Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Abdalah Mlawa na kipindi chake cha Kijaruba saa nne Usiku,

Chilambo Diminic akiwa mwanza na Charles Hilal akiwa dar wakati wa ligi kuu ya kipindi hicho
 
Ahlan wa sahalan.

Nimekumbuka mbali sana.

Namkumbuka Michael Katembo pale studio 3 na kipindi chake cha Midundo asilia.
Namkumbuka Mzee Angalieni Mpendu idara ya utangazaji biashara.
namkumbuka Edda Sanga wa chumba cha habari.

Nili enjo sana field yangu enzi hizo.

Sitaweza kumsahau Mama Tatu Mbotoni ambaye alikuwa mkuu wa maktaba ya rekodi. Klla tulichofanya au kuhitaji tulipitia kwake.

Sijawasahau wazee etu Mafundi mitambo.
Mzee Edmund Mria (mchaga)
Ali Said Tunku
Noel Namaloe

pamoja na wale engine wa OB.

Nilienjoy sna field angu chini ya wakongwe hawa.

Bila kumsahau fundi mitambo Domitila Urassa (RIP)
 
Kulikuwa na Karim Besta, Mohamed Kisengo, Jane Nonge, Ananilea Nkya Twende na Wakati, Bakari Msulwa, Idrisa Sadala,

Yuko wapi Bujago Izengo wa Kadago
 
Duuh!naona hakuachwa mtangazaji kila ninaye mkumbuka naona kesha tajwa sana sana sioni jina la peter makorongo !
 
Wengi wametajwa mbona wafuatao hamjawatendea haki? Wapi Suleiman Hegga wapi Suleiman Kumchaya wapi Suleiman Muhogora .... Ongezeni
 
Halima Kihemba
Titus Philipo huyu alikua R.T.D Tabora
Salim Mbonde
Suedi Mwinyi - genius wa kutangaza mpira nakumbuka nilikua nikisikiliza gemu za simba na yanga redioni uutadhani nashuhudia kwenye luninga au uwanjani
Betty Mkwasa
........................
........................
 
Mimi katika vipindi vya kutuma salam basi alikuwa akikaa Uncle J (Julius Nyaisanga Super Tall) nilikuwa sibanduki pembeni ya redio mpaka kipindi kiishe maana alikuwa anaweka debe nzito sana au akiamua kushuka kwa jirani zetu kule Zaire pia alikuwa anavipanga vitu ambavyo vinakufanya hutaki kuondoka, halafu alikuwa anawajua wanadendi wengi kwa majina na kuanza kuwataja mmoja baada ya mwingine.

Nina swali. Kuna kile kipindi maarufu sana cha usiku nadhani kilikuwa kuanzia saa 4 na robo usiku (baada ya taarifa ya habari) weekdays kiliitwa kijaluba. Hivi wale akina dada waliokuwa wanapiga kelele kuashiria kipindi kile walikuwa wanasema maneno gani? Kuna jamaa aliwahi kutifunga kamba ofisini eti walikuwa wanase mimi yangu nyeupe babu, na mwingine anasema mimi yangu nyeusi babu na mwingine anaitikia mimi yangu nyekundu babu na mwingine anasema mimi yangu bukta ;) nilijaribu sana kusikiliza walikuwa wanasema nini lakini sikupata kitu.
 
Mimi katika vipindi vya kutuma salam basi alikuwa akikaa Uncle J (Julius Nyaisanga Super Tall) nilikuwa sibanduki pembeni ya redio mpaka kipindi kiishe maana alikuwa anaweka debe nzito sana au akiamua kushuka kwa jirani zetu kule Zaire pia alikuwa anavipanga vitu ambavyo vinakufanya hutaki kuondoka, halafu alikuwa anawajua wanadendi wengi kwa majina na kuanza kuwataja mmoja baada ya mwingine.

Nina swali. Kuna kile kipindi maarufu sana cha usiku nadhani kilikuwa kuanzia saa 4 na robo usiku (baada ya taarifa ya habari) weekdays kiliitwa kijaluba. Hivi wale akina dada waliokuwa wanapiga kelele kuashiria kipindi kile walikuwa wanasema maneno gani? Kuna jamaa aliwahi kutifunga kamba ofisini eti walikuwa wanase mimi yangu nyeupe babu, na mwingine anasema mimi yangu nyeusi babu na mwingine anaitikia mimi yangu nyekundu babu na mwingine anasema mimi yangu bukta ;) nilijaribu sana kusikiliza walikuwa wanasema nini lakini sikupata kitu.

Hahaaaaaaaaa BAK una vituko wewe..Haya maneno hata mimi mpaka leo sijajua yalikuwa ni maneno gani aisee...Hiki ni kipindi nilichokipenda sana enzi hicho,hasa madoido na mikogo ya mtangazaji wake Abdallah Mlawa...Mkuu pia kulikuwa na kipindi cha Ngano za Muziki wakikumbuka hiki???,yaani hapa ilikuwa zakusanywa nyimbo zenye maudhui yanayoendana kisha latengenezwa/launganishwa bonge la stori
 
Hahaaaaaaaaa BAK una vituko wewe..Haya maneno hata mimi mpaka leo sijajua yalikuwa ni maneno gani aisee...Hiki ni kipindi nilichokipenda sana enzi hicho,hasa madoido na mikogo ya mtangazaji wake Abdallah Mlawa...Mkuu pia kulikuwa na kipindi cha Ngano za Muziki wakikumbuka hiki???,yaani hapa ilikuwa zakusanywa nyimbo zenye maudhui yanayoendana kisha latengenezwa/launganishwa bonge la stori

Nimeshasema Mkuu Balantanda naona tunashabihiana kwa mengi sana Mkuu :). Naam kipindi hicho kilikuwa kinaendeshwa na Abdallah Mlawa...yaani nilikuwa nayasikiliza yale maneno ili nijue wanasema nini mpaka nikakata tamaa. Hicho nacho cha Ngano ya Muziki kilikuwa ni moja ya vipindi ambavyo nilivipenda sana na stori zilizokuwa zinatungwa kuendeana na zile nyimbo zilikuwa safi sana. Miaka ile RTD ilikuwa bomba sana siku hizi hata sijui kama inapata wasikilizaji wengi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. Aisee ofisini kwangu kulikuwa na jamaa wanafunga kamba kali sana yaani ilikuwa ni raha tupu mengine nikiyakumbuka hadi hii leo huwa nacheka tu.
 
Jamani hivi Jacob Tesha yuko wapi? ukitaka kusikia "bass" ya kufurahisha basi ulikuwa unatakiwa usikilize taarifa za habari.
 
Back
Top Bottom