Tujuzane machimbo ya Mafuta ya Kupikia ya bei nafuu Dar Es Salaam

Cachondo

Senior Member
May 6, 2019
144
139
Habari za muda huu wachakalikaji?

Kama kichwa cha habari kinavyoeleza hapo juu, sisi kama watafutaji na wafanyabiashara wa mafuta ya kupima na kuwauzia wakaanga mihogo, samaki, chipsi na wengine wanaoyatumia kwa sana tunafeli kutokana na bei za mafuta kuwa juu sana na kupelekea kuwapandishia hao akina baba na mama zetu wanaoyahitaji sana kitu kinachopelekea kutopata faida au kula hasara moja kwa moja.

Huku kwetu Kimara dumu moja la lita 20 sasa hivi ni 60,000 Mpaka 57,000. Madukani reja reja kwa lita ni 3,500. Bei hii ni kubwa sana kwa muuza mihogo na chipsi.

Karibuni tujuzane bei za huko kwenu bei za mafuta kwa jumla na rejareja.

Karibuni ndugu zangu.
 
Wakuu Mimi Nina mafuta Safi ya kupikia sunflower yanaitwa NADIR LITA 5 NAUZA SH.25000(yanatoka Uturuki)nipo Zanzibar kwa Dar nakuletea Hadi ulipo kuanzia katoni 10. Punguzo lipo ukichukua kuanzia katoni 20. Karibuni. Njoo inbox
 
Back
Top Bottom