Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Daah wanangu kama kuna mtu ana wimbo wa yule mzee anaepiga ngoma kati ya 12 au 17 unaopigwa kabla ya habari auweke humu ndugu
 
Take a break, na tujikumbushe enzi zile za RTD, ambapo kulikuwa hakuna FMs rado kama sasa. Hakika kulikuwa na watangazaji, vipindi bomba na hata nyimbo za kutambulisha vipindi zilikuwa makini sana. Hebu ngoja niwakumbushe baadhi ya watangazaji wa wakati huo.

1. Nassoro Nsekeli- alikuwa na sauti kama ya mafua hivi alikuwa mtaalamu wa kipindi cha Majira- ndiye aliyetangaza kifo cha Nico Zengekala

2. Bujago Izengo wa Kadago- Kibesi chake kilikuwa safi sana

3. David Wakati (DG) - kipindi cha Nipe habari- Kwaherini wote, mungu awalinde na mmbaki salama, mungu akipenda..............

4, Khalid Ponera- Zilipendwa

5. Ahmed Kipozi- taarifa ya habari

6. Hassan Mkumba- matangazo ya vifo

7. Siwatu Luwanda

8. Salama Mfamao
9. Mohamed Amani (Mohamed Dahman)

10. Salim Seif Nkamba

12. CHisunga Steven- kipindi cha Ugua pole duu

13. Bathoromeo KOmbwa (bati Kombwa) - WAkati wa Kazi

14. Ahmed Jongo- Mpira

15. Christina Chokunogela

16. Dominic Chilambo- Mpira

17. Edda Sanga
18. Debora Mwenda- Mama na Mwana
19. Aloycea Maneno- Ombi lako, cheichei Shangazi, mama na mwana

Duu nawamiss sana hawa watu tofauti na watangazaji wa sasa


Jamani Rocus Matipa alifariki mwezi uliopita kimya kimya, wakati alikuwa Mtangazaji nguli wa enzi hizo?
 
Nakumbuka enzi hizo, mwanzoni mwa miaka ya 2000, kulikuwa na watangazaji na vipindi maarufu vilivyopeta kipindi hicho.
MISANYA BINGI WA REDIO ONE- Enzi zile alikuwa na kipindi chake cha chemsha bongo, ilikuwa burudani sana.
MARTHA NGWILA WA REDIO Tanzania, huyu alivuma sana na style yake ya kuripoti hasa kipindi cha harakati.
FRED WAA AKIWA REDIO FREE- Kipindi cha je huu no ungwana na vodacom burudani zaidi sindano tano za moto, hatari sana.
SEKION DAVID AKIWA EATV- enzi zile na kipindi cha city sounds
BETTY MKWASA AKIWA ITV-Alikuwa anatangaza habari.
RUKIA MTINGWA AKIWA ITV-AKITANGAZA HABARI.
PRINCE BAINA KAMUKULU.
FREDRICK BUNDALA- RADIO FREE KIPINDI CHA SITASAHAU
RAHABU FREDY- Kipindi cha search line, radio free.
ROSE CHITALA- Radio one, chombeza time.
GABRIEL ZAKARIA- Akiwa radio free, kipindi cha usiku.
JULIUS NYAISANGA- Akiwa ITV akisoma habari.
MOSES JUSTINE- Radio one, kipindi cha mtaa w mangoma.
RAINFRED MASAKO- ITV akitangaza matukio ya wiki.
SAMADA HASAN MADUHU- Star TV akitangaza kipindi cha anga za kimataifa.
JUMA AHMED BARAGHAZA- REDIO free, kipindi cha Bangua bongo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
BETTY MKWASA, huyo Shangazi namkubali sana.

Akimaliza Taarifa ya Habari, inafuata kipindi cha JIJI LETU.

Jamani
 
Haitotokea kama Sunday Shomari na Monica Mfumia wa ITV.

Walikuwa wanapendezesha sana Kipindi chao
 
Back
Top Bottom