Tukio la Kesho Arusha linanikumbusha sinema ya SARAFINA, na mapambano kule S.Afrika.

King Suleiman

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
496
327
Habari zenu wana jamvi,

kesho ni siku ya kuwaombea na kisha kuwazika mashujaa waliouwa wakati wa maandamano ya Amani na mkutano wa Amani ulioandaliwa na Chadema tar. 5/1/11, ni msiba mzito sana kwa wana Arusha na watanzania wote kwa ujumla wale wapenda haki na amani.

katika muv ya Sarafina askari wa kikaburu waliwaua vijana wapigania uhuru na kujeruhi wengi, baada ya siku kadhaa walifanya ibada na kuwazika wenzao. Hakika ni msiba wa kihistoria ambao kwa hakika ulipendeza sana, huku askari wa kikaburu wakiangalia kwa mbali na wanaharakati hawakusita kuwaambia ukweli hata hapo msibani " u may kill all of ths young people but u cant kill their ideas and changes ar comming, freedom is coming tommorrow" alisikika mtu mmoja.

sasa yaliyotokea kwa Sarafina kesho ndio yatatkea kesho Arusha, kwa hakika ni msiba wa majonzi sana lakini ni wa kihistoria na kukumbukwa sana.
"U MAY KILL PEOPLE BUT U MY NOT KILL THEIR IDEAS AND SPIRIT OF CHANGES"
 
Kweli kabisa nafikiri waandaaji watupe muda wa kuimba nyimbo zetu za kishujaa na kupita baadhi ya sehemu za Arusha tukiwa na majeneza ya mashujaa wetu
 
Yamkini ukawa mwanzo wa mageuzi makubwa amabayo hayajapata kutokea tangu Tanzania ianze kuitwa Tanzania.Natumaini waandaaji wa shughuli hii kubwa na muhimu watakuwa wamezingatia mambo yote muhimu yanayopaswa kuwekwa kwenye historia ili vizazi vijavyo visinyimwe haki ya kujua taifa letu lilipotoka.

Ningeomba wanaArusha mtupatie picha za kutosha bila choyo wala zengwe ili wanaJF waliombali na mji wa Arusha wajionee wenyewe jinsi mfalme mwenye kiburi na mikono iliyojaa damu za watu anavyoanza kuanguka taratibu mithili ya theluji inapokumbana na mionzi ya jua.Nilipenda sana nishiriki tukio hili muhimu sana lakini bahati mbaya sana niko mbali kidogo.najua kamanda PakaJimmy ataniwakilisha kwa asilimia zote.
 
Kweli kabisa nafikiri waandaaji watupe muda wa kuimba nyimbo zetu za kishujaa na kupita baadhi ya sehemu za Arusha tukiwa na majeneza ya mashujaa wetu

kama polisi na serikali wasipofanya mazingaombwe yao natabiri msiba wa kesho utaacha kumbukumbu kubwa sana kwenye historia ya nchi yetu. THE TRUE FREEDOM WILL BE MANIFESTED TOMMORROW AT ARUSHA.
 
Mkuu hakuna msiba unaopendeza.

ni kweli ndg yangu B, ila kuna misiba inayovuta hisia za watu kama ule wa Nyerere, Arafat, S.Husein, papa na wengineo. Huu wa kesho utavuta sana hisia za watu, hususan wanamageuzi.
 
Upigwe wimbo kama ule wa maziko ya wanamapinduzi soweto unaofanana na wa Sinema ya Sarafina.
 
Yamkini ukawa mwanzo wa mageuzi makubwa amabayo hayajapata kutokea tangu Tanzania ianze kuitwa Tanzania.Natumaini waandaaji wa shughuli hii kubwa na muhimu watakuwa wamezingatia mambo yote muhimu yanayopaswa kuwekwa kwenye historia ili vizazi vijavyo visinyimwe haki ya kujua taifa letu lilipotoka.

Ningeomba wanaArusha mtupatie picha za kutosha bila choyo wala zengwe ili wanaJF waliombali na mji wa Arusha wajionee wenyewe jinsi mfalme mwenye kiburi na mikono iliyojaa damu za watu anavyoanza kuanguka taratibu mithili ya theluji inapokumbana na mionzi ya jua.Nilipenda sana nishiriki tukio hili muhimu sana lakini bahati mbaya sana niko mbali kidogo.najua kamanda PakaJimmy ataniwakilisha kwa asilimia zote.
Nitakuwepo kiongozi...!

Nimeamua kuwa nitamrudishia mwajiri mshahara wake wa siku ya kesho maana sintokuwepo ofisini!

Haya ni mambo yanayotokea once in a blue moon!...na kama ulivyosema ni kwamba yanaingia moja kwa moja kwenye History-Lane!.

Will give you whatever will transpire!
 
kweli mtu wangu. watu wanadhani tunashindwa kupigania haki yetu! wanachekesha......................!
 
Back
Top Bottom