MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,975
Kwa mtu anayechambua na kuchanganua siasa za Tanzania atakubaliana na mimi kuwa ni vigumu sana kuiondoa CCM madarakani.
Tukio la kuaga Mwili wa Marehemu Kingunge Ngombare-Mwiru limefikirisha zaidi na kunionyesha jinsi ilivyo vigumu sana kuchukua dola kutoka CCM.
Nilimuona Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akipepesa macho huku na kule kwenye eneo la wageni mashuhuli(VIP) lakini kila akiangalia huku na kule alikuwa anakutana na nyuso za wanaCCM wastaafu au waliobado active katika chama na serikali.
Tukio la Freeman Mbowe kuzungukwa na wanaCCM ambao wengi wao ni statesman lilinifikirisha sana kuhusu hatima ya CCM lakini pia majukumu mazito na magumu ya vyama vya upinzani katika kuchukua dola kutoka CCM.
Tukio hili limeondosha shaka kuwa CCM bado ni chama dola lakini pia vyama vya upinzani nchini vina jukumu ambalo liko juu ya uwezo wao. Huu ni ukweli mchungu kwa wapinzani wa kweli nchini.
Kuna baadhi ya watu hupenda kuja na kauli wakisema, kama Roman Empire ilianguka, kwa nini CCM isianguke? Ikumbukwe kuwa kuanguka kwa Roman Empire kulichukua miaka zaidi ya 1000. Ni kweli kuna siku CCM itaanguka lakini kwa upinzani huu sioni kama siku hiyo itatokea.
Tukio hili linatoa somo linalosema, ni bora vyama vya upinzani vikaendelea na siasa za uanaharakati na kupata wabunge lakini sio siasa za kupata dola/madaraka. Bado sana.
Kazi iliyofanywa na waasisi wa CCM katika kujenga msingi wa chama dola itachukua muda mrefu sana kwa wapinzani kuuvunja kwa sabahu hata ambao tunadhani ni wapinzani kumbe sio wapinzani bali ni kama watoto waliochukizwa tu na baba/Mama yao na kususa lakini mahitaji yao yakitimizwa wanarudi nyumbani.
Wakati mwingine kuukubali ukweli wa kimazingira katika maisha yako sio kosa!
Ukitaka kumuona Mbowe alivyokuwa akipepesa macho angalia kuanzia dakika ya 2:50.
[MEDIA]
Tukio la kuaga Mwili wa Marehemu Kingunge Ngombare-Mwiru limefikirisha zaidi na kunionyesha jinsi ilivyo vigumu sana kuchukua dola kutoka CCM.
Nilimuona Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akipepesa macho huku na kule kwenye eneo la wageni mashuhuli(VIP) lakini kila akiangalia huku na kule alikuwa anakutana na nyuso za wanaCCM wastaafu au waliobado active katika chama na serikali.
Tukio la Freeman Mbowe kuzungukwa na wanaCCM ambao wengi wao ni statesman lilinifikirisha sana kuhusu hatima ya CCM lakini pia majukumu mazito na magumu ya vyama vya upinzani katika kuchukua dola kutoka CCM.
Tukio hili limeondosha shaka kuwa CCM bado ni chama dola lakini pia vyama vya upinzani nchini vina jukumu ambalo liko juu ya uwezo wao. Huu ni ukweli mchungu kwa wapinzani wa kweli nchini.
Kuna baadhi ya watu hupenda kuja na kauli wakisema, kama Roman Empire ilianguka, kwa nini CCM isianguke? Ikumbukwe kuwa kuanguka kwa Roman Empire kulichukua miaka zaidi ya 1000. Ni kweli kuna siku CCM itaanguka lakini kwa upinzani huu sioni kama siku hiyo itatokea.
Tukio hili linatoa somo linalosema, ni bora vyama vya upinzani vikaendelea na siasa za uanaharakati na kupata wabunge lakini sio siasa za kupata dola/madaraka. Bado sana.
Kazi iliyofanywa na waasisi wa CCM katika kujenga msingi wa chama dola itachukua muda mrefu sana kwa wapinzani kuuvunja kwa sabahu hata ambao tunadhani ni wapinzani kumbe sio wapinzani bali ni kama watoto waliochukizwa tu na baba/Mama yao na kususa lakini mahitaji yao yakitimizwa wanarudi nyumbani.
Wakati mwingine kuukubali ukweli wa kimazingira katika maisha yako sio kosa!
Ukitaka kumuona Mbowe alivyokuwa akipepesa macho angalia kuanzia dakika ya 2:50.
[MEDIA]