2013
JF-Expert Member
- Aug 2, 2011
- 11,358
- 6,059
kumekuwa na tabia ya wenye kusimamia kiswahili kulazimisha kuweka maneno ya lugha za mpya katika kutika kuongeza msamiati wa lugha ya kiswahili, mfano maneno kama ngamizi ya kupakata na ngamizi ya mezani, rununu , kikokotozi. tatizo ninaloona hapa ni kuwa maneno haya hayaendani na uwezo wa kiteknolojia wa tamaduni husika za waswahili pia haizendani na watumiaji/walaji wa lugha hii, hivyo yanabakia kuwa ni sehemu ya lugha lakini hayatumiki katika maisha ya kila siku ya wananchi wa kawaida. kwa lugha ili iendelee inahitaji ustaarabu, yaani kuheshimu teknolojia ya mwingine kupitia kutumia maneno ya wengine yanayoonekana kwepo katika jamii. mabadiliko ya kitechnolojia yanakwenda kasi mno siku hizi mfano kuna 4K television, google glass si vizuri kutafuta maneno ya kiarabu ama ya kienyeji yasiyotumika na kujifanya tunaijua saaana technolojia ya wenzetu kwa kupachika majina yetu yasiyo na haki miliki kwa kifaa husika. ajabu zaidi ni pale kukuta maneno ya kingereza kama computer(kompyuta=kwa kiswahili) yangeweza kutumika na kuongezwa katika lugha lakini yanaishia kuonekana sio maneno ya kiswahili bali ya kigeni lakini cha ajabu ni pale maneno yanayotokana na juzuu na kiarabu yanakubaliwa kuwa ni ya kiswahili wakati hata lafudhi ya kuyatamka tu ni shida tupu kwa wengi wetu. nadhani hapa wataalamu wa lugha wangejipanga freshi kujaribu kutotuchanganya watumiaji, kwani najua wanachokiandaa ni kwaajili ya watumiaji na sio maslahi yao binafsi. hakuna mswahili aliyegundua laptop wala simu ya mkononi, tuache kuchakachua. na pia kiarabu sio kiswahili tusichanganyane hapa.