Tujuzane aina ya manukato (perfume) unayotumia

Yes, Mara nyingi watu huniambia, na pia huwa inakaa sana kwenye nguo, weekend huwa natoa nguo chafu kwenye tenga zikafuliwe nasikia harufu zake bado.

Lakini pia mimi situmii perfume throught the year, kuna muda nazichoka natumia deodorant tu.

Ila mie naipenda sana hiyo Givenchy kuliko hiyo nyingine.
Maelezo murua kabisa, Asante
 
Adjustments.jpg

Natumia hii Inaitwa Amber flixir mystery EDP brand Oriflame kitu amazing sana
 
Hii harufu yake sio kali ya kuwakera wengine.
Mana natumia bitter peach,ni nzuri sana ila mwanzo nilikua napiga chafya sana,naona hata nikiwa kwenye usafiri wa uma naona abiria wenzangu wanapiga chafya hata ofisin ilikua ni hivyo ila sasa wameizoea.
Bitter peach bei ngapi
 
Wewe unatumia nini?
Namuunga mkono mdau mmoja pale juu amesema sabuni ya jamaa na maji ya chumvi

Mimi sijafika maisha yako ya kutumia perfume za bei kalii..
Huwa natumia body sprays+splash.
Na huwa nachanganya, sometimes inatokea harufu nzuri mno.

Sprays zangu pendwa mara nyingi ni knowledge, chastity(zote mbili),Dolby,na NYINGINE nyingi nimezisahau majina.
Splashs ndio nyingi zaidi i.e secret of Lady, Sweet,za vanilla.

Nikikosa hizo sprays basi natumia yoyote tu kama Galaxy na adorable.

Kutokana na tatizo langu la kiafya(nina nasal polyps),, specialist wangu alishauri niache kabisa!ama nijikite kwenye nivea dry impact,na ndiyo ninayotumia Sasa.
Kuacha kabisa ni ngumu.

Huwa natumia pia udi na manukato fulani ya kiislamu,huuzwa msikitini..majina yake sijayakariri...


Kwa ushauri wa mambo ya perfumes muone Kiranga .
Huyu mtu ,kwa perfumes alizonazo,nadhani anajua aina tofauti tofauti ya harufu za perfumes.
 
Back
Top Bottom