Tukiyahitaji maisha ya Libya enzi ya Gaddafi, hatuna budi kumpa nafasi zaidi Rais Magufuli

Inawezekana ikawa sawa, kwakuwa katiba ndo sheria mama ya nchi husika. Ila kipi kibebwe na hiyo katiba mpya? Hapo ndo kiini cha swali langu. Serikali 3,mgombea huru, tume huru, mahakama huru, bunge huru,majimbo nk ndo suluhisho la yote haya? Watanzania wengi wanalalamika na ubinafsi wa wenye nafasi, (ufisadi, kukosa uzalendo, uvivu au kutokuwajibika nk) je hayo yatatibu yote hayo? Tufikiri kwa kina kwanza hapa, inachukua miaka mingi katiba kurekebishwa, tufikiri kipi ni tiba haswa?
Kwa kiasi fulani yes, katiba mpya itakayotoa haki, uhuru na uwajibikaji ndio msingi na tiba bora ya matatizo karibu yote hayo. BAK yuko sahihi. Ubinafsi, ufisadi, uvivu, kukosa uzalendo,sifa, kujikweza nk, vyote ni sehemu ya tabia ya mwanadamu yanayotokana na utashi wa akili yake au mazingira aliyoishi au anayoishi. Katiba moja kati ya jukumu lake kubwa ni kuondoa na kuzuia/limits matumizi ya akili inayotoa utashi wa kufanya mambo hayo. Kwasababu katiba itabainisha mipaka kwa kila kitu hapo.

Angalia kilichotokea Brazil au Korea.
Hisia za rushwa zilipowafikia wananchi, na kubaini kuwa watu hao waliruhusu matumizi ya akili zao kinyume na maslahi ya taifa haikuwa shida kuwakumbusha( kupitia mfumo wa kuwaondoa uliowekwa na katiba zao).

Akili za kibinaadamu ikiwa pamoja na ubinafsi, wizi, matumizi yasiyofaa ya madaraka, uzinzi nk-nk yote yanahitaji sheria ambayo ni deterrence, punishable and enforceable bila kubagua nani au wa cheo gani. Uchaguzi ni moja kati ya deterrence and punishment ambapo wananchi wakiona hawaridhishwi na usimamizi wa wenye dhamana, wanatumia sanduku la kura kuwaadhibu na hivyo walio madarakani kwa kuogopa kuadhibiwa wanalazimika kuwajibika ipasavyo. Kwa msingi huo, ikiwa wanaopaswa kuadhibiwa kwa sanduku la kura wanajua hawawezi kuadhibiwa, uchaguzi unakuwa si deterrent tena na unakuwa hauna maana yoyote.

Kiongozi yoyote mwenye mema na anachokiongoza, mpime kupitia utayari wake wa kuondoka/kuachia madaraka. Ukiona kiongozi anaweka mifumo complex (na isiyoendana na uwajibikaji) ya yeye kutoondoka madarakani, hapo inabidi ujenge shaka kubwa, WHY? Kiongozi anatakiwa aruhusu wapiga kura waamue, na maamuzi yao yabaki hivyo hata kama kura zutahesabiwa mbele ya Malaika au Mungu muumba wa vyote.


Hivyo tume ambayo inaamua kwa haki matokeo ya wapiga kura ni jambo ambalo muhimu, kinyume cha hapo itakuwa tunajiongopea wenyewe na matatizo yote hayo hayatapungua abadan wachilia mbali kuondoka.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Magufuli ndio mwenye enzi Mungu? Sijakuelewa
Nope. ..rais wetu sio Mwenye Enzi Mungu. ..nimesema hakuna kinacho mshinda the Almighty Sovereign Supreme Creator of the universe. ....labda hapo umenielewa. .
UWE NA SIKU KUU NJEMA
 
Hapana, sio wote! Pamoja na yote lakini shida ipo pia katika economic policy management ya awamu hii. Seems like we are under "illusionary budget". Kwa msingi huo, economic principles zinazotakiwa kutekelezwa chini ya mwemvuli wa bajeti hazitaleta matunda wala manufaa. Sijui unanielewa?
Siwezi kukielewa kwa kuwa watanzania ni wavivu wa kufikiri na niwepesi wa kulaumu tupo kama watoto wadogo pale anapoachishwa ziwa na mama yake atalia saana akidhani ameonewa kumbe laa hasha

***** ampenda sana lakini kutokana wakati anatakiwa apitie hatua nyingine, sie Rais kwa jinsi alivyoikuta nchi kwa jinsi ilivyokuwa hata malaika angepewa asingeweza angerudi atokako

Alitukuta tunajifunza kutambaa huwezini niambia unataka kukimbia wakati hata kutambaa unatambaa na tumbo hiyo ni ndoto

Hata huyo aliyekuwa Rais wa libya hayo mafanikio aliyapata baada kuinyosha nchi na wale viherehere wakina tomaso ambao kila saa walitaka kushuhudia kwa macho aliwanyoosha kweli kweli ndio hatua aliyoifikia mpaka libya ikaitwa libya ya Gadafi kasome historia alivyoanza
Na minafiki ambayo leo ndio inajutia ndio iliyojanzwa upepo na kwa kutokujua ndio iliyoifikisha libya leo hapo ilipo
Mimi nina imani na Rais tena saana hata roma haikujengwa kwa siku moja wapo watakaoumia lakini nchi ikasonga mbele

Tusiwe wepesi wa kulaumu tuwe wepesi wa kusaheme kuombeana na kutakiana kheri hapo Mungu atakaa kati yetu na kutupa maarifa ili Taifa liweze songa mbele nina imani kwa pamoja tutaweza
 
Siwezi kukielewa kwa kuwa watanzania ni wavivu wa kufikiri na niwepesi wa kulaumu tupo kama watoto wadogo pale anapoachishwa ziwa na mama yake atalia saana akidhani ameonewa kumbe laa hasha

***** ampenda sana lakini kutokana wakati anatakiwa apitie hatua nyingine, sie Rais kwa jinsi alivyoikuta nchi kwa jinsi ilivyokuwa hata malaika angepewa asingeweza angerudi atokako

Alitukuta tunajifunza kutambaa huwezini niambia unataka kukimbia wakati hata kutambaa unatambaa na tumbo hiyo ni ndoto

Hata huyo aliyekuwa Rais wa libya hayo mafanikio aliyapata baada kuinyosha nchi na wale viherehere wakina tomaso ambao kila saa walitaka kushuhudia kwa macho aliwanyoosha kweli kweli ndio hatua aliyoifikia mpaka libya ikaitwa libya ya Gadafi kasome historia alivyoanza
Na minafiki ambayo leo ndio inajutia ndio iliyojanzwa upepo na kwa kutokujua ndio iliyoifikisha libya leo hapo ilipo
Mimi nina imani na Rais tena saana hata roma haikujengwa kwa siku moja wapo watakaoumia lakini nchi ikasonga mbele

Tusiwe wepesi wa kulaumu tuwe wepesi wa kusaheme kuombeana na kutakiana kheri hapo Mungu atakaa kati yetu na kutupa maarifa ili Taifa liweze songa mbele nina imani kwa pamoja tutaweza
Should be a joke!
 
gadaff kitu gani..??mmesahau wakati wa vita na uganda?au kwa vile aliwajengea misikiti?wanafiki
gadaff kitu gani..??mmesahau wakati wa vita na uganda?au kwa vile aliwajengea misikiti?wanafiki
Sio msikiti tuu
Alitupa mafuta ya bure tulipokuwa hatuna fedha za kigemi
Ametusaidia bajeti
Kina Membe mpaka Leo wanagombea fedha zake alizokuja kuwekeza
 
Back
Top Bottom