Tujiulize hivi hizi juhudi kubwa za kuwatoa kwa hila wabunge wa Chadema nia yake ni nini?

Lissu alishinda kwa 56% wakati huo huo Nasari alikuwa na karibu na banda, je yeye Nasari hakuibiwa? Ni wazi Lissu alishinda kwa kura chache na umaarufu wake kwenye jimbo lake si mkubwa hivyo marudio yoyote ya uchaguzi si habari njema kwake.

CCM tayari wana wabunge wa kutosha wa kuweza kubadilisha sheria yoyote. Unahitaji 2/3 tu ya bunge kuweza kubadilisha Katiba ambayo CCM tayari wanayo hivyo hii hoja ni mfu kama sio cheap propaganda.

Unaweza ukaniambia ni wabunge wangapi wa ccm walishinda kihalali zaidi ya 70%?. Mbunge aliyepata kura nyingi kuliko wabunge wote ni sugu. Je hiyo ni tiketi ya kwamba uchaguzi ujao anashinda? Tuje kwa Magufuli, yeye alishinda kaa 58%, je hiyo ni ishara kwamba uchaguzi ujao anashindwa?

Ni kweli ccm wanazaidi ya 2/3 wanaweza kubadili chochote hilo sipingi, ila inatakiwa kusiwe na wabunge wengi wa upinzani wanaoweza kupinga hili kwa hoja kwani kuna umma ambao jambo hilo ni zito.

Ukitaka kujua kwamba lengo ni kubadilisha katiba ili akae madarakani zaidi angalia sheria ya vyama vya siasa. Anatunga sheria kwamba maamuzi yatoke kwenye taasisi/mahakama apewa mtu (msajili). Azaki za kiraia pia anageuzwa msajili kuwa yeye ndio msemaji wa mwisho badala ya taasisi na mahakama. Sababu hasa, vyama vya siasa na azaki ndio haswa huonyesha kupinga mambo kama hayo ya kuongeza muda wa kukaa madarakani. Hivyo ni rahisi yeye kuwaagiza wasajili kufuta chama au azaki bila kuwajibika pindi zitakapohoji hali hiyo.

Ogopa kiongozi mzalendo asiyetaka katiba ya wananchi, bali kutunga sheria za kulinda madaraka yake. Narudia tena, hakuna sheria wala nini kuhusu hatua hiyo ya Lissu, bali ni wale wale waliotaka kumtoa uhai wamerudi kwa sura ya sheria na taratibu fullstop.
 
Mnachoshindwa kuelewa ni kwamba Bunge ni taasisi na siyo mtu binafsi. Kama ni taasisi basi ina taratibu na sheria zake. Spika kujua Tundu Lissu alipo hakufanyi sheria na taratibu za Bunge kuvunjwa au kutofuatwa. Tundu Lissu alipomiminiwa risasi hakuna aliemfukuza ubunge, kila mtu aliona hali tete aliyonayo na Bunge lilishiriki kwa namna moja au nyingine kuokoa uhai wake akiwa Dodoma. Japo chama chake baadae kiliamua kufuata utaratibu mwingine wa matibabu yake.

Kilichopelekea Bunge kuchukua hatua sasa, siyo tu kutojua Lissu alipo bali hata taarifa rasmi ya maendeleo ya matibabu yake haijulikani. Mara kadhaa Lissu ameombwa kufuata taratibu za kisheria kuhusu kutoa taarifa ya hali ya matibabu yake kwa muajiri wake lakini kutokana na kiburi amegoma kufanya hivyo. Badala yake amekua akilitaka Bunge kama linahitaji taarifa hiyo, likaombe kwa madaktari wanaomtibu. Sasa, hii ni dharau kubwa sana kwa taasisi kubwa kama ya Bunge.

Kiutaratibu mtumishi yoyote awe wa umma au sekta binafsi, anapoumwa au kuwa na dharura ya matibabu hasa ya muda mrefu, anapaswa yeye ndo atoe taarifa kwa muajiri wake na siyo muajiri kuanza kutafuta taarifa zake. Isitoshe matibabu ya Lissu hayagharamiwi na bunge hivyo ni ngumu kujua kama huyu mtu amepona au bado anaumwa. Hasa ukizingatia pia mwenendo wake, siyo kwamba yupo hospitali amelazwa mahututi kama ilivyokua mwanzo bali anaonekana akisafiri nchi mbalimbali na kufanya mahojiano na vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii. Hii inaleta tafsiri kwamba Afya yake imeimarika kwa kiasi kikubwa kuweza kutekeleza majukumu yake ya kibunge. Lakini hajawahi kuonekana bungeni wala kutoa taarifa yoyote.

Jambo lingine la kushangaza, watu wengi wamekua wakilaumu Lissu kufukuzwa ubunge kwa kuangalia sababu moja tu ya kutotoa taarifa za maendeleo matibabu yake. Lakini wanaiacha kwa makusudi sababu nyingine ya msingi ambayo imetajwa kikatiba nayo ni kutotoa taarifa ya Mali na Madeni kwa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Ukisoma ibara ya 71 (1)(c)(d) ya Katiba inasema wazi kabisa kwamba mbunge atakoma ubunge au ataacha kiti chake endapo (c) atakosa kuhudhuria vikao vya mikutano mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika na (d) itathibitishwa amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Yote haya Lissu ameenda kinyume nayo, Sasa kwanini asipoteze ubunge wake? Yeye ni nani mpaka awe juu ya Sheria na Katiba.
wewe nae ni mpuuzi tu!! Gazeti zima umeshindwa kutambua kuwa Lissu Dunia nzima ajua lissu ni mgonjwa?? Bunge lilichanga PESA za harusi kwa Lissu??, roho mbaya, chuki, fitina na udikteta ndio mnachokijua wapuuzi nyie.
 
Kuna tofauti kati ya binadamu na mtu. Sio kila binadamu ni mtu. Kila mtu ni binadamu. Wewe ni binadamu tu. Binadamu ni mnyama tu kama wanyama wengine. Sheria zipo binadamu wawe watu. Sheria inayomfanya mtu kuwa binadamu tu ni batili. Mashauri kwa Mbowe na Matiko alitumia vifungu vya sheria! Rumanyika alitumia nini? Tofauti kuu ni kwamba mmoja ni binadamu na mwingine ni mtu! Sheria zipo kuhudumia mtu.

Haya ya binadamu na mtu yapo kweye sheria??....
 
Unaweza ukaniambia ni wabunge wangapi wa ccm walishinda kihalali zaidi ya 70%?. Mbunge aliyepata kura nyingi kuliko wabunge wote ni sugu. Je hiyo ni tiketi ya kwamba uchaguzi ujao anashinda? Tuje kwa Magufuli, yeye alishinda kaa 58%, je hiyo ni ishara kwamba uchaguzi ujao anashindwa?

Ni kweli ccm wanazaidi ya 2/3 wanaweza kubadili chochote hilo sipingi, ila inatakiwa kusiwe na wabunge wengi wa upinzani wanaoweza kupinga hili kwa hoja kwani kuna umma ambao jambo hilo ni zito.

Ukitaka kujua kwamba lengo ni kubadilisha katiba ili akae madarakani zaidi angalia sheria ya vyama vya siasa. Anatunga sheria kwamba maamuzi yatoke kwenye taasisi/mahakama apewa mtu (msajili). Azaki za kiraia pia anageuzwa msajili kuwa yeye ndio msemaji wa mwisho badala ya taasisi na mahakama. Sababu hasa, vyama vya siasa na azaki ndio haswa huonyesha kupinga mambo kama hayo ya kuongeza muda wa kukaa madarakani. Hivyo ni rahisi yeye kuwaagiza wasajili kufuta chama au azaki bila kuwajibika pindi zitakapohoji hali hiyo.

Ogopa kiongozi mzalendo asiyetaka katiba ya wananchi, bali kutunga sheria za kulinda madaraka yake. Narudia tena, hakuna sheria wala nini kuhusu hatua hiyo ya Lissu, bali ni wale wale waliotaka kumtoa uhai wamerudi kwa sura ya sheria na taratibu fullstop.
Naona umeamua kuweka siasa za kufikirika hapa, CCM tayari ina 2/3 bungeni, inaweza pitisha chochote inachohitaji. Lissu amevuliwa ubunge kwa sababu ya kibri chake cha kijinga, kama ana uwezo wa kuwa anaandika makala kwa kila tukio linaloendelea Tz Kwa nn ashindwe kuandika barua ya kikazi ?

Upinzani bila kuambiwa ukweli watazidi kudondoka, sababu badala ya kuwaambia mapungufu yao mnasujudu ujinga wao. Haiwezekani unajua kabisa unatakiwa utoe taarifa usipokuwepo bungeni ila hautoi kwa maksudi ukitegemea utaogopwa, sasa ndio Ubunge ameshavuliwa na 2020 hashindi Ubunge wala urais, Strategists wa CHADEMA ni wapumbavu, no offense na mnavyotetea ujinga wao ndio wanavyo endelea kuvurunda.
 
wewe nae ni mpuuzi tu!! Gazeti zima umeshindwa kutambua kuwa Lissu Dunia nzima ajua lissu ni mgonjwa?? Bunge lilichanga PESA za harusi kwa Lissu??, roho mbaya, chuki, fitina na udikteta ndio mnachokijua wapuuzi nyie.
Sasa kati yangu Mimi nawwe nani Mpuuzi. Kuandika tu kunakupa shida, utaweza kuelewa kweli nilichoandika? Unaonekana tu shule yako ni ndogo hata taratibu za kazi huzielewi.
 
Naona umeamua kuweka siasa za kufikirika hapa, CCM tayari ina 2/3 bungeni, inaweza pitisha chochote inachohitaji. Lissu amevuliwa ubunge kwa sababu ya kibri chake cha kijinga, kama ana uwezo wa kuwa anaandika makala kwa kila tukio linaloendelea Tz Kwa nn ashindwe kuandika barua ya kikazi ?

Upinzani bila kuambiwa ukweli watazidi kudondoka, sababu badala ya kuwaambia mapungufu yao mnasujudu ujinga wao. Haiwezekani unajua kabisa unatakiwa utoe taarifa usipokuwepo bungeni ila hautoi kwa maksudi ukitegemea utaogopwa, sasa ndio Ubunge ameshavuliwa na 2020 hashindi Ubunge wala urais, Strategists wa CHADEMA ni wapumbavu, no offense na mnavyotetea ujinga wao ndio wanavyo endelea kuvurunda.
Ukweli mchungu. Lissu ni mwanasheria anajua vizuri sana utaratibu ulivyo ila alifanya makusudi kabisa, kwa sababu wanawajua wafuasi wao wengi ni mambumbumbu.
 
Naona umeamua kuweka siasa za kufikirika hapa, CCM tayari ina 2/3 bungeni, inaweza pitisha chochote inachohitaji. Lissu amevuliwa ubunge kwa sababu ya kibri chake cha kijinga, kama ana uwezo wa kuwa anaandika makala kwa kila tukio linaloendelea Tz Kwa nn ashindwe kuandika barua ya kikazi ?

Upinzani bila kuambiwa ukweli watazidi kudondoka, sababu badala ya kuwaambia mapungufu yao mnasujudu ujinga wao. Haiwezekani unajua kabisa unatakiwa utoe taarifa usipokuwepo bungeni ila hautoi kwa maksudi ukitegemea utaogopwa, sasa ndio Ubunge ameshavuliwa na 2020 hashindi Ubunge wala urais, Strategists wa CHADEMA ni wapumbavu, no offense na mnavyotetea ujinga wao ndio wanavyo endelea kuvurunda.

Kama unaamini hizo ni siasa za kufikirika basi subiri, nitakuvutia huu uzi hayo yalianza kutokea maana huna uwezo wa kuona mbali. Hizi ni tabia za viongozi wengi wa kiafrika na ndio walivyofanya mpaka wakakaa madarakani zaidi ya miongo miwili, tena bila ridhaa ya umma, bali kupitia hizo taasisi walizozipata nguvu. Vinginevyo ungeniambia kwanini msajili anageuzwa kuwa ndio final say wa taasisi hizo.

Uko sahihi kwamba hatashinda urais au ubunge hiyo 2020. Sio kwasababu hakubaliki na wananchi, bali katiba inayompa rais mamlakani makubwa ya kuwa muamuzi wa nani kutangazwa mshindi. Haya tumeyaona kwa macho yetu kwenye chaguzi zote za marudio chini ya awamu hii jinsi wapinzani walivyofanyiwa ukatili wa wazi, na hujuma za wazi wazi katika box kura, tena kwa uratibu wa vyombo vya dola na tume ya uchaguzi! Na hayo yote yana baraka zake, kwa kutumia madaraka yake kupitia katiba hii yenye mapungufu ya dhahiri.
 
Hakika siyo siri tena kuwa serikali ya utawala wa awamu ya tano inafanya juhudi kubwa sana kuwafuta kwa hila wabunge wa upinzani, hususani Chadema

Tumeona wabunge wa Chadema "wakinunuliwa" ili wahame kutoka Chadema na kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli za kuleta maendeleo

Hata hivyo juhudi hizo ni kinyume kabisa na faksafa anayoitangaza Rais mwenyewe kwenye majukwaa ya kisiasa, kuwa maendeleo hayana chama

Tumeshuhudia wabunge kadhaa wa Chadema wakihama chama chao cha Chadema na kujiunga na CCM na kupitishwa "automatically" kuwa wagombea tena wa ubunge

Tumeona pia juhudi kubwa za hawa wakereketwa wakubwa wa CCM, maDED waliopigwa chini na mahakama kuu, kuwa hawastahili kuendelea kusimamia chaguzi zozote za hapa nchini, wakiwatangaza wagombea hao waliohamia CCM wakipita bila kupingwa!

Kumekuwepo pia na juhudi kubwa "kuwapunguza" kwa hila mbalimbali wabunge wa Chadema wa kuchaguliwa na wananchi wao kwenye majimbo yao

Tulianza kuona hizi hila zikifanywa kumwondoa kwenye ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari

Lakini lililostua dunia mzima, ni huu uamuzi wa majuzi wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania, Mheshimiwa Ndugai wa kumvua ubunge wa jimbo la Singida Mashariki, Mheshimiwa Tundu Lissu, kwa madai kuwa ni mtoto na yeye Spika, hajui Tundu Lissu alipo!

Hivi ni nani katika dunia hii asiyejua Tundu Lissu alipo, isipokuwa yeye Spika peke yake!

Kila mtu anafahamu namna Tundu Lissu alivyomiminiwa risasi zaidi ya 38 kwenye gari lake, kwenye makazi ya viongozi wa serikali, tena mchana kweupe

Lakini kwa kudra ya Mwenyezi Mungu, amemuokoa na kifo, ambacho hao watesi wake wakikuwa wamekipanga kwa Lissu

Miongoni ya watu waliokwenda kumwona Dodoma hospital, alikokimbizwa baada ya kupata majetaha hayo, alikuwa ni Spika mwenyewe

Kutokana na hali aliyokuwa nayo, ilibidi uamuzi wa dharula uchukuliwr siku hiyo ya tarehe 7/9/2019 wa kumuhamishia hospitali ya Agakhan jijini Nairobi, huku Spika mwenyewe akiunga mkono uamuzi huo

Sasa ninachojiuliza iweje leo Spika Ndugai, adai kuwa hajui akipo, Mheshimiwa Tundu Lissu??

Ni dhahiri hizi ni njama za wazi za serikali hii ya utawala wa awamu ya tano, ya kutaka kuwapungiza wabunge hao waliochagiliwa na wananchi katika majimbo yao

Swali la msingi ambao sisi wananchi tunajiuliza ni hilo, hivi hizi juhudi kubwa sana xinazofanyika na Bunge letu la kuwapungiza wabunge wa kuchahiliwa na wananchi, lengo lake halisi ni nini??

Naomba mwenye kujua lengo hilo anijuze na Mimi ili nielewe
JIBU NI ILI ::: kiongozi wenu Mkuu anataka aweke wabunge wengi wa chama chake, ili adhma yake karibia na Mwaka wa mwisho wa muhula wake, ipelekwe hoja kwenye bunge kuwa ifanyike marekebisho, bwana Mkubwa aongoze tena vipindi kumi vingine,

wataandaliwa wapambe mitaani na majimboni, na ndani ya chama chake na vyama mamluki, wakipita mitaani na Kwenye media kueneza propaganda kuwa bwana mkubwa aongezewe muda, katiba sio msahafu, mtaani itakuwa patashika, mwishowe bunge litapiga Kura kujua idadi ya wanaoafiki ilo suala, mwishowe life president is coming,,

HALI NDO ITAKUWA IVYO KWA 90%
 
Kama unaamini hizo ni siasa za kufikirika basi subiri, nitakuvutia huu uzi hayo yalianza kutokea maana huna uwezo wa kuona mbali. Hizi ni tabia za viongozi wengi wa kiafrika na ndio walivyofanya mpaka wakakaa madarakani zaidi ya miongo miwili, tena bila ridhaa ya umma, bali kupitia hizo taasisi walizozipata nguvu. Vinginevyo ungeniambia kwanini msajili anageuzwa kuwa ndio final say wa taasisi hizo.

Uko sahihi kwamba hatashinda urais au ubunge hiyo 2020. Sio kwasababu hakubaliki na wananchi, bali katiba inayompa rais mamlakani makubwa ya kuwa muamuzi wa nani kutangazwa mshindi. Haya tumeyaona kwa macho yetu kwenye chaguzi zote za marudio chini ya awamu hii jinsi wapinzani walivyofanyiwa ukatili wa wazi, na hujuma za wazi wazi katika box kura, tena kwa uratibu wa vyombo vya dola na tume ya uchaguzi! Na hayo yote yana baraka zake, kwa kutumia madaraka yake kupitia katiba hii yenye mapungufu ya dhahiri.
Wewe jamaa una fanya siasa za kufikirika, Magu hana nia na wala hawezi kukaa madarakani baada ya 2025, since watakao ongoza kumchomoa si hata upinzani wala wananchi ni CCM wenyewe. Kuna political animals huko ambao tayari wanajipanga kwa 2025 na 2035 kwa ambao umri unaruhusu so kufikiria tu Magu anaweza kuongeza muda wake ni siasa za kufikirika.
 
Wewe jamaa una fanya siasa za kufikirika, Magu hana nia na wala hawezi kukaa madarakani baada ya 2025, since watakao ongoza kumchomoa si hata upinzani wala wananchi ni CCM wenyewe. Kuna political animals huko ambao tayari wanajipanga kwa 2025 na 2035 kwa ambao umri unaruhusu so kufikiria tu Magu anaweza kuongeza muda wake ni siasa za kufikirika.

Nimekuuliza tena, kwanini anatengeneza sheria za kupora nguvu za maamuzi ya kitaasisi na kuwapa watu, naona unaishia kuzunguka tu. Nimerudia zaidi ya mara moja kuhusu nguvu zinazohamishwa kutoka mahakamani na kupewa watu kuwa final say. Sioni popote inapotoweka kwenye hilo. Nimekuambia hivyo ni viashiria vya wazi vya mtu huyu kujikita madarakani zaidi muda.

Nataka nikupe mfano mmoja mrahisi ili kukuonyesha hao ccm ikiwepo ww hawana nguvu dhidi yake, kuhusu maamuzi ya mtu, na wengi wao hawajausoma mchezo na wakiamka watakuwa wamechelewa. Mgombea wa ubunge wa ccm huwa anashindanishwa na wengine kupata mmoja, lakini nyakati za uchaguzi wa marudio maamuzi yalifanyika na genge dogo kupitisha wagombea waliotoka huko upinzani, wakapewa nafasi bila hata kukijua chama na wakapitishwa kibabe. Na kwenye hizo chaguzi zikafanyika rafu za wazi za kuvunja sheria ambazo leo mnasema maamuzi ya Lissu yamezitii hizo hizo, ili mgombea wa ccm atangazwe mshindi. Kama aliweza kufanya vile huku wanachama wakilalamika kichini chini, watamfanya nini hiyo 2025 akitanua goli? Kungekuwa na wanaccm wasafi ningekuelewa, lakini hawa wagombea ambao wakichomoza pua tu, Takukuru wanaambiwa wafuatilie skendo zao?
 
Mku ukiwaondoa au kuwanunua kuna faida gani wakati waliowawachagua wanabaki na Itikadi zao ndani ya mioyo yao
 
Mku wakati huo huyu anakiwa awe ktk hali gani.
Hats mgonjwa anawekwa kwenye hii ibara au
Mnachoshindwa kuelewa ni kwamba Bunge ni taasisi na siyo mtu binafsi. Kama ni taasisi basi ina taratibu na sheria zake. Spika kujua Tundu Lissu alipo hakufanyi sheria na taratibu za Bunge kuvunjwa au kutofuatwa. Tundu Lissu alipomiminiwa risasi hakuna aliemfukuza ubunge, kila mtu aliona hali tete aliyonayo na Bunge lilishiriki kwa namna moja au nyingine kuokoa uhai wake akiwa Dodoma. Japo chama chake baadae kiliamua kufuata utaratibu mwingine wa matibabu yake.

Kilichopelekea Bunge kuchukua hatua sasa, siyo tu kutojua Lissu alipo bali hata taarifa rasmi ya maendeleo ya matibabu yake haijulikani. Mara kadhaa Lissu ameombwa kufuata taratibu za kisheria kuhusu kutoa taarifa ya hali ya matibabu yake kwa muajiri wake lakini kutokana na kiburi amegoma kufanya hivyo. Badala yake amekua akilitaka Bunge kama linahitaji taarifa hiyo, likaombe kwa madaktari wanaomtibu. Sasa, hii ni dharau kubwa sana kwa taasisi kubwa kama ya Bunge.

Kiutaratibu mtumishi yoyote awe wa umma au sekta binafsi, anapoumwa au kuwa na dharura ya matibabu hasa ya muda mrefu, anapaswa yeye ndo atoe taarifa kwa muajiri wake na siyo muajiri kuanza kutafuta taarifa zake. Isitoshe matibabu ya Lissu hayagharamiwi na bunge hivyo ni ngumu kujua kama huyu mtu amepona au bado anaumwa. Hasa ukizingatia pia mwenendo wake, siyo kwamba yupo hospitali amelazwa mahututi kama ilivyokua mwanzo bali anaonekana akisafiri nchi mbalimbali na kufanya mahojiano na vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii. Hii inaleta tafsiri kwamba Afya yake imeimarika kwa kiasi kikubwa kuweza kutekeleza majukumu yake ya kibunge. Lakini hajawahi kuonekana bungeni wala kutoa taarifa yoyote.

Jambo lingine la kushangaza, watu wengi wamekua wakilaumu Lissu kufukuzwa ubunge kwa kuangalia sababu moja tu ya kutotoa taarifa za maendeleo matibabu yake. Lakini wanaiacha kwa makusudi sababu nyingine ya msingi ambayo imetajwa kikatiba nayo ni kutotoa taarifa ya Mali na Madeni kwa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Ukisoma ibara ya 71 (1)(c)(d) ya Katiba inasema wazi kabisa kwamba mbunge atakoma ubunge au ataacha kiti chake endapo (c) atakosa kuhudhuria vikao vya mikutano mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika na (d) itathibitishwa amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Yote haya Lissu ameenda kinyume nayo, Sasa kwanini asipoteze ubunge wake? Yeye ni nani mpaka awe juu ya Sheria na Katiba.
 
Mnachoshindwa kuelewa ni kwamba Bunge ni taasisi na siyo mtu binafsi. Kama ni taasisi basi ina taratibu na sheria zake. Spika kujua Tundu Lissu alipo hakufanyi sheria na taratibu za Bunge kuvunjwa au kutofuatwa. Tundu Lissu alipomiminiwa risasi hakuna aliemfukuza ubunge, kila mtu aliona hali tete aliyonayo na Bunge lilishiriki kwa namna moja au nyingine kuokoa uhai wake akiwa Dodoma. Japo chama chake baadae kiliamua kufuata utaratibu mwingine wa matibabu yake.

Kilichopelekea Bunge kuchukua hatua sasa, siyo tu kutojua Lissu alipo bali hata taarifa rasmi ya maendeleo ya matibabu yake haijulikani. Mara kadhaa Lissu ameombwa kufuata taratibu za kisheria kuhusu kutoa taarifa ya hali ya matibabu yake kwa muajiri wake lakini kutokana na kiburi amegoma kufanya hivyo. Badala yake amekua akilitaka Bunge kama linahitaji taarifa hiyo, likaombe kwa madaktari wanaomtibu. Sasa, hii ni dharau kubwa sana kwa taasisi kubwa kama ya Bunge.

Kiutaratibu mtumishi yoyote awe wa umma au sekta binafsi, anapoumwa au kuwa na dharura ya matibabu hasa ya muda mrefu, anapaswa yeye ndo atoe taarifa kwa muajiri wake na siyo muajiri kuanza kutafuta taarifa zake. Isitoshe matibabu ya Lissu hayagharamiwi na bunge hivyo ni ngumu kujua kama huyu mtu amepona au bado anaumwa. Hasa ukizingatia pia mwenendo wake, siyo kwamba yupo hospitali amelazwa mahututi kama ilivyokua mwanzo bali anaonekana akisafiri nchi mbalimbali na kufanya mahojiano na vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii. Hii inaleta tafsiri kwamba Afya yake imeimarika kwa kiasi kikubwa kuweza kutekeleza majukumu yake ya kibunge. Lakini hajawahi kuonekana bungeni wala kutoa taarifa yoyote.

Jambo lingine la kushangaza, watu wengi wamekua wakilaumu Lissu kufukuzwa ubunge kwa kuangalia sababu moja tu ya kutotoa taarifa za maendeleo matibabu yake. Lakini wanaiacha kwa makusudi sababu nyingine ya msingi ambayo imetajwa kikatiba nayo ni kutotoa taarifa ya Mali na Madeni kwa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Ukisoma ibara ya 71 (1)(c)(d) ya Katiba inasema wazi kabisa kwamba mbunge atakoma ubunge au ataacha kiti chake endapo (c) atakosa kuhudhuria vikao vya mikutano mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika na (d) itathibitishwa amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Yote haya Lissu ameenda kinyume nayo, Sasa kwanini asipoteze ubunge wake? Yeye ni nani mpaka awe juu ya Sheria na Katiba.

Ni kweli kabisa kwa sababu hata aliposhambuliwa ni katiba ndiyo iliyofuata na kukamilisha upelelezi na matibabu alitibiwa kwa mujibu wa hiyo katiba. Hongera sana mamlaka husika kwa kusimammia sheria na katiba kwenye tukio la Lissu kila mtu anaona namna sheria zilivyofanya kazi yake kukamata waliomshambulia na kumhudumia matibabu.

Hivi ni wote tuliomuona Lissu pale Dodoma kweli au wengine hawakuoma, kwa yale madhira aliyopitia kulikuwa na taratibu hadi lile shambulizi ambalo alishatoa taarifa kuwa gari linamfuatilia. Waliohusika kumshambulia ndiyo wamemvua ubunge sasa hakuna haja ya maneno mengi hakuna ambaye haelewi kinachoendelea na hao wanaoitwa wasiojulikana siwalijulikana pale Musoma Mjini mbona kila mtanzania anaelewa kila kitu.

Tunapoteza muda wetu mwingi kuongea taratibu zipi za kupigana risasi nazo ziko kwenye katiba ipi hiyo. Shame on all who behind this shameful decision.
 
Aw
Hakika siyo siri tena kuwa serikali ya utawala wa awamu ya tano inafanya juhudi kubwa sana kuwafuta kwa hila wabunge wa upinzani, hususani Chadema

Tumeona wabunge wa Chadema "wakinunuliwa" ili wahame kutoka Chadema na kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli za kuleta maendeleo

Hata hivyo juhudi hizo ni kinyume kabisa na faksafa anayoitangaza Rais mwenyewe kwenye majukwaa ya kisiasa, kuwa maendeleo hayana chama

Tumeshuhudia wabunge kadhaa wa Chadema wakihama chama chao cha Chadema na kujiunga na CCM na kupitishwa "automatically" kuwa wagombea tena wa ubunge

Tumeona pia juhudi kubwa za hawa wakereketwa wakubwa wa CCM, maDED waliopigwa chini na mahakama kuu, kuwa hawastahili kuendelea kusimamia chaguzi zozote za hapa nchini, wakiwatangaza wagombea hao waliohamia CCM wakipita bila kupingwa!

Kumekuwepo pia na juhudi kubwa "kuwapunguza" kwa hila mbalimbali wabunge wa Chadema wa kuchaguliwa na wananchi wao kwenye majimbo yao

Tulianza kuona hizi hila zikifanywa kumwondoa kwenye ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari

Lakini lililostua dunia mzima, ni huu uamuzi wa majuzi wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania, Mheshimiwa Ndugai wa kumvua ubunge wa jimbo la Singida Mashariki, Mheshimiwa Tundu Lissu, kwa madai kuwa ni mtoto na yeye Spika, hajui Tundu Lissu alipo!

Hivi ni nani katika dunia hii asiyejua Tundu Lissu alipo, isipokuwa yeye Spika peke yake!

Kila mtu anafahamu namna Tundu Lissu alivyomiminiwa risasi zaidi ya 38 kwenye gari lake, kwenye makazi ya viongozi wa serikali, tena mchana kweupe

Lakini kwa kudra ya Mwenyezi Mungu, amemuokoa na kifo, ambacho hao watesi wake wakikuwa wamekipanga kwa Lissu

Miongoni ya watu waliokwenda kumwona Dodoma hospital, alikokimbizwa baada ya kupata majetaha hayo, alikuwa ni Spika mwenyewe

Kutokana na hali aliyokuwa nayo, ilibidi uamuzi wa dharula uchukuliwr siku hiyo ya tarehe 7/9/2019 wa kumuhamishia hospitali ya Agakhan jijini Nairobi, huku Spika mwenyewe akiunga mkono uamuzi huo

Sasa ninachojiuliza iweje leo Spika Ndugai, adai kuwa hajui akipo, Mheshimiwa Tundu Lissu??

Ni dhahiri hizi ni njama za wazi za serikali hii ya utawala wa awamu ya tano, ya kutaka kuwapungiza wabunge hao waliochagiliwa na wananchi katika majimbo yao

Swali la msingi ambao sisi wananchi tunajiuliza ni hilo, hivi hizi juhudi kubwa sana xinazofanyika na Bunge letu la kuwapungiza wabunge wa kuchahiliwa na wananchi, lengo lake halisi ni nini??

Naomba mwenye kujua lengo hilo anijuze na Mimi ili nielewe
Awamu ya pili ya jiwe katiba itabadilishwa aendelee, hayo matayarisho
 
JIBU NI ILI ::: kiongozi wenu Mkuu anataka aweke wabunge wengi wa chama chake, ili adhma yake karibia na Mwaka wa mwisho wa muhula wake, ipelekwe hoja kwenye bunge kuwa ifanyike marekebisho, bwana Mkubwa aongoze tena vipindi kumi vingine,

wataandaliwa wapambe mitaani na majimboni, na ndani ya chama chake na vyama mamluki, wakipita mitaani na Kwenye media kueneza propaganda kuwa bwana mkubwa aongezewe muda, katiba sio msahafu, mtaani itakuwa patashika, mwishowe bunge litapiga Kura kujua idadi ya wanaoafiki ilo suala, mwishowe life president is coming,,

HALI NDO ITAKUWA IVYO KWA 90%

Uko sahihi sana. Sasa hivi kwenye nyumba za ibada unaona kabisa kuna viongozi wa dini wanamsifia Magufuli na kumpigia kampeni bila hofu, lakini ikitokea kiongozi yoyote wa dini akamkosoa au kukosoa uongozi wake utasikia akiambiwa anachanganya siasa na dini na hata ataanza kuzongwa zongwa na taasisi za kimamlaka. Mfano wa viongozi wa dini wanaomsifia Magufuli wazi wazi madhabahuni ni mzee wa upako, tena hata vipindi vyake vinarushwa na TV Kama channel 10 nk akiwa anamsifia Magufuli. Tuliona viongozi wa dini waliotoa waraka jinsi serekali ilivyokuja juu kwamba dini inachanganywa na siasa. Iwapo huyo kiongozi yuko kimya akisifiwa kwenye nyumba za ibada, lakini akikosolewa hataki, atashindwa kujiongezea kukaa madarakani zaidi ya muda husika?
 
Ndugai kama mtu binafsi anajua Lissu alipo. Je Bunge kama taasisi inajua? Kuna any documents zinazonesha Lissu alipo na taarifa zake za maendeleo ya matibabu? Jifunzeni kutofautisha kati ya Ndugai na Speaker.
 
Mnachoshindwa kuelewa ni kwamba Bunge ni taasisi na siyo mtu binafsi. Kama ni taasisi basi ina taratibu na sheria zake. Spika kujua Tundu Lissu alipo hakufanyi sheria na taratibu za Bunge kuvunjwa au kutofuatwa. Tundu Lissu alipomiminiwa risasi hakuna aliemfukuza ubunge, kila mtu aliona hali tete aliyonayo na Bunge lilishiriki kwa namna moja au nyingine kuokoa uhai wake akiwa Dodoma. Japo chama chake baadae kiliamua kufuata utaratibu mwingine wa matibabu yake.

Kilichopelekea Bunge kuchukua hatua sasa, siyo tu kutojua Lissu alipo bali hata taarifa rasmi ya maendeleo ya matibabu yake haijulikani. Mara kadhaa Lissu ameombwa kufuata taratibu za kisheria kuhusu kutoa taarifa ya hali ya matibabu yake kwa muajiri wake lakini kutokana na kiburi amegoma kufanya hivyo. Badala yake amekua akilitaka Bunge kama linahitaji taarifa hiyo, likaombe kwa madaktari wanaomtibu. Sasa, hii ni dharau kubwa sana kwa taasisi kubwa kama ya Bunge.

Kiutaratibu mtumishi yoyote awe wa umma au sekta binafsi, anapoumwa au kuwa na dharura ya matibabu hasa ya muda mrefu, anapaswa yeye ndo atoe taarifa kwa muajiri wake na siyo muajiri kuanza kutafuta taarifa zake. Isitoshe matibabu ya Lissu hayagharamiwi na bunge hivyo ni ngumu kujua kama huyu mtu amepona au bado anaumwa. Hasa ukizingatia pia mwenendo wake, siyo kwamba yupo hospitali amelazwa mahututi kama ilivyokua mwanzo bali anaonekana akisafiri nchi mbalimbali na kufanya mahojiano na vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii. Hii inaleta tafsiri kwamba Afya yake imeimarika kwa kiasi kikubwa kuweza kutekeleza majukumu yake ya kibunge. Lakini hajawahi kuonekana bungeni wala kutoa taarifa yoyote.

Jambo lingine la kushangaza, watu wengi wamekua wakilaumu Lissu kufukuzwa ubunge kwa kuangalia sababu moja tu ya kutotoa taarifa za maendeleo matibabu yake. Lakini wanaiacha kwa makusudi sababu nyingine ya msingi ambayo imetajwa kikatiba nayo ni kutotoa taarifa ya Mali na Madeni kwa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Ukisoma ibara ya 71 (1)(c)(d) ya Katiba inasema wazi kabisa kwamba mbunge atakoma ubunge au ataacha kiti chake endapo (c) atakosa kuhudhuria vikao vya mikutano mitatu mfululizo bila ya ruhusa ya Spika na (d) itathibitishwa amevunja masharti ya sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Yote haya Lissu ameenda kinyume nayo, Sasa kwanini asipoteze ubunge wake? Yeye ni nani mpaka awe juu ya Sheria na Katiba.
Waraka mreeeefu lakini ni pumba tupu,
 
Back
Top Bottom