Uchaguzi 2020 Tukiwanyima CCM kura tutaingia kwenye kitabu cha Historia ya Ukombozi

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Tunawasoma watu maarufu waliopingana na uonevu wa wakoloni wakatuletea ukumbozi. Waliofanya hayo walianza kwenye sanduku la kura 1958 na 1961 wakaingia ikulu na mzungu akafungasha virago.

Toka 1961 Hadi leo kwanini tunawakumbuka na kuwashukuru? Ni kwa sababu watu waliamua kutotawaliwa, kuminywa haki zao na mateso mbalimbali

Leo 2020 tunapaswa kuandika historia tuwaachie watoto wetu historia, tufanye maamuzi ya kuifuta ccm tuanze upya maisha yetu.

Uchaguzi Ni fursa ya ajira kwa wasio na ajira, Ni fursa ya biashara na fursa yakutengeneza watu wapya tunaoweza kuwasimamia. Leo chama Tawala hakifanyi kampeni kwa juhudi na ratiba ya tume kwa sababu hawaoni umuhimu wetu.

Kama hawaoni umuhimu wetu sisi tunawaonaje wa muhimu kwetu? Wapo waliofadhili kampeni 2015 wapo segerea bila kesi kusikilizwa, wapo watumishi wa Umma walikua ccm kindakindaki wapo benchi na pressure juu. Tunapaswa kuchagua utawala wa sheria.

Tuamue bila kujali chama tujali Uhuru wetu wakujitawala.
 
Mwaka huu lazima itawekwa historia. Maana Magufuli amewadharau sana watanzania ktk kipindi cha miaka 5 iliyopita.
Sema amekudharau wewe, mmeo watoto wenu kwa sababu mnafanya biashara haramu..na madili..rudini njia kuu na nyie walau mlipe kodi na kuchangia maendeleo ya nchi kwa kufanya biashara halali
 
Sema amekudharau wewe, mmeo watoto wenu kwa sababu mnafanya biashara haramu..na maadili..rudini njia kuu na nyie walau mlipe kodi na kuchangia maendeleo ya nchi
Umeona nyomi za Lissu kote anakopita mpaka kwa dada zake na jiwe (a.k.a nyoko) mfano Chato, Lamadi, Bariadi,. Simiyu, Mwanza, n.k.

Hii Ni ishara kwamba huyu nyoko hastahili heshima. Amelinajisi taifa.
 
Umeona nyomi za Lisu kote anakopita mpk kwa dada zake na jiwe (a.k.a nyoko) mfano Chato, Lamadi, Bariadi,. Simiyu, Mwanza, n.k.

Hii Ni ishara kwamba huyu nyoko hastahili heshima. Amelinajisi taifa.
Kwani Magufuli hana nyomi?. Mbona lowasa, Mbowe, Slaa walikuwa na wafuasi kama wa Lissu tu sasa mbona hawakushinda.

Kwa taarifa yako, chama cha Mbowe kinakwenda kufutiliwa mbali na wananchi, tuone hiyo jeuri yake ya kutafuna ruzuku na michango ya wabunge pamoja na kula vitu maalum ataitoa wapi. Kazi mnayo.
 
Hiiiiii.........kuna watu bado wanafikiria kwamba madaraka yanatolewa kwa kipande cha karatasi tu..........
 
KANU kule Kenya walikuww na mawqzo mganndo kama wwwe.Leo hii haipo kwenye ramani ya dunia.
Screenshot_20201016-214914_Samsung Internet.jpg
Screenshot_20201016-214616_Samsung Internet.jpg


Ngojeeni kanzu mtakalopigwa tarehe 28
 
Back
Top Bottom