Tukiweka siasa nje Rais Barack Obama ni moja ya watu waungwana sana!

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,644
Ana madhaifu mengi kama binadamu, alifanya makosa kama binadamu lakini ukimfuatilia vizuri huyu Mzee utatambua kwamba ni moja kati ya watu waungwana mno.

Kuna baadhi ya mambo mabaya alikuwa anafanyiwa nadhani ni vigumu binadamu wa kawaida kuyachukulia kirahisi au hata kuyapuuza. Mtu wa kawaida tena mwenye mamlaka makubwa ukizomewa na mtu mmoja wakati unatoa hotuba nadhani ni lazima utatoka nje ya mstari kwa hasira tu.

Lakini huyu mzee kuna mambo makubwa ambayo aliyachukulia kawaida sana, nadhani ni watu wachache sana wenye mamlaka wanaweza kufanya kama yeye alivyofanya. Huu ni uungwana wa hali ya juu sana. Ukitazama video ambayo nimeambatanisha hapa nchini nadhani kuna kitu cha kujifunza.

 
Uungwana...?, Jamaa kaua raia wengi sana wa Pakistan, Somalia, Yemen,Iraq,Syria maana akiwa Ikulu matumizi ya 'drone' yaliongezeka maradufu na kusababisha maelfu ya vifo kwa raia wema.

Labda kuna maana nyingine ya uungwana.
 
Uungwana...?, Jamaa kaua raia wengi sana wa Pakistan, Somalia, Yemen,Iraq,Syria maana akiwa Ikulu matumizi ya 'drone' yaliongezeka maradufu na kusababisha maelfu ya vifo kwa raia wema.

Labda kuna maana nyingine ya uungwana.
 
Sitamsamehe kwa kuiharibu Libya ,nchi ilikuwa na amani lakini katika utawala wake akiwa amiri jeshi mkuu yeye ndie mshika bendera wa ile vita ya kidhalimu na kifisadi dhidi ya Ghadaffi
 
Kwangu mimi huenda Obama ndio Rais Muungwana zaidi kuwahi kutokea katika kizazi hiki hapa duniani. Wamerekani hawakukosea na wala hawakubahatisha kumchagua kuwa rais wao kwa vipindi viwili mfululizo.
 
Sitamsamehe kwa kuiharibu Libya ,nchi ilikuwa na amani lakini katika utawala wake akiwa amiri jeshi mkuu yeye ndie mshika bendera wa ile vita ya kidhalimu na kifisadi dhidi ya Ghadaffi
Siku zote kumbuka tu, Obama alikuwa ni rais wa Marekani, alichaguliwa kuwaongoza wamerekani, na siku zote wamarekani hawana huruma wakiwa wanasaka maslahi yao.

Kabla ya kuivamia Libya na kumuua Ghadafi, tayari mabunge yote mawili (senet na congress) ya USA yalipitisha azimio la kuivamia Libya na kumtoa Ghadaffi. Pona ya Ghadafi ilikuwa ni kujisalimisha tu. Usitegemee Obama angeenda tofauti. Never.
 
Usitegemee Obama angeenda tofauti. Never.
Angejiuzulu urais kama kweli ni muungwana kwa kiasi tunacholazimishwa kuamini.

Najua mleta mada analengo la kupima kama tumesahau ubaya uliofanywa na mataifa tunayoaminishwa ni ya kidemokrasia, haki, utu na mengine ya namna hiyo !
 
Ana madhaifu mengi kama binadamu, alifanya makosa kama binadamu lakini ukimfuatilia vizuri huyu Mzee utatambua kwamba ni moja kati ya watu waungwana mno.

Kuna baadhi ya mambo mabaya alikuwa anafanyiwa nadhani ni vigumu binadamu wa kawaida kuyachukulia kirahisi au hata kuyapuuza. Mtu wa kawaida tena mwenye mamlaka makubwa ukizomewa na mtu mmoja wakati unatoa hotuba nadhani ni lazima utatoka nje ya mstari kwa hasira tu.

Lakini huyu mzee kuna mambo makubwa ambayo aliyachukulia kawaida sana, nadhani ni watu wachache sana wenye mamlaka wanaweza kufanya kama yeye alivyofanya. Huu ni uungwana wa hali ya juu sana. Ukitazama video ambayo nimeambatanisha hapa nchini nadhani kuna kitu cha kujifunza.


Sijawahi kumkubali huyu orator.
 
Obama alipenda vita sana,visingizio vya alichaguliwa na wamarekani mara mabunge yalitoa msimamo haina mashiko mbona trump hakumpiga kiduku pamoja na mikwara yote ile ina maana mabunge ya marekani yalikua hayapo?
 
The Best President. Hearts of Majority Americans still with Obama.
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom