digba sowey
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 7,894
- 14,353
Wakuu natumaini kuwa hamjambo na mnaendelea na shughuli zenu kama kawaida.
Naomba niende kwenye hoja yangu. Wahenga walisema Muda ni mwalimu mzuri, Bwana huyu anayeitwa Tundu Lissu baada ya kujeruhiwa na kunusurika kifo alikimbilia ughaibuni akidai kuwa anaenda pata matibabu, akiwa huko ughaibuni alitumia njia za kila aina kuichafua nchi yetu na kumchafua rais wetu, na alijiapiza kuwa lazima nchi wahisani zikome kutoa misaada kwa Tanzania na Watanzania.
Baada ya kuona hoja na chuki zake hazijazaa matunda amebadili uelekeo na kuutaka urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania akijidai eti ni mtetezi wa wanyonge, wanyonge wepi hao anaowatetea wakati akiwa ng'ambo aliwatakia maisha mabaya?
Huyu Lissu kwa kauli zake ambazo amekuwa akizitoa zinathibitisha kuwa ana nia ovu imefichika juu ya kuutaka urais, na kwa akili zake anaamini kabisa Watanzania watampa kura. Chonde chonde Watanzania tumuepuke huyu mtu, nikimwangalia naona kama kuna nguvu nyuma yake, nguvu hiyo siyo zuri maana imelenga kuharibu mstakabari na umoja wa taifa letu.
Shime Watanzania, Lissu ni garasa tusijaribu kuharibu umoja na mshikamano wetu uliodumu kwa miaka zaidi ya 50 kumpa kura eti awe Rais maana huyu mtu ni mbinafsi, ni mwenye chuki na hana staha mdomoni kwake, lakini pia anatumika kuharibu amani ya taifa letu.
Naomba niende kwenye hoja yangu. Wahenga walisema Muda ni mwalimu mzuri, Bwana huyu anayeitwa Tundu Lissu baada ya kujeruhiwa na kunusurika kifo alikimbilia ughaibuni akidai kuwa anaenda pata matibabu, akiwa huko ughaibuni alitumia njia za kila aina kuichafua nchi yetu na kumchafua rais wetu, na alijiapiza kuwa lazima nchi wahisani zikome kutoa misaada kwa Tanzania na Watanzania.
Baada ya kuona hoja na chuki zake hazijazaa matunda amebadili uelekeo na kuutaka urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania akijidai eti ni mtetezi wa wanyonge, wanyonge wepi hao anaowatetea wakati akiwa ng'ambo aliwatakia maisha mabaya?
Huyu Lissu kwa kauli zake ambazo amekuwa akizitoa zinathibitisha kuwa ana nia ovu imefichika juu ya kuutaka urais, na kwa akili zake anaamini kabisa Watanzania watampa kura. Chonde chonde Watanzania tumuepuke huyu mtu, nikimwangalia naona kama kuna nguvu nyuma yake, nguvu hiyo siyo zuri maana imelenga kuharibu mstakabari na umoja wa taifa letu.
Shime Watanzania, Lissu ni garasa tusijaribu kuharibu umoja na mshikamano wetu uliodumu kwa miaka zaidi ya 50 kumpa kura eti awe Rais maana huyu mtu ni mbinafsi, ni mwenye chuki na hana staha mdomoni kwake, lakini pia anatumika kuharibu amani ya taifa letu.