Tujiulize hivi hizi juhudi kubwa za kuwatoa kwa hila wabunge wa Chadema nia yake ni nini?

Shetani anataka awamalize wabunge wa upinzani ili apitishe muswaada wa Nkamia akiwa na wabunge wa ccm peke yake .
 
Nimekuuliza tena, kwanini anatengeneza sheria za kupora nguvu za maamuzi ya kitaasisi na kuwapa watu, naona unaishia kuzunguka tu. Nimerudia zaidi ya mara moja kuhusu nguvu zinazohamishwa kutoka mahakamani na kupewa watu kuwa final say. Sioni popote inapotoweka kwenye hilo. Nimekuambia hivyo ni viashiria vya wazi vya mtu huyu kujikita madarakani zaidi muda.

Nataka nikupe mfano mmoja mrahisi ili kukuonyesha hao ccm ikiwepo ww hawana nguvu dhidi yake, kuhusu maamuzi ya mtu, na wengi wao hawajausoma mchezo na wakiamka watakuwa wamechelewa. Mgombea wa ubunge wa ccm huwa anashindanishwa na wengine kupata mmoja, lakini nyakati za uchaguzi wa marudio maamuzi yalifanyika na genge dogo kupitisha wagombea waliotoka huko upinzani, wakapewa nafasi bila hata kukijua chama na wakapitishwa kibabe. Na kwenye hizo chaguzi zikafanyika rafu za wazi za kuvunja sheria ambazo leo mnasema maamuzi ya Lissu yamezitii hizo hizo, ili mgombea wa ccm atangazwe mshindi. Kama aliweza kufanya vile huku wanachama wakilalamika kichini chini, watamfanya nini hiyo 2025 akitanua goli? Kungekuwa na wanaccm wasafi ningekuelewa, lakini hawa wagombea ambao wakichomoza pua tu, Takukuru wanaambiwa wafuatilie skendo zao?
tindo nadhani umeamua kutonielewa au hujanielewa. CCM hawawezi kuruhusu mtu akae zaidi ya miaka 10 sababu kutatokea maasi na hayo maasi yataongozwa na inner circle ya CCM. Mtu kama January Makamba, Mwigulu nk wametulia sababu wanajua wana nafasi 2025. Watu wa aina hii wakijua hawana nafasi tena ujue hapo kuna maasi yanakuja.

Kwa lugha nyepesi, kuwepo ukomo wa madaraka kunaleta hali ya uvumilivu ndani ya CCM na nchi, CCM wanalitambua hili vyema na hivyo mawazo yako ya kufikirika kuwa Magu atajiongezea muda hayapo na hayawezekaniki.
 
Tunao madokita na maprofesa wengi bungeni na serikalini wangetetea demokrasia iimarishwe lakini imekuwa kinyume cha matarajiyo ya watanzania walio wengi .Wengi wamejikita kwenye ajira zao,ubinafsi wakujifanya ni wanyonge huku waki focus kujipatia mali na madaraka zaidi .Mwalimu Ndie pekee alikuwa anawafahamu watu wa aina hii sasa tuseme demokrasia ilikwenda na Mwalimu kwa nini turudi katika mfumo wa chama kimoja?
 
tindo nadhani umeamua kutonielewa au hujanielewa. CCM hawawezi kuruhusu mtu akae zaidi ya miaka 10 sababu kutatokea maasi na hayo maasi yataongozwa na inner circle ya CCM. Mtu kama January Makamba, Mwigulu nk wametulia sababu wanajua wana nafasi 2025. Watu wa aina hii wakijua hawana nafasi tena ujue hapo kuna maasi yanakuja.

Kwa lugha nyepesi, kuwepo ukomo wa madaraka kunaleta hali ya uvumilivu ndani ya CCM na nchi, CCM wanalitambua hili vyema na hivyo mawazo yako ya kufikirika kuwa Magu atajiongezea muda hayapo na hayawezekaniki.

Unachekesha ile mbaya, utaleta uasi kama una support ya nguvu ya umma. Ni mwanachama gani anaweza kusimama na kusema kweli ana nguvu ya umma, huku ushindi wao kwenye box la kura unategemea vyombo vya dola na tume ya uchaguzi? Na kwa bahati nzuri hata Magu anajua yeye na wanaccm wenzake hawana nguvu ya ushawishi kwa umma. Hiyo ndio sababu ya yeye kupiga marufuku siasa na kuihujumu wazi wazi cdm.

Mfano mrahisi wa wanaccm mtazame Lowasa, alitoka ccm kwa kujidanganya ana nguvu ya umma, lakini aliwarubuni viongozi wa cdm kwa fedha zake na kupewa nafasi kwenye chama ambacho tayari kina support ya umma. Kama anaamini alikuwa na nguvu mbona hakwenda TLP, au Chauma? Lakini baada ya kukosa madaraka ili awe na nguvu ya dola ameshindwa siasa, ndio maana karudi ccm kwenye siasa za mbeleko ya dola. Hao kina Mwigulu na Januari sio kwamba wametulia, bali aliyeko madarakani hatumii madaraka yake kuwapa mbeleko na wao nguvu yao iko kwenye mbeleko.

Wanasiasa wanaoweza kusimama na kufanya siasa za kweli za ushawishi wa hoja ndani ya ccm, ni wachache sana, wengi wao wanategemea vyombo vya dola ikiwemo Magu. Kwenye maisha yako umewahi kumuona akijenga hoja kwenye mdahalo wowote? Jaribu kufuatilia sehemu zenye uhuru wa maoni au ambapo hamna nguvu ya dola uone ujengaji hoja wa wanaccm. Mfano kwenye mitandao ya kijamii, kwenye luninga na midahalo mbalimbali. Hata huko bungeni huwa tunaona hoja za wabunge wa ccm, mpaka unashangaa alishindaje ubunge.

NB: hata hapa umekwepa kujibu kuhusu hizo sheria za kupora nguvu za taasisi na hasa mahakama, na kumpa msajili ambayo yeye ndio anamchagua. Na ili msajili awepo hapo inategemea fadhili zake. Ogopa kiongozi anayeua nguvu za taasisi na kuhamishia kwa watu. Huyo lengo lake ni ovu tu.
 
Kuna tofauti kati ya binadamu na mtu. Sio kila binadamu ni mtu. Kila mtu ni binadamu. Wewe ni binadamu tu. Binadamu ni mnyama tu kama wanyama wengine. Sheria zipo binadamu wawe watu. Sheria inayomfanya mtu kuwa binadamu tu ni batili. Mashauri kwa Mbowe na Matiko alitumia vifungu vya sheria! Rumanyika alitumia nini? Tofauti kuu ni kwamba mmoja ni binadamu na mwingine ni mtu! Sheria zipo kuhudumia mtu.
"Sheria zimewekwa ili binadamu tuwe watu" basi tuzifuate na kuziheshimu ili tukamilishe utu wetu.
 
Back
Top Bottom