bakuza
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 490
- 100
Siku kama ya leo 03/04/2012 miaka 834 iliyopita sawa na tarehe 11 Jamadul Awwal mwaka 597 Hijiria ya mwaka wa kiislamu, alizaliwa Khoja Nasruddin Tusi, mwanafalsafa, mwanahisabati, mnajimu na mwanazuoni mkubwa wa Kiirani katika mji wa Tusi kaskazini mashariki mwa Iran. Katika maisha yake aliasisi kituo kikubwa cha kielimu na akademia ya kwanza ya sayansi yaani mahala pa kuangalilia mwenendo wa nyota, mwezi na jua iliyojulikana kwa jina la Maraghe huko kaskazini magharibi mwa Iran. Aalimu huyo aligundua namna mpya za kutumia saa ya jua kwa ajili ya kituo hicho. Kituo hicho kilikuwa na suhula muhimu zaidi ambazo kwa miaka 300 baada ya hapo hazikuweza kushushudiwa katika nchi za Magharibi.:nod: