Uchaguzi 2020 Tukishafikia hapa hatuiti tena kampeni za kistaarabu

onjwayo

JF-Expert Member
Apr 8, 2020
1,346
1,303
Amani na utulivu huvunjwa na wahubiri wake. Inapotokea mhubiri akatoa hubiri kusisitiza jambo halafu yeye akaenda kinyume chako basi matokeo lazima yawe hasi. Ukihubiri amani halafu ukaanza kuwa katili unaowahubiri watakuwa wakatili kuliko wewe. Tujifunze kuishi maneno tunayatamka kwenye mahubiri.

Kampeni zilizoanza jana ziwe za kistaarabu na amani. Polisi wafuatilie hao vijana wanaosadikiwa kuandaliwa kuteka ,kuua na kuumiza watu. Sera na ilani safi siyo kulaximisha na kutoa roho za watu. Vyombo huru za habari kemeeni la sivyo wanasiasa wanaweza kuchoka na kutoa matamko ya kulipiza kisasi. Mbona viongozi wetu mnatupeleka kubaya. Kama wewe ni DC unawatumia vijana kumfurahisha aliyekuteua basi ujue sisi hatufurahishwi na wala hatupendi kuumizwa. Tufanye kampeni kwa amani

FB_IMG_15986662653452481.jpg
 
Mungu muumba mbingu na ardhi,
Naikabidhi nchi yangu mikononi mwako,
Nchi hii kwasasa ipo katika mchakato wa uchaguzi mkuu,
Kila anaepanga kufanya baya, hila, kuua, uonevu, ukandamizaji, wizi, ubabe na mengineyo yasiyofaa kwenye uchaguzi mkuu,
Mungu nakuomba, ikikupendeza, mtu au watu hao, roho zao na uzichukue 2020 hii.
Ili kusudi wasije wakajivunia matunda ya uonevu wao.
Amina, Amen.
 
Tunathibitishaje kuwa majeraha hayo yanatokana na masuala ya kisiasa? Acheni kuanzisha nyuzi zenye lengo LA kuamsha hisia za chuki na ugonvi namna hii!

Huenda ni kweli ila kwa kutoonesha kiashilia cha kisiasa kwenye majeraha kwangu naona umemkosea uliyempost picha yake!
 
Back
Top Bottom