Tujifunze matumizi sahihi ya 'kuonesha' na 'kuonyesha'

Chimbekeha

JF-Expert Member
Dec 1, 2018
1,193
2,163
KUONYESHA na KUONESHA ni maneno ya kiswahili fasaha, maneno haya yamekuwa yakitumiwa tofauti katika mazungumzo yetu ya kila siku...

Nini mzizi wa maneno haya? Swali hili litaweza kutupatia majibu sahihi kama ifuatavyo hapo chini;

KUONYESHA linatokana na mzizi wa neno ONYA, mzizi huo una maana ya KUTAHADHARISHA au KUKARIPIA jambo,kitu, hali au tabia fulani unaweza ukanyumbua mzizi huo ukapata hali tofauti... Mfano; ONYWA, ONYEKA, ONYESHA, ONYESHANA, ONYEWA nk..

KUONESHA linatokana na mzizi wa neno ONA, mzizi huo una maana ya kupepesa macho juu ya kitu au mtu fulani..
unaweza ukanyumbua mzizi huo wa neno na kupata hali tofauti, mfano; ONWA,ONEKANA ONEKA,ONESHA nk.

MFANO WA SENTENSI kutokana na maneno tajwa hapo juu;

- TUNU atakuonyesha popote pale mtakapokutana.
Sentensi hii inamaana ya kuwa TUNU anatarajia kutoa tahadhari kwa mtu ambaye atakutanana nae ila ukisema

- TUNU atakuonesha popote pale mtakapokutana.
Sentensi hii ina maana ya kwamba; TUNU anatarajia kumfanya mtu atakae kutana nae apepese macho yake juu ya jambo, kitu au mtu fulani.

Karibu kukosoa, kuuliza, kupongeza au kurekebisha pale ambapo unahisi panastahili.
 
Kamusi ya Kiswahili ya TUKI na Hata Oxford, zinafasili neno ‘onyesha’ kama kuonyeshwa.

Je, neno ‘onea’ maana yake nini?

Kwamba uone kwa niaba ya mtu au ni dhulma dhidi ya mtu?
 
KUONYESHA na KUONESHA ni maneno ya kiswahili fasaha, maneno haya yamekuwa yakitumiwa tofauti katika mazungumzo yetu ya kila siku...

Nini mzizi wa maneno haya? Swali hili litaweza kutupatia majibu sahihi kama ifuatavyo hapo chini;

KUONYESHA linatokana na mzizi wa neno ONYA, mzizi huo una maana ya KUTAHADHARISHA au KUKARIPIA jambo,kitu, hali au tabia fulani unaweza ukanyumbua mzizi huo ukapata hali tofauti... Mfano; ONYWA, ONYEKA, ONYESHA, ONYESHANA, ONYEWA nk..

KUONESHA linatokana na mzizi wa neno ONA, mzizi huo una maana ya kupepesa macho juu ya kitu au mtu fulani..
unaweza ukanyumbua mzizi huo wa neno na kupata hali tofauti, mfano; ONWA,ONEKANA ONEKA,ONESHA nk.

MFANO WA SENTENSI kutokana na maneno tajwa hapo juu;

- TUNU atakuonyesha popote pale mtakapokutana.
Sentensi hii inamaana ya kuwa TUNU anatarajia kutoa tahadhari kwa mtu ambaye atakutanana nae ila ukisema

- TUNU atakuonyesha popote pale mtakapokutana.
Sentensi hii ina maana ya kwamba; TUNU anatarajia kumfanya mtu atakae kutana nae apepese macho yake juu ya jambo, kitu au mtu fulani.

Karibu kukosoa, kuuliza, kupongeza au kurekebisha pale ambapo unahisi panastahili.
Mbona katika mifano yako hujatumia maneno tofauti!
Umetumia neno Onyesha katika sentensi mbili tofauti?
Ila katika mnyambuliko wako huko juu nimekupata sana
 
Mbona katika mifano yako hujatumia maneno tofauti!
Umetumia neno Onyesha katika sentensi mbili tofauti?
Ila katika mnyambuliko wako huko juu nimekupata sana
Ni kweli nilikosea kutofautisha katika utungaji wa sentensi badala yake nilitumia mzizi mmoja katika sentensi mbili.
asante kwa umakini wako ila nimerekebisha tayari.
 
Kamusi ya Kiswahili ya TUKI na Hata Oxford, zinafasili neno ‘onyesha’ kama kuonyeshwa.

Je, neno ‘onea’ maana yake nini?

Kwamba uone kwa niaba ya mtu au ni dhulma dhidi ya mtu?
Neno kuonyesha kutumika kama "kuonyeshwa" nakubaliana na wewe kabisa kuwa hapo wamenyumbua tu ila je maana yake halisi ni ipi?

Na kuhusu neno "onea" ni dhulma na sijajua mzizi wake ni upi ila kutazama badala yako inakuwa "onewa" ambayo mzizi wake ni ONA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom