Tujikumbushe mechi zetu za utotoni, timu tulizochezea na mafanikio tuliyoziletea

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,860
12,291
Habari zenu ndugu zangu. Baada ya kuwajulia hali, ningepeenda niende moja kwa moja kwenye mada iliyonileta hapa. Bila shaka asilimia kubwa ya vijana tuliozaliwa na kukulia Dar es Salaam miaka ya 90, tuliwahi kucheza au kupitia michezo mbali mbali kama vile karate, ngumi, soka (mpira) na michezo mingine mbali mbali. Katika aina hizi za michezo, mi niliwahi kujifunza michezo miwili ambayo ni ngumi na soka.

Nikiwa na umri wa miaka 12 Tu, nlijifunza ngumi kupitia kwa baba angu mdogo ambae alikuwa anaishi Tabata makuburi kama unaenda kule ilipokuwa kambi ya jeshi zamani (sina uhakika kama kambi hiyo bado ipo mpaka Leo). Bamdogo alikuwa anapenda ngumi kwahiyo enzi za utoto wake alitumia muda wake mwingi kujifunza mchezo huo kupitia wataalam mbali mbali. Japo hakufanikiwa kufika mbali kutokana na changamoto za maisha, lkn aliamua kuutumia ujuzi huo wa kurusha madongo kuwagawia na wengine ambao walikuwa na lengo la kujilinda na vibaka wa mitaani (waliozaliwa na kukulia bongo miaka hiyo, nadhani wanafaham vizuri hali ya usalama ilivyokuwa mitaani).

Baada ya mimi kujifunza na kuujua mchezo huo na baadae kupambanishwa na watu mbali mbali ambao wapo walionipiga (asiekubali kushindwa, sio mshindani) na niliowachapa kweli kweli. Baadae pia nikajielekeza kwenye mchezo wa soka. Huku nilichezea timu mbali mbali, lkn nilichezea zaidi timu mbili za mtaani. Kwanza nilichezea timu moja ya mtaani iliyoitwa YOUNG KIDS ambapo tuliwahi kufika fainali mara tano, ila tukabeba kombe mara mbili.

Kombe la kwanza lilikuwa la jogoo wawili, na kombe la pili lilikuwa la jogoo mmoja.. bata mmoja na njiwa wawili. Baadae nilichezea timu nyingine ya mtaa ila mbali kidogo na maskani ya timu ya YOUNG KIDS FC. Timu hii ya pili iliitwa SUPER INTER SPORT CLUB. Nikiwa captain wa timu huku nikicheza namba 6 uwanjani, nikishirikiana na wachezaji wenzangu wenye bidii uwanjani, tulifanikiwa kuiingiza timu yetu fainali mara 8 na kubeba makombe manne.

Tumebeba makombe ya mbuzi mara 2, na makombe ya kawaida aina kama silver pia mara mbili. Ila pia pamoja na uwezo mkubwa wa kusakata kabumbu uwanjani, lkn kuna mechi zingine tulikuwa tunapoteza katika round za mwanzo mwanzo kutokana na makosa madogo madogo ya hapa na pale.

Hii ni baadhi ya michezo iliyokuwa inapendwa sana jijini Dar es Salaam miaka ya 90. Kama kuna mungine ambae aliwahi kupitia mchezo fulani na kuleta au kupata mafanikio kutokana na mchezo au michezo hiyo, anakaribishwa kuchangia uzi huu.

Asanteni sana.
 
Chama langu Ghetto FC la Mvomero Moro tulishinda kombe la Kuanzishwa kwa Wilaya ya Mvomero 2001 dhidi ya Townstars ya Dakawa Morogoro iliyokuwa na Mamluki akina Kipanya Marapa, Godfrey Masamaki, Chachala Muya, Ramadhani Aweso,Jumanne Shengo Tondolo, Kimune Mwita n.k.
 
Mpira ni mchezo wa hadharani.....
Mguu wangu wa kushoto Mungu aliweka kipaji Cha kipekee....walipenda kuni ita ROBIN VAN PERSIE

Uliitaji kua na macho na sekunde kadhaa mpira ukiwa mguuni kwangu kugundua kipaji Cha ajabu kilichopo ndani yangu

Tulikua na timu moja undisputed mtaan tulipeleka moto kwel kwel....

Mm ni mkimya na mpole Huwa sina maneno mengi.....

Mara nyingi ugenini uta nyimwa namba...kutokana na kutokujulikana ugenini.. uta baki nje kupiga dana dana....kosa likitokea au emergency nikapewa namba....sekunde kadhaa mpira ukiwa Mguu wa KUSHOTO watu hubakia midomo wazi na kustaajabu...

A-level niliwaacha hoi watu hawakuwai kutegemea kua ningeweza kua kipaji na uwezo nilio uonyesha Miaka miwili tuli ibuka mabingwa.....

Mpaka leo hii mm ni fundi wa kupiga mipira iliyokufa na penalty huwaga sikosei hata kipa awe OLIVER KHAN

Mpira wa miguu ungeninunulia magari na nyumba ila niliupotezea nili jua mpira kibongo bongo usingenipa maisha...

Countless watu walisimamisha magari yao na shughuli Zao kuja kunitizama na kunituza.....nilitabiliwa makubwa Sana ila mm nili udharau mpira wa miguu....nili amini Sana ELIMU ndio itanitoa kimaisha.

Wito wangu kwa Vijana kama una kipaji kifuate....
 
Niliichezea timu moja ikiitwa TABATA KIDS miaka 90s ilikuwa moto sema kupigana mara kwa mara kaka alinipiga marufuku na talent yangu iliishia hapo hapo hapo nilikuwa beki mshambuliaji mzuri akanirudisha kijijini
 
Niliichezea timu moja ikiitwa TABATA KIDS miaka 90s ilikuwa moto sema kupigana mara kwa mara kaka alinipiga marufuku na talent yangu iliishia hapo hapo hapo nilikuwa beki mshambuliaji mzuri akanirudisha kijijini
Alishajua talent yako ni ndondi na siyo mpira
 
Chama langu Ghetto FC la Mvomero Moro tulishinda kombe la Kuanzishwa kwa Wilaya ya Mvomero 2001 dhidi ya Townstars ya Dakawa Morogoro iliyokuwa na Mamluki akina Kipanya Marapa, Godfrey Masamaki, Chachala Muya, Ramadhani Aweso,Jumanne Shengo Tondolo, Kimune Mwita n.k.
Aisee mlikuwa na list nzuri ya wachezaji, na ndio maana mliweza kuchukua kombe la wilaya. Vipi uliendelea na mpira au uliachana nao au uliachana nao kwa sababu ya mambo mengine ya kimaisha?
 
Mpira ni mchezo wa hadharani.....
Mguu wangu wa kushoto Mungu aliweka kipaji Cha kipekee....walipenda kuni ita ROBIN VAN PERSIE

Uliitaji kua na macho na sekunde kadhaa mpira ukiwa mguuni kwangu kugundua kipaji Cha ajabu kilichopo ndani yangu

Tulikua na timu moja undisputed mtaan tulipeleka moto kwel kwel....

Mm ni mkimya na mpole Huwa sina maneno mengi.....

Mara nyingi ugenini uta nyimwa namba...kutokana na kutokujulikana ugenini.. uta baki nje kupiga dana dana....kosa likitokea au emergency nikapewa namba....sekunde kadhaa mpira ukiwa Mguu wa KUSHOTO watu hubakia midomo wazi na kustaajabu...

A-level niliwaacha hoi watu hawakuwai kutegemea kua ningeweza kua kipaji na uwezo nilio uonyesha Miaka miwili tuli ibuka mabingwa.....

Mpaka leo hii mm ni fundi wa kupiga mipira iliyokufa na penalty huwaga sikosei hata kipa awe OLIVER KHAN

Mpira wa miguu ungeninunulia magari na nyumba ila niliupotezea nili jua mpira kibongo bongo usingenipa maisha...

Countless watu walisimamisha magari yao na shughuli Zao kuja kunitizama na kunituza.....nilitabiliwa makubwa Sana ila mm nili udharau mpira wa miguu....nili amini Sana ELIMU ndio itanitoa kimaisha.

Wito wangu kwa Vijana kama una kipaji kifuate....
Dah mkuu.. i wish kipindi hicho tungekuwa team moja, yan kwa aina ya mpira wang na huu wa kwako basi nina uhakika tungeweza kujizolea makombe kibao na kuziletea heshima team zetu. Hongera mkuu kwa kupaji chako.
 
Niliichezea timu moja ikiitwa TABATA KIDS miaka 90s ilikuwa moto sema kupigana mara kwa mara kaka alinipiga marufuku na talent yangu iliishia hapo hapo hapo nilikuwa beki mshambuliaji mzuri akanirudisha kijijini
Pole mkuu labda bro aliogopa usije kupata majeraha ya kudumu ktk ugomvi wenu, kitu ambacho kingekusababishia majeraha makubwa ktk maisha yako.
 
Aisee mlikuwa na list nzuri ya wachezaji, na ndio maana mliweza kuchukua kombe la wilaya. Vipi uliendelea na mpira au uliachana nao au uliachana nao kwa sababu ya mambo mengine ya kimaisha?
Niliacha tokana na kusonga na maisha. Mara ya mwisho kucheza mpira nilikuwa nasoma SUA 2008. Nilikuwa naupiga mwingi sana. Sasa nikirudi nyumbani Mama yangu huwa ananikumbusha na kuniuliza "hivi ule mpira umeishia wapi"
 
Mpira ni mchezo wa hadharani.....
Mguu wangu wa kushoto Mungu aliweka kipaji Cha kipekee....walipenda kuni ita ROBIN VAN PERSIE

Uliitaji kua na macho na sekunde kadhaa mpira ukiwa mguuni kwangu kugundua kipaji Cha ajabu kilichopo ndani yangu

Tulikua na timu moja undisputed mtaan tulipeleka moto kwel kwel....

Mm ni mkimya na mpole Huwa sina maneno mengi.....

Mara nyingi ugenini uta nyimwa namba...kutokana na kutokujulikana ugenini.. uta baki nje kupiga dana dana....kosa likitokea au emergency nikapewa namba....sekunde kadhaa mpira ukiwa Mguu wa KUSHOTO watu hubakia midomo wazi na kustaajabu...

A-level niliwaacha hoi watu hawakuwai kutegemea kua ningeweza kua kipaji na uwezo nilio uonyesha Miaka miwili tuli ibuka mabingwa.....

Mpaka leo hii mm ni fundi wa kupiga mipira iliyokufa na penalty huwaga sikosei hata kipa awe OLIVER KHAN

Mpira wa miguu ungeninunulia magari na nyumba ila niliupotezea nili jua mpira kibongo bongo usingenipa maisha...

Countless watu walisimamisha magari yao na shughuli Zao kuja kunitizama na kunituza.....nilitabiliwa makubwa Sana ila mm nili udharau mpira wa miguu....nili amini Sana ELIMU ndio itanitoa kimaisha.

Wito wangu kwa Vijana kama una kipaji kifuate....
Ni sahihi, hata mimi nilikuwa naupiga mwingi sana. Miaka ya 1997 walikuwa waniita "Lunyamila" mtaani kwetu ila nikaja acha.
 
Back
Top Bottom