Babaako
Member
- Mar 10, 2016
- 15
- 22
Mimi sio mfuasi wa chama chochote cha siasa na huwa sipendi sana kuongelea siasa lakini huwezi kuikwepa siasa kwa sababu tunaishi kwa kuongozwa na wanasiasa, tunafuata sheria zilizotungwa na wanasiasa kwa hiyo japo sipendi kujihusisha na siasa lakini maamuzi ya wanasiasa yana effect kwenye maisha yetu. Chanzo cha matatizo yote duniani ni siasa. Duniani kote ambako kuna machafuko chanzo ni siasa.
Anyway acha niende kwenye mada moja kwa moja. Kama nilivyoeleza kwenye kichwa cha habari tukiacha unafiki na kusimama kwenye haki rais anapiga kazi. Mnyonge mnyongeni lakini mpeni haki yake. Anachokifanya Magufuri hakuna mtangulizi wake aliyeweza kukifanya.
Tukianzia kwenye ajira serikalini zamani ilikuwa karibia na kwamba haiwezekani kwa mtu wa asiyekuwa na mtu anayemjua kupata kazi nzuri serikalini. Kupata kazi kama tra, wizara ya fedha na mashirika ya serikali ambayo yana maslahi mazuri ilikuwa haiwezekani kwa mtoto wa mkulima asiyekuwa na refa huko juu. Lakini sasa hivi kila mwenye sifa anapata kazi (zinapotangazwa). Ukija kwenye miundo mbinu, japo watu wanabeza, rais anajitahidi sana.
Bila kuboresha miundo mbinu huwezi kukuza uchumi. Magufuri ana vision, ana malengo ya muda mrefu. Watu wanaweza wasione effects za hii standard gauge kwa sasa lakini hii inakuja kuchochea uchumi kwa kasi sana. Nchi zote zilizoendelea zimewekeza pakubwa kwenye miundo mbinu na mawasiliano. Bila miundo mbinu bora kukuza uchumi haiwezekani. Kwa wachumi hilo wanalielewa.
Pamoja na kazi kubwa anayoifanya kuna mapungufu madogo madogo bado yanaendelea kumharibia. Ningependa kuyataja mambo mawili ambayo yanawagusa moja kwa moja raia wa kawaida.
1. Swala la fao la kujitoa kusitishwa hapo anahitaji kupaangalia kwa jicho la tatu. Haiwezekani mtu aishi maisha ya tabu baada ya kuacha kazi wakati hela anayo. Hiyo sio haki hata kidogo. Mtu asipangiwe jinsi ya kutumia hela yake aliyoitafuta kwa jasho. Apewe hela yake aanze maisha mapya. Ukisema asubiri mpaka afikishe miaka 60, unategemea ataifikishaje hiyo miaka bila kufa na magonjwa au stress kwa sababu ya ugumu wa maisha? Mpe mtu mafao yake afanye hata biashara ili ajihudumie yeye na familia yake.
2. Hili sina uhakika nalo sana ila nina imani lipo ndani ya uwezo wake kulifanyia kazi. Siasa sio uadui, kama watendaji wake wa chini wanafanya haya mambo bila ridhaa yake inabidi aliangalie vizuri.
All in all Tanzania haijapata rais kama huyu. Tunaweza tusiyaone matunda kwa sasa ila vizazi vyetu hakika vitakuja kuishi kwenye nchi ya asali na maziwa.
Anyway acha niende kwenye mada moja kwa moja. Kama nilivyoeleza kwenye kichwa cha habari tukiacha unafiki na kusimama kwenye haki rais anapiga kazi. Mnyonge mnyongeni lakini mpeni haki yake. Anachokifanya Magufuri hakuna mtangulizi wake aliyeweza kukifanya.
Tukianzia kwenye ajira serikalini zamani ilikuwa karibia na kwamba haiwezekani kwa mtu wa asiyekuwa na mtu anayemjua kupata kazi nzuri serikalini. Kupata kazi kama tra, wizara ya fedha na mashirika ya serikali ambayo yana maslahi mazuri ilikuwa haiwezekani kwa mtoto wa mkulima asiyekuwa na refa huko juu. Lakini sasa hivi kila mwenye sifa anapata kazi (zinapotangazwa). Ukija kwenye miundo mbinu, japo watu wanabeza, rais anajitahidi sana.
Bila kuboresha miundo mbinu huwezi kukuza uchumi. Magufuri ana vision, ana malengo ya muda mrefu. Watu wanaweza wasione effects za hii standard gauge kwa sasa lakini hii inakuja kuchochea uchumi kwa kasi sana. Nchi zote zilizoendelea zimewekeza pakubwa kwenye miundo mbinu na mawasiliano. Bila miundo mbinu bora kukuza uchumi haiwezekani. Kwa wachumi hilo wanalielewa.
Pamoja na kazi kubwa anayoifanya kuna mapungufu madogo madogo bado yanaendelea kumharibia. Ningependa kuyataja mambo mawili ambayo yanawagusa moja kwa moja raia wa kawaida.
1. Swala la fao la kujitoa kusitishwa hapo anahitaji kupaangalia kwa jicho la tatu. Haiwezekani mtu aishi maisha ya tabu baada ya kuacha kazi wakati hela anayo. Hiyo sio haki hata kidogo. Mtu asipangiwe jinsi ya kutumia hela yake aliyoitafuta kwa jasho. Apewe hela yake aanze maisha mapya. Ukisema asubiri mpaka afikishe miaka 60, unategemea ataifikishaje hiyo miaka bila kufa na magonjwa au stress kwa sababu ya ugumu wa maisha? Mpe mtu mafao yake afanye hata biashara ili ajihudumie yeye na familia yake.
2. Hili sina uhakika nalo sana ila nina imani lipo ndani ya uwezo wake kulifanyia kazi. Siasa sio uadui, kama watendaji wake wa chini wanafanya haya mambo bila ridhaa yake inabidi aliangalie vizuri.
All in all Tanzania haijapata rais kama huyu. Tunaweza tusiyaone matunda kwa sasa ila vizazi vyetu hakika vitakuja kuishi kwenye nchi ya asali na maziwa.
Last edited by a moderator: