Tujuzane kuhusu E-commerce [Maswali, Shuhuda, Ideas]

Nikianza na mimi,

Main issue ni programming/graphics na web design. Baada ya hustle za muda mrefu kidogo, nilicreate ki Branding Agency (15 Men Team) ambako nlipewa kuifanyia Re-Branding, E-Commerce store ya majamaa wawili, walikuwa ndugu, mtu na mdogo ake.

Ile kupewa access, nikakutana tu na mi graph ya mapato, matumizi, visitors, products in stock, in sale, in auction. Na walikuwa wanakimbiza atleast $25-30 sales per day. Walikuwa wanauza viatu, so nikawa na interest kuulizia, ulizia nikapewa dry answers ikabidi nikafanye research zangu mwenyewe.
 
Kufupisha story, nimekuwa na store inayoship kwa nchi 25, bidhaa mbali mbali za kiume. Huu ni mwaka wa pili, na challenges zipo kibao, japo na matunda yanaonekana soon yataanza kulika.

Operation Plan:

Hii nimei re-modify kama mara kumi ivi. Mwanzo, nlikuwa nataka niwe na physical products ambazo mtu akinunua online namtumia, sikuwahi uza.

Plan 2, niingie partnership na maduka mbali mbali kama dalali anaesaidia kutangaza bidhaa zao. Hapa nliuza kidogo mno, sales kama 12, ndani ya miezi minne.

Nikaanza nikaachana nayo, siku zikasonga, ndipo wale jamaa wakataka tena Rebranding, na naona data zao n wanazid kupanda tu. So ikabidi niwafuatilie kidogo. Nikajaribu nunua kwa store yao, nikaambiw my country ain't supported.
So walikuw na nchi specific wanauzia. Nikaingia kitabuni kwa mara nyingine na baada ya majaribio ya hapa na pale ndipo nikaja na Operation plan nnayotumia hadi sasa
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Current Operation Plan;

1. Ilibidi issue nzima ilwe serious na legal. So nikasajili jina la biashara Brela, nikapata pass TRA, ya kampuni tu la kawaida.

Then haiishi hapo, unaenda kwa kila nchi unakoenda kuuzia, zile za msingi, unasajili kampuni. Aim kubwa ni upate Postal Address. So in m case ilikuwa USA, CA na FR.

2. Ilibidi niingie partnership na manufactures wawili wanaopokezana kwa miezi. That means huu mwezi anaproduce huyu, na huu mwezi huyu. Mchina anaamini uko serious ukishafanya order ya stock unayotaoa.( Piece 500 za kuanzia)

Partnership haina mengi, mnachokubaliana ni kuwa; ataziekea bidhaa zote logo ako, lakini manufactured in China. Then atafanya packaging.

3. Delivery nafanya na E-Packet, so ni faster na nafuu kidogo.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
So manufucture ananipa 3d model za kila bidhaa inayotoka kwake, ikiwa na logo angu. Then mimi naamua pricing na kueka kwa store.

Order zote za wiki zinakuwa forwarded kwa manufucture kila J4 na JMos. So Mteja anapata mzigo wake in 5 days max/min. Na E-Packet.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Mimi nimeshawahi kutengeneza classified ads hii ishu ni rahisi sana kupata wateja na mapato kwa haraka kama utaiweka vizuri search engine kwenye Google vizuri

Mfano kama una store ya viatu ilikupata waingiaji wengi kwenye store yako nenda kwenye Google angalia watu wengi wanagoogle kitu gani kuhusu viatu hii itakurahishia kutarget waingiaji kwenye store yako
 
Changamoto;
(so far...)

1. Kuuza hakutabiriki. Hii ni changamoto, kuna muda wiki inapita, sales ni zero. Na kuna mda unalamba sales 70 in one week.
Nimejaribu SEO, Backlinking, kuwatumia Instagram Influencers ila bado, soko linakuwa halitabiliki.

Issue inaua zaidi, kwenye kutafuta first sale.

2. Refunds. Hii nime i experience majuzi, ila nayo ni changamoto kubwa. Reputation uliyohangaika kuijenga kwa mwaka mzima unaweza ipoteza kwa malalamiko ya mteja mmoja anaetaka kurudishiwa hela ake.
Hii inahesabika kama 100% loss, maana hela unaitoa, na bidhaa inarudishwa kwa Virtual Address ulonunua. In short inaishia posta.

3. Kupokea malipo. Changamoto kabambe, ni hii. Ili store iende itahitaji namna kama 20 hivi za kupokea malipo, kama huduma utakuwa unawapea watu wa nje. Providers wengi hawasapoti nchi ya Tanzania, so itabidi uumize kichwa namna ya kupata Verified Account haswa ya Stripe.

4. Exposure. Unaweza hustle na matangazo ya FB, Insta na Google, na bado store yako ukabakia kuifahamu na mkeo.
 
Mimi nimeshawahi kutengeneza classified ads hii ishu ni rahisi sana kupata wateja na mapato kwa haraka kama utaiweka vizuri search engine kwenye Google vizuri

Mfano kama una store ya viatu ilikupata waingiaji wengi kwenye store yako nenda kwenye Google angalia watu wengi wanagoogle kitu gani kuhusu viatu hii itakurahishia kutarget waingiaji kwenye store yako
Dadavua zaidi mkuu,
Je hizo classfied ads hawatumii na competitors wako?
 
Kwa Faida

1. Baada ya muda Store itajiendesha.
Utakuwa na jamaa wa kukusevu kama Customer Support, Instagram na kwa Email. Unaeza mlipa fixed amount au kwa kila tatizo atakalo tatua.

Kuhusu kupost kwa Social Media, unaweza automate kila kitu na huduma kama Social Rabbit.

Earnings zako baada ya mda zitakuwa zinatosha kulipia costs zote za uendeshaji, Bando, Domain, Hosting, Team Salary na hata matangazo.

2. Iko scalable ndani ya mda mfupi, now nina exposure ya nchi 25. Nlianza na nchi tatu. Nina partnership na manufactures wawili, nlianza na mmoja. Avg. Weekly sales zilikuwa 2, for the first 5 months. Now ni 22.

3. Similiki stock. Siingii gharama kutengeneza kitu, japo nnauza na vinafika.

4. Wewe ndo unaamua HQ za business yako ziwe wapi.
 
Hihi ni seller panel.

E-commerce nayo develop ina sede 3
1. Customer side - Hapa ndo account ya mtu anawaza kununua, ku-return, history, wishlist's etc
2. Seller Panel - Hapa ni kama ww bwana mwandishi, una upload bidhaa zako nina option 2 (single listing na multiple listing excel inatumika hapa ku upload Multiple) pia unauwezo ka kufungu store zaidi ya moja.
3. Logistic panel
View attachment 1836139

Multiple Currency feature - shukurani kwe django currency exchange

View attachment 1836141

Mfano wa Store page kwa Seller Account pia ina mwonekano tofauti kwa customers side

View attachment 1836142

Ukiachana na CSS3, HTML5, JavaScript, Jquery Font end inmetumia pia react .js

Back-end natumia python (Django Framework)

Storage natumia Azure ya microsoft inanipastorage kwa ajili ya testing

Database natumia PostgreSQL

billa kusahau mkuu Redis
Hii iko vizuri mkuu, kati ya Kutumia CMS kama WordPress, Shopify na ku code from Scratch what's better?
 
One of the great content zilizosoma in a while big up sana mkuu, unachokifanya hakitofautiani sana na dropshipping Sema ile imebase sana watu wanachukua products aliexpress then wanauza kwenye store zao kupitia shopify. Umejiongeza sana kupata suppliers wako na nimependa wanatuma products on weekly basis bonge moja la advantage tofauti na kwingine. Pia kwa kujudge backend UI ya store yako naona kabisa ni something iko next level...... Ushauri wangu mdogo Jaribu kuwa na Email lists audience kwa ajili ya e-commerce email marketing hii ni very important unaweza uka integrate mailchimp api kwenye store, unapofanya kazi na influencers especially wa instagram usisahau kucheck kama followers na likes zao ni za kweli huu mchezo tumefanya sana kwenye CPA marketing unakuta acc ina followers wengi na engagements za kutosha lakini zote BOKO, sijajua kama store yako ni Niche targeting (bidhaa moja) au ni General store (bidhaa tofauti) ila unapofanya SEO single product SEO ni bora kuliko whole Store SEO, jaribu kufanya sales funnels kwenye products zako, coupons, discounts na freebies kwa ajili ya kupata leads ni muhimu pia kwenye store, make sure content marketing iko fresh na copywriting ni muhimu pia unapofanya advertisements, usisahau kuweka pixels kwenye store kwaajili ya retargeting ads na ku build audience, lastly kwa experience yangu PPC ads ni bora sana kuliko FB or IG ads kwa e-commerce but do your own research all in all Goodluck with sales
 
Na develop Payment system kwa ajiri ya ku accept malipo mtandaoni kwa njia ya Mobile Money kama Mpesa, Halopesa, Tigopesa, Airtel money (Mtandao wowote ulio na huduma ya Mobile Money)

Haitotumia Third party APIs za mitandao husika,

Haito deal kabisa na pesa yako

Hii ni overview ya system kwa ufupi na the way itakavyo fanya kazi

1.Buyer ana visit store yako
2.Ana click product atakayokua interested nayo
3.At enda kwenye check out page
4.Ata chagua payment method, (naiita Lipal)
5.Atachagua mtandao wake(Mpesa,Halopesa etc)
6.Ata lipia kama anavyolipia normally kulingana na USSD codes za mtandao wake
(Namba ya malipo ni Namba yako ya simu, sharti uwe angalau ni mitandao ya simu mitatu tofauti, in this case utaweza accepts pesa kutoka kwa buyers wenye hio mitandao)
7.Lipal itamtaka aweke namba ya muamala ambayo huwa ina tumwa kawaida na mtandao husika baada ya kutuma pesa
8.System ita validate muamala, na kuendelea na flow nyingine ya store yako

Pesa yako utapokea kawaida tu kama unavyopokea pesa yoyote unayotumiwa via Mobile money bila makato Wala kuchelewa

Kwa hii Payment yoyote mwenye e-commerce store au website itakayotaka ku accept payments online itaweza

Advantages kubwa ni kuwa haitohitaji third-party APIs wala ku handle pesa ya mtu yoyote

Jinsi gani sasa itafanya kazi siwezi weka
 
One of the great content zilizosoma in a while big up sana mkuu, unachokifanya hakitofautiani sana na dropshipping Sema ile imebase sana watu wanachukua products aliexpress then wanauza kwenye store zao kupitia shopify. Umejiongeza sana kupata suppliers wako na nimependa wanatuma products on weekly basis bonge moja la advantage tofauti na kwingine. Pia kwa kujudge backend UI ya store yako naona kabisa ni something iko next level...... Ushauri wangu mdogo Jaribu kuwa na Email lists audience kwa ajili ya e-commerce email marketing hii ni very important unaweza uka integrate mailchimp api kwenye store, unapofanya kazi na influencers especially wa instagram usisahau kucheck kama followers na likes zao ni za kweli huu mchezo tumefanya sana kwenye CPA marketing unakuta acc ina followers wengi na engagements za kutosha lakini zote BOKO, sijajua kama store yako ni Niche targeting (bidhaa moja) au ni General store (bidhaa tofauti) ila unapofanya SEO single product SEO ni bora kuliko whole Store SEO, jaribu kufanya sales funnels kwenye products zako, coupons, discounts na freebies kwa ajili ya kupata leads ni muhimu pia kwenye store, make sure content marketing iko fresh na copywriting ni muhimu pia unapofanya advertisements, usisahau kuweka pixels kwenye store kwaajili ya retargeting ads na ku build audience, lastly kwa experience yangu PPC ads ni bora sana kuliko FB or IG ads kwa e-commerce but do your own research all in all Goodluck with sales
Hello mkuu, tho nimechelewa kujibu.
Thanks for the advice.
Hao influencers najuaje kama ni fake au real?

Kuhusu store angu ni ninche-based, sema ntajitahd kuw na hizo email lists. Sales funnels nimezitengeneza mkuu, tho haziko as productive as means nyingine.
 
i feel like something is missing kwenye huu uzi, tuutangaze twiter watu waje humu tuongee vizur wabongo
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom