Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Kwa rais ambaye mambo yake hayaeleweki eleweki kama siri ya kinachotokea kaburini. Lazima tuwe na majibu ya swali hili kabla, kwani chochote kinaweza kutokea. Inawezekana akaunda baraza jipya lakini likiwa na sura zilezile huku huyu akimuhamisha wizara hii na kumpeleka ile. Bado atakuwa hajakidhi matakwa ya malalamiko ya watanzania. Itakuwa sawa na sifuri. Pia huyu ni rais ambaye anaweza kubadilika kama kinyonga, ikitokea pia akaghairi kutangaza baraza hilo jipya. Sisi watanzania tumejiandaa kuchukua hatua gani? Au tutapiga kimya kama kawaida yetu?