Tujiulize uwezo wa kisiasa kati ya timu Comred Abdulrahman Kinana, Nape Vs Dr. Bashiru Ally, Humphrey Polepole

mcoloo

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
918
1,401
Nimetafakari sana nakuona mtindo wa Siasa zetu unavyo pata mabadiliko hasa ndani ya chama chetu pendwa cha CCM .

Tangu mfumo wa siasa za vyama vingi ulipo anzishwa hapa Tanzania tumeona viongozi wa kisiasa katika chama wakitenda kwa mitindo mbalimbali , kabla ya uchaguzi wa 2015 tulishuhudia CCM ilipo ona ari na mapenzi ya watanzania kukichoka chama ,kutokana namfumo mbovu wa watendaji ndani ya serikali uliopelekea uchaguzi wa mwaka 2000 kuibuka na ushindi mwembamba ambao haujawahi kutokea,

Katibu Mkuu wa CCM wa wakati huo ndugu Abdrahaman Kinana akiwa na Katibu Mwenezi wa chama wakati huo Nape Nnawie, waliinuka wakaacha ofisi na kuelekea kwa wananchi moja kwa moja ili kujaribu kurejesha imani ya wananchi kwa chama. Kwakweli kwa jitihada walizo zifanya kwa kukosoa wazi wazi baadhi ya watendaji wa serikali,kwa kiasi Fulani wananchi ilirudisha imani kwa chama . Na ikumbukwe kuwa wakati hawa viongozi wakitenda haya upinzani ulikuwa nao unachukuwa kasi ya kujiimarisha sana.

Lakini baada ya mabadiliko yaliyo fanyika kwa kuwabadilisha katika nafasi zao na kuchukuliwa na Dr Bashiru na Polepole, tumeona mabadiliko yakijitokeza japo ni kweli kwamba kila uongozi huwa na mbinu zake za kiuongozi, hawa wamekuja na mbinu ambayo siyo ya kwenda kwa wananchi ila wao wamekuja na chamambinu ya kwenda kwa viongozi viongozi wa vyama vya upinzani na kuwashawishi wahame vyama vyao na kujiunga na chama chao,

Jambo la kujiuliza hapa ni kuwa unapo kwenda kwa viongozi na kuwashawishi wahame huku ukiwaacha maelfu ya wananchi wakiwa na mashaka makubwa hasa kwenye mfumo wa siasa zinazo endelea ndani ya nchi ambayo kwa kiasi kikubwa ni kwamba hata wana CCM wenyewe wanaziona kama zimekuwa kandamizi kwa vyama vya upinzani , kwani kama Taifa liliamua kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi basi ni wazi kuwa ilikuwa imekubaliana kupambana kwa hoja majukwaani na wala sio kuziba midomo ya vyama vya upinzani ili isiweze kunena.

Hivi kati ya hizi timu mbili kati ya ile ya Comrade na ya Dr ni ipi imeonyesha mafanikio ya kweli ya kidemokrasia halisi ?.
 
Bahati mbaya hujafatilia tu..katika timu ambayo inaenda kwa wananchi na kusaidia kutatua kero ni hii ya kina bashiru na Polepole..hawa jamaa hawasubiri uchaguzi ukaribie..wanafanya kazi kiuhalisia kabisa..
 
ccm hii ya jiwe huitofautishi na magenge ya kiharamia dhidi ya raia, hivyo kufananisha ccm ya Vasco da gama na hii ni tusi kubwa sana kwa wanaccm
 
Bahati mbaya hujafatilia tu..katika timu ambayo inaenda kwa wananchi na kusaidia kutatua kero ni hii ya kina bashiru na Polepole..hawa jamaa hawasubiri uchaguzi ukaribie..wanafanya kazi kiuhalisia kabisa..

Ukienda kutatua kero ndio uzuie demokrasia kutamalaki? Kama unafanya vyema unatumia vyombo vya dola vya nini ili ukubalike? Kuleta maendeleo kwa hela za mkopo ambao walipaji ni watanzania wote kunatoaje uhalali wa kuua demokrasia? Mpaka sasa deni la taifa ni 50t+, ni nadra kulipa 4t kwa mwaka. Hivyo uongozi huu wa kina Polepole hata ufanyeje hauwezi kulipa haya madeni zaidi ya kuongeza deni, sasa wanapata wapi uhalali wa kuzuia demokrasia?
 
Hawa wa sasa hawana tone la uadilifu.. Wizi, utekaji, ulaghai, ufisadi wa kutumia fedha za walipakodi kununua wanasiasa, matumizi ya nguvu ya dola na udanganyifu wa kila aina kwny chaguzi ndo vimetamalaki..

Hawana uwezo tena wa kushinda kwny uchaguzi wa huru na haki
 
Kila zama na kitabu chake,Enzi za Kinana na Nape Upinzani ulikuwa unashinda chaguzi enzi za Bashiru na Pole Pole upinzani unashindwa chaguzi
Kwa wizi, gilba, unyanganyi na udanganyifu? kwa msaada wa nec-ccm na mapolisi-ccm? Huna hata aibu? ccm kweli mna 'uso wa mbuzi'
 
Kila zama na kitabu chake,Enzi za Kinana na Nape Upinzani ulikuwa unashinda chaguzi enzi za Bashiru na Pole Pole upinzani unashindwa chaguzi
Binafsi sikuona mantiki ya kumtoa Dr.Bashiru UDSM kama hatuoni hata kwa chembe usomi wake ukitumika katika siasa za ushindani.Ni afadhali CCM wangewekeza katika kumteua Sirro kuwa katibu mkuu wao.Kwa haya yanayoendelea kipindi hiki ambapo wengine wanafanya siasa na wengine wanazuiliwa,kusakamwa na kuandamwa ni vigumu sana kuwapima Polepole na timu yake.Katika kipindi ambapo ni sura zile zile kwenye kila runinga,mizengwe,fitna na vitisho vimetamalaki,Dr.Bashiru na Polepole ni sawa na Blanketi bichi Makete
 
Binafsi sikuona mantiki ya kumtoa Dr.Bashiru UDSM kama hatuoni hata kwa chembe usomi wake ukitumika katika siasa za ushindani.Ni afadhali CCM wangewekeza katika kumteua Sirro kuwa katibu mkuu wao.Kwa haya yanayoendelea kipindi hiki ambapo wengine wanafanya siasa na wengine wanazuiliwa,kusakamwa na kuandamwa ni vigumu sana kuwapima Polepole na timu yake.Katika kipindi ambapo ni sura zile zile kwenye kila runinga,mizengwe,fitna na vitisho vimetamalaki,Dr.Bashiru na Polepole ni sawa na Blanketi bichi Makete
Usomi wa Bashiru wote umeingia doa kwa kujiingiza kwenye siasa.
 
Back
Top Bottom