiepuka dhambi ya unafki uliotukuka.
Tumeiacha hadhi na heshima ya nchi kutwezwa huku tukijificha nyuma ya kichaka cha unafiki wa kuiheshimu taasisi ya rais,vyama vya siasa na chuki binafsi,na sio ajabu tukaona watu wanatetea tendo hili.
Nyeti ni rafiki sana wa rais na mpambe mzuri
 
Acha kuhamisha magoli ili tu ufute kiu yako ya kisiasa.Mlitaka fisadi liingie ikulu saa hizi tungekua wapi?
Hata hivyo tuhuma za mnyeti ni za kutengenezwa tu kisiasa,kama kweli flash ina nguvu waambieni akina kibatala waipeleke tume ya utawala bora,Mbona Boniface alipeleka kesi ya vyeti vya makonda huko?Tatizo lenu mnapenda sana kulia mitandaoni kana kwamba huku kuna wapiga kura
Sasa kama Lowassa ni fisadi na Baba J anajua, na mahakama ya mafisadi ipo, mnasubiri nini kumpeleka huko? Acheni kutupigia kelele.
 
umepewa mfano hai haiwezekani maamuzi magum tu yatoke kwa dk tano wakati mlizunguka nchi nzima kutuaminisha lowassa fisadi namba moja ..acheni ufala toa boliti kwako before ya kibanzi cha kwa mwenzako.

Hakuna mfano hapo imeshapitwa na wakati kwa sasa tumeaminishwa na JPM anapiga vita RUSHWA tunapoona anakengeuka tunatakiwa tumwambie hii siyo ahadi yako.Kama watanzania tutashindwa kukemea ati kwa sababu Chadema ilimweka Lowassa kuwa mgombea basi tuna walakini kichwani.

JPM anasupport kutoa RUSHWA halafu tunamlaumu Lowassa,then mwenye akili hii hastahili kuitwa Mtanzania.
 
Tatizo letu hatuna upinzani makini.
Mnaona upande wapili,hivi mtu mliemuita fisadi kwa miaka nane mkamfanya mgombea urais ndani ya dakika 30 tu,nani atawasamehe wasanii kama nyinyi?mnapata wapi kuona uchafu wa serikali wakati ya kwenu mnayafutika chini ya uvungu na kuwafanya watanzania mafala
Sisi tunaongelea Tanzania yetu, ya watoto wetu, wajukuu wetu hata wewe ukifa, tunafikilia miaka 50 mbele Tanzania inaelekea wapi? Wewe unasema eti upinzani ulituaminisha!! aliekuwa ana kuaminisha nani, si uende kumuuliza wewe? Kama uliamini si uende ukafungue kesi ya kumshtaki huyo ulieaminishwa?

Kwako wewe Tanzania ni huyo ulioaminishwa, Tunaongelea kiburi, jeuri, utemi, ubaguzi na chuki nyingi zinazofanywa na watawala tulio wapa dhamana ya kutuongoza. Wewe unakuja kuleta tamthilia hapa, una nini wewe,
 
Tatizo letu hatuna upinzani makini.
Mnaona upande wapili,hivi mtu mliemuita fisadi kwa miaka nane mkamfanya mgombea urais ndani ya dakika 30 tu,nani atawasamehe wasanii kama nyinyi?mnapata wapi kuona uchafu wa serikali wakati ya kwenu mnayafutika chini ya uvungu na kuwafanya watanzania mafala
Utawajibu nini kama wakikuuliza huyo Fisadi mlimfanya nini alipokuwa kwenu na mmemfanya nini alipkwenda kwao?
 
Back
Top Bottom