GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,546
- 108,875
1. Nyumba unayokaa kama unafuga Njiwa na ukiwa Unauguza Mgonjwa ndani ukiona Njiwa Wote wanaondoka anza kuweka Oda ya Jeneza kwa Mgonjwa wako kwani utake usitake atakufa tu.
2. Nyumba unayoishi kama unafuga Mbwa kuanzia Saa 5 Usiku na Saa 11 Alfajiri ukisikia wanabweka sana jua Wachawi wanaingia Kazini na wanarejea kutoka Kututesa kwa Kutulimisha Majarubani Usiku kucha.
3. Ukiona Paka kuanzia Watatu kwenda mbele wanalia mno ama Dirishani Kwako au Getini Kwako Nyumbani jiandae kupokea Taarifa mbaya ya Msiba.
4. Kwa Mwanaume kama kuna Mwanamke au Mkeo umempa Mimba ( Ujauzito ) na ukiona tu mara kwa mara Mjusi Mdogo anakutambaa na Kukurikia na hatoki sehemu ulipo jua hiyo Mimba imeshaharibika.
5. Ukiwa umepanga Kusafiri (na hii ni hasa ukiwa Kijijini) kisha Usiku ukasikia au ukaona Bundi ametua Darini ya Nyumba uliyopo aihirisha upesi hiyo Safari yako kwani ukilazimisha lazima Ndugu zako waanze Kuulizia Maturubai ya Kukuwekea Msiba Kwenu yanapatikana (yanakodishwa) wapi.
6. Usiku kati ya Saa 7 mpaka Saa 9 kama Kwako unafuga Kuku ukiwasikia tu wanalia kwa Sauti isiyo ya Kawaida jua hapo Kwako kuna Watu wabaya ( hasa Majambazi ) wamekuja kusema nawe ili uwape vyao na ukikataa 'Wakucharange' vizuri.
7. Ukiona Mnyama Simba kaenda Mbuga ya Ugenini ( ya mbali kama ya Botswana ) kaua Adui mara Mbili jua baada ya Wiki Moja Simba huyo huyo ( akiwa Kwake Tanzania ) akibahatika tena kukutana na Adui wa Kufanana na Yule basi atamuua vibaya, Kikatili tena kati ya mara Tano au hata Saba kwani Simba huwa wakiwa Mbuga ya Lupaso Temeke Dar es Salaam huwa anakuwa Mkali na mwenye Hasira zaidi.
Na nyie ongezeni pia na zenu tafadhali.
2. Nyumba unayoishi kama unafuga Mbwa kuanzia Saa 5 Usiku na Saa 11 Alfajiri ukisikia wanabweka sana jua Wachawi wanaingia Kazini na wanarejea kutoka Kututesa kwa Kutulimisha Majarubani Usiku kucha.
3. Ukiona Paka kuanzia Watatu kwenda mbele wanalia mno ama Dirishani Kwako au Getini Kwako Nyumbani jiandae kupokea Taarifa mbaya ya Msiba.
4. Kwa Mwanaume kama kuna Mwanamke au Mkeo umempa Mimba ( Ujauzito ) na ukiona tu mara kwa mara Mjusi Mdogo anakutambaa na Kukurikia na hatoki sehemu ulipo jua hiyo Mimba imeshaharibika.
5. Ukiwa umepanga Kusafiri (na hii ni hasa ukiwa Kijijini) kisha Usiku ukasikia au ukaona Bundi ametua Darini ya Nyumba uliyopo aihirisha upesi hiyo Safari yako kwani ukilazimisha lazima Ndugu zako waanze Kuulizia Maturubai ya Kukuwekea Msiba Kwenu yanapatikana (yanakodishwa) wapi.
6. Usiku kati ya Saa 7 mpaka Saa 9 kama Kwako unafuga Kuku ukiwasikia tu wanalia kwa Sauti isiyo ya Kawaida jua hapo Kwako kuna Watu wabaya ( hasa Majambazi ) wamekuja kusema nawe ili uwape vyao na ukikataa 'Wakucharange' vizuri.
7. Ukiona Mnyama Simba kaenda Mbuga ya Ugenini ( ya mbali kama ya Botswana ) kaua Adui mara Mbili jua baada ya Wiki Moja Simba huyo huyo ( akiwa Kwake Tanzania ) akibahatika tena kukutana na Adui wa Kufanana na Yule basi atamuua vibaya, Kikatili tena kati ya mara Tano au hata Saba kwani Simba huwa wakiwa Mbuga ya Lupaso Temeke Dar es Salaam huwa anakuwa Mkali na mwenye Hasira zaidi.
Na nyie ongezeni pia na zenu tafadhali.