Asbm
Member
- Jun 26, 2019
- 38
- 33
Ndugu WanaJf, Heshima kwenu
Tunapoelekea kufunga mwaka, kuna matukio mengi mbele yake yote yakihitaji fedha nyingi kuyafanikisha.
Kwa mfano tu, kuna sikukuu kubwa ya kuadhimisha kuzaliwa kwa mtoto Yesu Kristo (25 Dec-Christmass), Boxing day, na kuukaribisha mwaka mpya. Lakini isitoshe kwa wazazi wana watoto wanaotakiwa kuwapeleka shule hivo ada zahtajika. Kuna wapangaji ambao tunatakiwa kulipia kodi za nyumba kwa wenyenyumba.
Yawezekana muda ukawa hautoshi kama hukujipanga mapema kwa mwaka mzima kufanikisha hilo na kuishia kusumbua ndugu, jamaa na marafiki ili wakuazime fedha kufanikisha mahitaji yako.
Ni kipindi ambacho kila mmoja anakuwa na matumizi makubwa hivo unapoomba mahitaji yako kwa mtu na akashindwa kukusaidia usichukie.
Nakumbushia tu ili tusije kuishia kukwazana na kuchukiana eti kwa sababu tu tumeshindwa kusaidiana. Ni muda mzuri wa kujipanga tunapoelekea mwishoni mwa mwaka ili mwakani tuwe na vyanzo vya mapato vitakavyosaidia kukidhi mahtaji yetu kwa miaka ya mbeleni inayokuja.
Ahsanteni
Tunapoelekea kufunga mwaka, kuna matukio mengi mbele yake yote yakihitaji fedha nyingi kuyafanikisha.
Kwa mfano tu, kuna sikukuu kubwa ya kuadhimisha kuzaliwa kwa mtoto Yesu Kristo (25 Dec-Christmass), Boxing day, na kuukaribisha mwaka mpya. Lakini isitoshe kwa wazazi wana watoto wanaotakiwa kuwapeleka shule hivo ada zahtajika. Kuna wapangaji ambao tunatakiwa kulipia kodi za nyumba kwa wenyenyumba.
Yawezekana muda ukawa hautoshi kama hukujipanga mapema kwa mwaka mzima kufanikisha hilo na kuishia kusumbua ndugu, jamaa na marafiki ili wakuazime fedha kufanikisha mahitaji yako.
Ni kipindi ambacho kila mmoja anakuwa na matumizi makubwa hivo unapoomba mahitaji yako kwa mtu na akashindwa kukusaidia usichukie.
Nakumbushia tu ili tusije kuishia kukwazana na kuchukiana eti kwa sababu tu tumeshindwa kusaidiana. Ni muda mzuri wa kujipanga tunapoelekea mwishoni mwa mwaka ili mwakani tuwe na vyanzo vya mapato vitakavyosaidia kukidhi mahtaji yetu kwa miaka ya mbeleni inayokuja.
Ahsanteni