friendfx
JF-Expert Member
- Oct 16, 2017
- 246
- 250
Walimuuliza mtu mmoja mwenye umri mkubwa: Umejifunza nini kutokana na umri wako uliopita?
Akajibu:
Nimejifunza kwamba dunia ni karadha na deni
Nimejifunza kwamba aliyedhulumiwa lazima atashinda japo baada ya muda
Nimejifunza kwamba mshale wa usiku haukosei
Nimejifunza kwamba maisha yanaweza kumalizika wakati wowote huku tukiwa tumeghafilika
Nimejifunza kwamba maneno matamu na uso wenye bashasha na ukarimu ni rasilimali za tabia
Nimejifunza kwamba tajiri kuliko matajiri wote duniani ni yule ambaye anamiliki afya na amani
Nimejifunza kwamba anayepanda kitunguu hatavuna mawaridi
Nimejifunza kwamba umri unamalizika lakini shughuli hazimaliziki
Nimejifunza kwamba anayetaka watu wamsikilize basi na yeye awasikilize
Nimejifunza kwamba kusafiri na watu ni zana bora ya kugundua tabia zao
Nimejifunza kwamba ambaye anaongea sana (anasema mimi, mimi) huyo ni mtupu ndani yake
Nimejifunza kwamba ambaye madini yake ni dhahabu atabaki dhahabu, na ambaye madini yake ni chuma atabadilika na kuchuja
Nimejifunza kwamba wote waliozikwa makaburini walikuwa na mashughuli na maagano na kwenye nia zao walikuwa na mengi ambayo hawakuyatimiza
Nimejifunza kwamba sisi tunatandika kitanda na tunabaridisha chumba ili tuneemeke na mauti madogo, lakini je tumeratibu matendo yetu na kubaridisha makaburi yetu kwa kufanya twaa ili tuneemeke na mauti makubwa?
Anasema mmoja wa watu wema; Nimestaajabishwa na watu wanajihadhari na baadhi ya vyakula kwa kuogopa maradhi, lakini hawajihadhari na dhambi kwa kuogopa moto
Nimeyasoma, yakanivutia na nikapenda niyatume kwa nafsi njema
Akajibu:
Nimejifunza kwamba dunia ni karadha na deni
Nimejifunza kwamba aliyedhulumiwa lazima atashinda japo baada ya muda
Nimejifunza kwamba mshale wa usiku haukosei
Nimejifunza kwamba maisha yanaweza kumalizika wakati wowote huku tukiwa tumeghafilika
Nimejifunza kwamba maneno matamu na uso wenye bashasha na ukarimu ni rasilimali za tabia
Nimejifunza kwamba tajiri kuliko matajiri wote duniani ni yule ambaye anamiliki afya na amani
Nimejifunza kwamba anayepanda kitunguu hatavuna mawaridi
Nimejifunza kwamba umri unamalizika lakini shughuli hazimaliziki
Nimejifunza kwamba anayetaka watu wamsikilize basi na yeye awasikilize
Nimejifunza kwamba kusafiri na watu ni zana bora ya kugundua tabia zao
Nimejifunza kwamba ambaye anaongea sana (anasema mimi, mimi) huyo ni mtupu ndani yake
Nimejifunza kwamba ambaye madini yake ni dhahabu atabaki dhahabu, na ambaye madini yake ni chuma atabadilika na kuchuja
Nimejifunza kwamba wote waliozikwa makaburini walikuwa na mashughuli na maagano na kwenye nia zao walikuwa na mengi ambayo hawakuyatimiza
Nimejifunza kwamba sisi tunatandika kitanda na tunabaridisha chumba ili tuneemeke na mauti madogo, lakini je tumeratibu matendo yetu na kubaridisha makaburi yetu kwa kufanya twaa ili tuneemeke na mauti makubwa?
Anasema mmoja wa watu wema; Nimestaajabishwa na watu wanajihadhari na baadhi ya vyakula kwa kuogopa maradhi, lakini hawajihadhari na dhambi kwa kuogopa moto
Nimeyasoma, yakanivutia na nikapenda niyatume kwa nafsi njema