Tujiulize uchawi, ramli na mazindiko vina nafasi gani kwenye siass za Tanzania? Je wasomi hawaamini taaluma zao?

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,603
29,743
Amani iwe kwenu wachambuzi jadidifu.

Ninaleta hoja kwenu ili tuelimishane ikibidi tukosoane ama kuwajibishana

Wanasiasa wengi kama siyo wote, wamekuwa wakionesha matendo yao fulani fulani kwa kificho au kwa uwazi kabisa.

Wamejenga mazoea ya kutumia watu wanaoitwa waganga wa kienyejj ili kupata vyeo vya kuchaguliwa au uteuzi. Wanasiasa hawa wengi wamehusika kutoa kafara mbalimbali hususani wanyama na hata wengine wametuhumiwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu ili wapate wanachokikusudia.

Tumeona hata chaguzi nyingi za ndani ya chama kikubwa, watu wakitumia usaidizi wa ulozi kufanikisha malengo yao wachaguliwe. Wengi wa wanasiasa hao ni wasomi na wengine viwango vya juu. Lakini inapofika wakati wa kusaka vyeo wanaweka taaluma pembeni na kuwatumia waganga ambao wengi hawana hata elimu ya sekondari

Kitu cha ajabu ni kwamba wanasiasa hao hao wakishinda chaguzi au wakiteuliwa huwa wanatumia misahafu wakati wa kuapishwa. Misahafu hiyo inakemea uchawi na namna yoyote inayofanania uchawi.

Screenshot_20230226_083826_Google.jpg


tujjulize maswali.

  1. Je uchawi na ramli vina nafasi gani kwenye maendeleo ya Taifa letu?
  2. Je utendaji usioridhisha wa viongozi wetu ambapo hata walioteuliwa hawagusiki, hayo yanatokana na nguvu za uchawi huo?
  3. Wananchi kugojishughulisha kuhoji ama kutaka utatuzi wa athari za utendaji mbovu, nao wefubazwa na nguvu za uchawi ambazo ziliwslazimisha kuwapa kura viongozi wababaifu kwenye utendaji?
  4. Kwa nini wasomi ndiyo wanaongoza kwa idadi kubwa kwenda kwa wachawi kuroga ili wachaguliwe, wateuliwe ai waajirike?
Katika huu mwenendo wa wanasiasa kutunga sheria inayokataza uchawi, lakini wao ndiyo wsnaoongoza kupanga foleni kwa wachawi. Nikukaribishe tujadili
  • Una mtazamo gani kwenye eneo hili?
  • Nini kifanyike?
Screenshot_20230226_083456_Chrome.jpg
 
Amani iwe kwenu wachambuzi jadidifu.

Ninaleta hoja kwenu ili tuelimishane ikibidi tukosoane ama kuwajibishana

Wanasiasa wengi kama siyo wote, wamekuwa wakionesha matendo yao fulani fulani kwa kificho au kwa uwazi kabisa.

Wamejenga mazoea ya kutumia watu wanaoitwa waganga wa kienyejj ili kupata vyeo vya kuchaguliwa au uteuzi. Wanasiasa hawa wengi wamehusika kutoa kafara mbalimbali hususani wanyama na hata wengine wametuhumiwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu ili wapate wanachokikusudia.

Tumeona hata chaguzi nyingi za ndani ya chama kikubwa, watu wakitumia usaidizi wa ulozi kufanikisha malengo yao wachaguliwe. Wengi wa wanasiasa hao ni wasomi na wengine viwango vya juu. Lakini inapofika wakati wa kusaka vyeo wanaweka taaluma pembeni na kuwatumia waganga ambao wengi hawana hata elimu ya sekondari

Kitu cha ajabu ni kwamba wanasiasa hao hao wakishinda chaguzi au wakiteuliwa huwa wanatumia misahafu wakati wa kuapishwa. Misahafu hiyo inakemea uchawi na namna yoyote inayofanania uchawi.

View attachment 2530255

tujjulize maswali.

  1. Je uchawi na ramli vina nafasi gani kwenye maendeleo ya Taifa letu?
  2. Je utendaji usioridhisha wa viongozi wetu ambapo hata walioteuliwa hawagusiki, hayo yanatokana na nguvu za uchawi huo?
  3. Wananchi kugojishughulisha kuhoji ama kutaka utatuzi wa athari za utendaji mbovu, nao wefubazwa na nguvu za uchawi ambazo ziliwslazimisha kuwapa kura viongozi wababaifu kwenye utendaji?
  4. Kwa nini wasomi ndiyo wanaongoza kwa idadi kubwa kwenda kwa wachawi kuroga ili wachaguliwe, wateuliwe ai waajirike?
Katika huu mwenendo wa wanasiasa kutunga sheria inayokataza uchawi, lakini wao ndiyo wsnaoongoza kupanga foleni kwa wachawi. Nikukaribishe tujadili
  • Una mtazamo gani kwenye eneo hili?
  • Nini kifanyike?
View attachment 2530254
Mbele ya madaraka, PhD tupa kule, sangoma njoo
 
Nyuma ya kila jambo lazima kuwe na nguvu. Hapo inategemea hiyo nguvu chanzo chake kipi.. Nguvu zote zina gharama, ila shortcut ushirikina na uchawi ndio maana wanakimbilia huko.. hata ukiwa na elimu vipi.. ukikosa nguvu nyuma yako umefail
 
Nyuma ya kila jambo lazima kuwe na nguvu. Hapo inategemea hiyo nguvu chanzo chake kipi.. Nguvu zote zina gharama, ila shortcut ushirikina na uchawi ndio maana wanakimbilia huko.. hata ukiwa na elimu vipi.. ukikosa nguvu nyuma yako umefail
Je wanavyoapa kwa kutumia vitabu vitakatifu wanatuonesha namna walivyo wanafiki au nayo ni nguvu nyuma yao?
 
Uchawi Kwa akili za watu wa Afrika usifundishwe.. Watu wenye vichwa wachache, Nazi nyingi.... Tutauana walahi
Kwa hivyo ni mila na desturi ya mwafrika?

Dunia sasa ipo kwenye advanced science era. Sisi tupo na tunguli zetu tangu tunazaliwa hadi kaburini. Na usipoangalia unageuzwa zindiko la walio hai
 
Kwa hivyo ni mila na desturi ya mwafrika?

Dunia sasa ipo kwenye advanced science era. Sisi tupo na tunguli zetu tangu tunazaliwa hadi kaburini. Na usipoangalia unageuzwa zindiko la walio hai
Uchawi dunia nzima upoo. Wazungu wanajua na kuelewa vizuri. Kisayansi jamii, kuna mtaalamu mmoja wa jamii aliwahi kuzungumzia kitu kinaitwa "Survival" yani hata mwana damu awe na Maendeleo kias gani wanaovaa magome ya miti watakuwepo. Hata kuwe na sayansi na teknolojia ya Aina gani wanga, walozi na wehuwehu watakuwepo tu
 
Back
Top Bottom