Tujikumbushe Serikali ilivyotoa tamko juu ya adhabu ya viboko kwa wanafunzi

cheusimangala_

Senior Member
Dec 1, 2018
114
174
Ole nasha.jpg





Serikali ilitoa tamko rasmi kuhusu adhabu ya kuchapwa fimbo kwa wanafunzi wanapokuwa shuleni, na kuwapa onyo walimu kutembea na fimbo katika eneo la shule ama kuwachapa wanafunzi.
kupitia Bungeni Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, William Tate OleNasha, alisema kuna waraka ambao ulitolewa kisheria kwa wadau wa elimu kuhusu uchapwaji wa viboko, ambao ulisema wazi utaratibu huo wa uchapwaji, na lazima iombwe kibali na kutolewa na maandishi.
“Haitakiwi vizidi viboko vinne na lazima kiombwe kibali cha kufanya hivyo, ni marufuku kumchapa mwanafunzi kinyume na taratibu na sheria, lakini vile vile kwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria na hatua zitachukuliwa
 
Mkuu wanasiasa wa nchi hii wafanye siasa sehemu zote ila kwenye suala la elimu wakae pembeni kidogo maana wanalikwamisha taifa .
 
Back
Top Bottom