Tukipiga marufuku majenereta na matanki ya "SIMS", tutatatua tatio la umeme na maji

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Mnafikiri ni kwa haraka kiasi gani watawala wetu watajaribu kutatua tatizo la umeme na maji endapo majenereta na matanki ya maji yatapigwa marufuku mijini? I bet you very soon...wouldn't you agree?
 
Ni kweli tangu 1994 wakati wa mgawo mkuu wa umeme, ndo watu walipogundua kuwa majenereta ni dili. Lakini naamini kuwa kupiga marufuku majenereta hakutaondoa tatizo la msingi la wabongo la ufisadi. Utapiga marufuku watabuni mbinu nyingine ya ufisadi.
 
hofu yangu ni kuwa matajiri na watu wenye uwezo hawasumbuliwi na tatizo la nishati na maji kwa sababu they can afford the alternative...
 
Mnafikiri ni kwa haraka kiasi gani watawala wetu watajaribu kutatua tatizo la umeme na maji endapo majenereta na matanki ya maji yatapigwa marufuku mijini? I bet you very soon...wouldn't you agree?

Kuna mambo mengi yanayofanana majenereta na matanki ya maji. Kukiwa na matatizo ya shule, mtu anatafuta pesa ampeleke mtoto wake shule nzuri ya kulipia. Wakati wa zamani shule ya kulipia walikwenda waliokosa nafasi shule za umma. Barabara zikiwa mbovu, mtu anataka kununua SUV, shangingi. Na vitu vingine vinasababisha sehemu fulani ya inflation.
 
Mnafikiri ni kwa haraka kiasi gani watawala wetu watajaribu kutatua tatizo la umeme na maji endapo majenereta na matanki ya maji yatapigwa marufuku mijini? I bet you very soon...wouldn't you agree?

Wa kuyapiga marufuku ni nani kama si hao hao watawala wenyewe?
 
HAITAKAA IWEZEKANE BANA!!

Tanzania bila ya ufisadi na rushwa hiawezekani (hasa kwa serikali hii ya JK)
 
Kuna mambo mengi yanayofanana majenereta na matanki ya maji. Kukiwa na matatizo ya shule, mtu anatafuta pesa ampeleke mtoto wake shule nzuri ya kulipia. Wakati wa zamani shule ya kulipia walikwenda waliokosa nafasi shule za umma. Barabara zikiwa mbovu, mtu anataka kununua SUV, shangingi. Na vitu vingine vinasababisha sehemu fulani ya inflation.


unajua kama jua haliwapigi wao unafikiri wanasumbuka kuona wengine wanapata vivuli? Mimi naamini ni kama template fulani hivi inatumika. Yaani, kwa mfano lile la taasisi ya Moyo.. shule zetu na hata kwenye jeshi la polisi.. can you imagine kuna mashirika ya kuzima moto ya binafsi yanayofanya kazi ya umma kwa malipo? Hata Polisi imefikia kuwa na ubinafsishaji wa aina fulani..
 
unajua kama jua haliwapigi wao unafikiri wanasumbuka kuona wengine wanapata vivuli? Mimi naamini ni kama template fulani hivi inatumika. Yaani, kwa mfano lile la taasisi ya Moyo.. shule zetu na hata kwenye jeshi la polisi.. can you imagine kuna mashirika ya kuzima moto ya binafsi yanayofanya kazi ya umma kwa malipo? Hata Polisi imefikia kuwa na ubinafsishaji wa aina fulani..

Hiyo ni template na ambayo ina-negative impact kubwa sana kiuchumi. Mtu mmoja anapokuwa na jenereta na akaongeza comfort yake, basi hata jirani yake ambaye kipato chake sio kikubwa atataka kuwa na jenereta. Hivyo jirani ataiba au kwa lugha ya sasa kufisadi kwa kiwango cha chini. Na ununuzi wao utaongeza demand ambayo itafanya atokee supplier ambaye atatumia pesa ya kigeni kuagiza jenereta kutoka nje ya nchi. Matokeo ni kuongeza demand ya dollar na kuwa na currency ambayo sio stable.

Kwa maoni yangu binafsi sioni sababu ya form six anayefanya TRA kupata mshahara mkubwa kuliko university professor. Ukiangalia kwa undani hili mtu wa TRA asiibe inabidi alipwe mshahara utakaomwezesha kununua simm tank, jenereta n.k

Na kuhusu wao kutopigwa na jua, huo ni ulimbukeni tu.
 
Fikiria mlolongo wa hili ulivyo:

Nunua jenereta
Nunua mafuta
Nunua spare parts


Lakini jingine ni kuwa unaweza ukakuta nyumba ina jenereta kubwa na lina uwezo hata wa kugawa umeme kwa jirani lakini hakuna utaratibu ambao ungeweza kuhakikisha utaratibu wa kuunganisha majirani. Matokeo ni kuwa jirani na jirani wana umeme wa kutosha kwenye majenereta ambao wangeweza kutangeneza hata ka network fulani hivi.. maana nimewahi kuona jamaa anayo yale ma industrial generators kwa matumizi ya nyumbani..
 
Swala la nishati na madini linaendeshwa kisaani humu nchini kwetu hadi hapo tutakapo kurupuka na kujua ni kipi cha kufanya. Bila kuitikisa seriklai ni sawa na kutwanga tu maji kwa kinu. Sera ni mbovu hazi wezi kutuletea maendeleo kamwe Umeme utakuwa wa mgao tuu siku zote mfano mzuri mpaka leo watanzania wengi hawajui chanzo cha mgao huu bali wachache wanasikila kuwa kuna tatizo la vipuli vimeharibika huko Dar sasa kwanini huku mikoani tukumbwe na hilo tatatizo la umeme je ingekuwa ni mwanza wana tatizo hilo je Dar wange wekwa kwa mgao nao???

Kama Tanesco wanashindwa tuu kuagiza Transformer tokea Tanelec Arusha ambako zinatengenezwa na kubadirishi ile iliyo haribi mfano hapo masaki labda ianawachukua miezi 2. Haliingii akilini kabisa
 
Proposal iliyoko kwenye title ya thread inaangalia zaidi symptoms. Is it sustainable? Not quite...I will say.

Mzuie mlevi kunywa bia..... atatengeneza gongo mwenyewe (uliza watu wanaoishi maeneo fulani kule UAE).
Mlevi hata petroli atakunywa.

Solution ya tatizo hili is one radical bing-bong....so for starters, ditch those pretenders currently occupying that Magogoni house.
 
interesting thinking...ivi umeme kutoka makampuni binafsi ni marufuku?
sidhani kama ku-ban majenereta itawezekana!dawa ni kuja na alternative means ya ku-dili na hii ishu! kuanzisha kampuni binafsi inaweza kuwa moja ya alternatives!
 
Mi mwenyewe na mpango wa kuanzisha duka la vifaa vya majenereta Dar nzima hakuna likiloga ndo basi tena.
Kufa kufaana hapo
 
Swala la nishati na madini linaendeshwa kisaani humu nchini kwetu hadi hapo tutakapo kurupuka na kujua ni kipi cha kufanya. Bila kuitikisa seriklai ni sawa na kutwanga tu maji kwa kinu. Sera ni mbovu hazi wezi kutuletea maendeleo kamwe Umeme utakuwa wa mgao tuu siku zote mfano mzuri mpaka leo watanzania wengi hawajui chanzo cha mgao huu bali wachache wanasikila kuwa kuna tatizo la vipuli vimeharibika huko Dar sasa kwanini huku mikoani tukumbwe na hilo tatatizo la umeme je ingekuwa ni mwanza wana tatizo hilo je Dar wange wekwa kwa mgao nao???

Kama Tanesco wanashindwa tuu kuagiza Transformer tokea Tanelec Arusha ambako zinatengenezwa na kubadirishi ile iliyo haribi mfano hapo masaki labda ianawachukua miezi 2. Haliingii akilini kabisa

Wala tatizo si transformer mkuu hii ilikuwa ni kisingizio cha kwanza, jana nilimsikia msemaji wa Tanesco dada mmoja nafikiri ni Badru Masoud kama sikosei. Sababu alizozitoa zinakatisha hata tamaa, mgao si wa leo wala kesho, huu tunao na huenda tukamaliza nao mwaka.


 
interesting thinking...ivi umeme kutoka makampuni binafsi ni marufuku?
sidhani kama ku-ban majenereta itawezekana!dawa ni kuja na alternative means ya ku-dili na hii ishu! kuanzisha kampuni binafsi inaweza kuwa moja ya alternatives!

Naungana nawe Chapakazi, dawa ni kuishinikiza Serikali iache ukiritimba kwenye huduma hii, iruhusu makampuni binafsi yaingie, yazalishe na kusambaza umeme kama zilivyo kampuni za simu! Haja jeuri ya TANESCO itakwisha kama TTCL!
 
ni maajabu sana, kuwa badala ya wenye bajeti kuimarisha zimamoto, wanakodisha binafsi ha hela ya kulipa inapatikana!!! haya yanawezekana Tanzania tu!! nikati ya sife zetu maalum za pekee
 
Toka lini serikali yetu ikawa na ufanisi kwa lolote? Hata wakiamua kupiga marufuku (kwa raia) wala hawatafanikiwa kuleta umeme wala maji na haitapita muda wataacha hayo majenerata na matanki yarudi kinyemela. Labda ni pale tu watapojua kua bila luleta umeme na maji watakosa kushika serikali, lakini ubabe wao bado unawahakikishia kushika serikali.
Inanikumbusha historia yetu pale ambapo mashamba ya binafsi yalipopigwa mkwara ili mashamba ya vijiji yaendelee - bado vijiji havikuimarika.
 
ni maajabu sana, kuwa badala ya wenye bajeti kuimarisha zimamoto, wanakodisha binafsi ha hela ya kulipa inapatikana!!! haya yanawezekana Tanzania tu!! nikati ya sife zetu maalum za pekee

Si ajabu, wanasababu nzito na watakuambia FIRE wanaiba spea na mafuta. Kazi ya kukodi ni rahisi kuliko kazi ya kusimamia kuimarisha hizo zimamoto.
Chukulia kua pesa ipo: Pia ni kazi rahisi kufikiria na kuchimba visima vya maji Dar kuliko kujenga mtandao wa mabomba ya mji toka Mto Ruvu ama Rufiji, pia rahisi kufikiria na kununua SUV ili waheshimiwa waweze kupita kwenye barabara zisizopitika. Ndivyo walivyo kwenye serikali yetu ama ndivyo tulivyo - tunapenda kilicho rahisi kufanya leo ili kupooza tatizo kwa leo, ya kesho tutajua kesho. Ni ubinafsi pamoja na akili finyu katika kuendesha shughuli zetu.
 
Mnafikiri ni kwa haraka kiasi gani watawala wetu watajaribu kutatua tatizo la umeme na maji endapo majenereta na matanki ya maji yatapigwa marufuku mijini? I bet you very soon...wouldn't you agree?

...Wakati kampeni zinaanza, kuna jamaa alidai ataipigia kura ccm, ili aendelee kuuza maji ya kisima alichochimba.

...Point yake ikiwa;ku-maintain status quo kunampa ulaji mzuri.
 
Ni kufikiria jinsi gani jamii hasa watendaji wetu wakubwa wa serikali ambao kwao umeme siyo tatizo wala maji siyo tatizo wataona umuhimu wa kutafuta suluhisho? Watu binafsi sina tatizo kabisa wao wanapata vipi umeme lakini watendaji wa serikali (nafikiria wale wa Tanesco) hili kweli hawana majenereta majumbani kwao na hivyo umeme unapokatika wao wenyewe haiwagusi?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom