Sir_Mimi
JF-Expert Member
- Jun 21, 2013
- 7,152
- 15,604
Hizi zilitamba sana mwishoni mwa miaka ya 80's na mwanzoni mwa 90's,yaani ndo zilikuwa za kijanja wakati huo na zilikuwa za mpira zinakuwa na mchanganyiko wa rangi.chupi za VIP ndio zikoje mdau ndio nasikia leo aisee
Kipindi hiko kwa sisi tuliotumia utoto wetu shamba ilikuwa ukienda kuogelea mtoni halafu hujawahi kuonekana umevaa hii brand unachekwa so tulikuwa tunalia na wazee mpaka watununulie.
Nakumbuka miaka hiyo siku nikiivaa kuendea shule {maana ilikuwa ya kuendea Kanisani tu} nilikuwa nachomekea shirt upande mmoja ndani ya chupi ili ionekane na wenzangu ila ilikuwa haiwezi kuhimili purukushani ilikuwa ukicheza mpira kidogo tu hauchelewi kuikuta imeshakatika ipo makwapani inang'ang'ana ipande shingoni,wapevu ilikuwa siku hiyo tukivaa tunatulia tulii.