Tujikumbushe NYAKATO SEC.Bukoba

chiborie

JF-Expert Member
Sep 24, 2011
491
345
wazee wa Nyakato mpo? unakumbuka nini hasa katika shule hii? mi nilifika pale mwaka 1996, Du! nilishangaa kuona viranja wakichapa wanafunzi wenzao, kiukweli form one hakua na thamani pale{kijana}. wakati huo mzee Kalema ndio alikua mkuu sijui yuko wapi kwa sasa! mchaka mchaka wa kila asubuhi saa kumi na moja na wakati huo lazima bogi lishuke. upande wa msosi ilikua noma, asubuhi lazimu mscramble nyuka, mchana ugali maharage ambayo hajakarakaniswa, mafunda ndio usisema hadi waalimu kama akina kadasto! na hapo form one mnapigwa kwanza ndio mnapata msosi, na baada ya msosi mnakimbia nyamshongoma kuleta maji! ila taaluma ilikua poa
 
Kweli mimi naikumbuka sana Nyakato kipindi hicho naingia form one mwaka 2002 system hiyo ya viongozi kuwachapa wanafunzi wenzao ilikuwa ni kugusa sababu nia na madhumuni ilikuwa hasa hasa kuwaogopesha wasichana wapate njia rahisi ya kuwapata. Bila ya kusahau cicrambling ya nyuka hata muda mwingine kukosa kabisa hiyo nyuka!!! Wazee wa nyakato wa kipindi hicho uongozi ulikuwa wa Mr.Ifunya, Exavery G. (a.k.a MIROSO), Kadasto, Kipara na wengine wengi kwa kweli shule ilikuwa ni mchakamchaka lakini na taaluma kipindi hicho ilkuwa juu, ambapo mtulifanikiwa mwaka wetu kwenda form five mwanafunzi 30 lilikuwa sio kazi ndogo. Pamoja na ukali wa hao walimu lkini walikuwa wanafundisha (Mungu hawabariki katika shughuri zao za kila siku). Walzee wa Nyakato kama mnakumbuka kijiwe cha CCM maarufu kama "CUBIC" WAZEE hapo ndiyo yalikuwa masikani yangu ya O-Level lkni mungu ni wa ajabu sana niliweza kufahuru kwenda form five MWANZA SENGEREMA kwa combination ya CGB. Nwapa big up wote mliopita NYAKATO SEC Mungu hawabariki.
 
Viranja kuchapa wanafunzi? Kwani yeye si mwanafunzi? Wangenifukuza shule siku hiyo hiyo sababu nisingekubali hata kwa hirizi kuchapwa na mwanafunzi mwenzangu, poleni mliopitia kadhia hiyo
 
Du! yaani hadi mwaka 2002 bado viranja walikua wanachapa! Nyakato kiboko, halafu umenikumbusha issue moja ya viranja kutafuta mademu wa day kwa nguvu, Nakumbuka mwaka 1996, HP alikua anaitwa Johnson John. Yaani jamaa alikua akiingia darasa la form one analazimishwa asalimiwe kama mwalimu vile, msipofanya hivyo kichapo kitatembea darasa zima. Kiukweli wakati huo pale Nyakato, HP alikua na tittle hata zaidi ya mwalimu wa kawaida, alikua hadi na kijana[ mwanafunzi mwenzake] wa kumchukulia chakula. kumfulia nguo etc.Ila speak english policy ilikua tait kinoma!
 
da! Umenikumbusha nyamishongoma,bugashani.nyakato viranja hasa HP wa bwaro na kiranja wa ulinzi waliendelea kuchapa hadi miaka ya hivi karibuni.nakumbuka,nakumbuka ukikosea ukapelekwa kwa HP,ulikua unachapwa viboko vitatu kabla ujaeleza,then ukijielezea ukashindwa kesi unachapwa vingine vitatu na adhabu nyingine.nakumbuka HP akitangaza kazi na muda huo huo mwalimu wa zamu akatangaza kazi, wanafunzi wanafanya kazi ya ya HP kwanza.
 
Back
Top Bottom