karagwe2005
Member
- Apr 26, 2012
- 27
- 20
Jamani siwezi kumsahau Bi Eda Sanga na sauti yake. Pia English Service of Radio Tanzania akiwa anasoma taarifa. Those good days are gone!
Mchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu
Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii
Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee
Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa
Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa
Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee
Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa
Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi
Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.
2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu
3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa
4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa
5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa
6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji
7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa
8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo
Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu
ngoja nichangamkie fursaaaNitafutie audio ya haya matangazo ntakulipa dau nzuri sana.
Are they real best days?the good days are over, the best days are now!
Kipindi cha mkoa kwa mkoa na pia kuandama kwa mwezi mnasubiri RTD itangaze saa tano usiku!Mama na mwana kila j2 saa 8 mchana. Mazungumzo baada ya habari kila baada ya taarifa ya habari ya saa1 asubuhi na saa2 usiku
Baba yake juma katia viraka vinauliza umekuja lini nimekujaa janaaaa narudi leooo maendeleeoooooooo viraaaakaaa viraaaaaaaka viraaa aaakaaa aaaaaaaKipindi cha Pwagu na Pwaguzi
Matangazo ya vifo
Maneno hayoooo
Mazungumzo baada ya Habari
Ile jingle ya habari za michezo tulikuwa tunaimba hivi " baba yake juma ana mavilaka..anamavilaka.
.anamavilakaaaaaaa!'...
Sikiliza bwana umeme..
tingtingtingtingtingtingtingiiiiiiiiiiiiiiiii
HIVI SASA NI SAA KUMI KAMILI....
Jangala mwanae aliitwa Mshamu hizo nyimbo nakumbuka asubuhi jua la asubuhi la pendeezaaaa jua jua juaaaaaa daaah.... Pia wimbo wa muongo na mulozi ni watu wa kuchoomaaaaa1 Taarifa ya habari na ile ngoma ya yule mzee asiyeona na ngoma kumi
2. Wakati wa kazi. "ujuzi niliupata hapa hapa kazini"
3. Hii ni kwaresimaa.
4. Lala salama.
5. Vipindi vya masomo ya shule za msingi tukikaa darasa zima watoto 40 na kusikiliza mwalimu wa redio. Wengine hata hiyo redio ilikuwa haisikiki vizuri lakini ilikuwa lazima mhu!
6. Kipindi cha wagonjwa. (Ajuaye bwana Mungu kwa mzima kuwa mfu, mgonjwa kuwa salaaaama leo tunatoa pole).
7. Mchezo wa Redio (Mkataa pema pabaya panamwita) Sikosi hapo. watu mnakaa kana kwamba mnawaona akina Jangala na wenzie na yule mwenye sauti kubwa na yule mama aliyekuwa na roho mbaya. Mtu unamchukia mtu hata bila kuona sura yake.
8. Mpiraa. Nakumbuka Yanga ilikuwa inacheza na Simba 74 tulipiga teke redio ya baba mimi na kaka yangu. Tulikula mkong'oto.
9. Hotuba za Mwalimu. Kila wakisema anaongea na wazee wa Dar ujue kuna kitu. Hapo hatutoki kama tupo likizo, wazee wote wa jirani wanakuja kwetu ili wasililize hotuba. Shuleni boarding kulikuwa na redio moja inazunguka kila bweni kila week.
10. Mchana na usiku mwema na miziki yake!! We acha akina Mbaraka Mwinshehe, Juma ******, Marijani Rajab, Western Jazz, Ndala Kasheba, Polisi Jazz, JKT, Tankat Almasi, Taarab nk. Samahani nimeandika mengi lakini ni kama therapy kutoa haya ya sasa kichwani. Big up mtoa mada.
majogoo yanawika vijijini, na nyota za mbinguni zinawaka, wazalendo amkeni tufanye kazi sasa ... (Marijan wa Rajab)Kumekucha sasa kumekuchaaa...
kumekuchaa sasa kumekuchaa na jogoo kijijini anawikaaaa watu wote amkeni twende tutafanye kaziKumekucha sasa kumekuchaaa...
Siku hizi hawa Facebook wanasikiliza akina kibonde na wazee wa kukojoza basiVijana mpo Facebook na Instagram na humu mmejazana sana kule Chit-chat na MMU..
Muhasisi=muasisiAksante Rtd bila kumsahau muhasisi wa taifa letu Nyerere
Siku hizi hawa Facebook wanasikiliza akina kibonde na wazee wa kukojoza basi
Mwenye kipindi alikufa aisee RIP Bi Sarah DumbaCheiii cheiii shangaziiiiiii
Ninatizama dirishani ohoo, naona ni mvua inanyesha oho hakuna kilichobakia oho ila ni huzuni na uchungu ehe, mwingine ni Asha usifate mambo ya dunia asha wewe kumbuka wemaaa Tabora jazz. Tulikuwa tunakacha Math siku nyingine na physics ili kusikia vigongo hivyo. Mhu.Jangala mwanae aliitwa Mshamu hizo nyimbo nakumbuka asubuhi jua la asubuhi la pendeezaaaa jua jua juaaaaaa daaah.... Pia wimbo wa muongo na mulozi ni watu wa kuchoomaaaaa