The Assassin
JF-Expert Member
- Oct 30, 2018
- 4,355
- 17,320
Nimekua nikijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu kuhusu elimu ya sasa, nashindwa kuelewa elimu imebadilika tofauti na niliyosoma mimi au waalimu wetu ndio walikua hawafundishi.
Siku hizi unakutana na mtoto wa darasa la pili amebeba begi zito hadi mgongo unataka kupinda, hasa hizi zinazoitwa english medium schools. Nakumbuka enzi nasoma darasa la pili tulikua na masomo 2 tu, kusoma na kuandika. Leo mtoto wa darasa la pili ana masomo karibu 9 alafu hakuna ratiba ya kesho atasoma somo lipi hivyo inamlazimu kuchukua kwenye begi lake madaftari yote 9 na vitabu vyake maana haijulikani mwalimu gani ataingia.
Huko India serikali imepiga marufuku homework kwa watoto wadogo ili kuwalinda na athari za kupimda migongo kutokana na walimu kuwarundikia kazi.
Hizi shule za english medium zitaua watoto.
Siku hizi unakutana na mtoto wa darasa la pili amebeba begi zito hadi mgongo unataka kupinda, hasa hizi zinazoitwa english medium schools. Nakumbuka enzi nasoma darasa la pili tulikua na masomo 2 tu, kusoma na kuandika. Leo mtoto wa darasa la pili ana masomo karibu 9 alafu hakuna ratiba ya kesho atasoma somo lipi hivyo inamlazimu kuchukua kwenye begi lake madaftari yote 9 na vitabu vyake maana haijulikani mwalimu gani ataingia.
Huko India serikali imepiga marufuku homework kwa watoto wadogo ili kuwalinda na athari za kupimda migongo kutokana na walimu kuwarundikia kazi.
Hizi shule za english medium zitaua watoto.