Tujifunze kitu kwa misiba ya vigogo hawa na idadi ya watoto

comrade_kipepe

JF-Expert Member
Jun 25, 2019
3,303
4,237
Nipo nacheki hapa msiba wa Ndugulile, kuacha watoto wawili tu, pamoja alikuwa ana uwezo wa kipesa na cheo lakini kaishia kwenye watoto wawili, watoto wawili hawa naona kawakuza na kuwasomesha kwenye shule za gharama inawezekana nje ya nchi maana hata Kiswahili chao ni broken sana wanakuwa kama sio watanzania.

Lawrence Mafuru nae nadhani aliacha watoto wawili tu.

Swali kwa makapuku wenzangu, hivi Sisi maskini tunazaa watoto wengi ili iweje? Na utakuta pengne hata uwezo wa kuwahudumia tuu kikamilifu kwenye elimu na gharama za kila siku hatuwezi, nini maana ya hii?

Nahis NI vizuri kuzaa watoto kulingana na kipato chako, ambao utawamudu vizuri, utakaowapa elimu ya uhakika sio hii ya kuunga unga.

Sisi maskini tunawaza eti tukizaa watoto wengi ndio hao badae watatusaidia, wewe mzazi somesha mtoto, hudumia kwa kadiri ya uwezo wako maana ni jukumu lako, badae akipata maisha mazuri NI yeye sasa atajua atakusaidiaje, ndio ile utakuta wazazi wananunia wakwe zao wanaona kama wao ndio wanafanya wasipewe pesa na mtoto wao.

Tuzae Kwa mahesabu, utakuta mtu ana watoto wanne, halafu kapanga chumba na sebule, sasa jiulize hapo ndani wanaishije, tuwekeze nguvu kwenye kujenga uchumi Kwanza na kuzaa kwa akili.

 
Kosa kubwa alilofanya ni ile akili ya MTU mweusi ya kufanya Accumulation bila distribution

Yale maeneo potential yote aliyojimilikisha kigamboni Kama angeamua kutoa ghorofa lake moja akawapa wanafunzi wakaishi bure au akawa na programs maalumu za kuwalipia Ada wanafunzi hata wanafunzi 100 kila mwaka .

Tafsiri sahihi ya utajiri ya MTU mweusi huwa inafikirisha Sana .
 
Nipo nacheki hapa msiba WA Ndugulile, kuacha watoto wawili tuu, pamoja alikua na uwezo WA kipesa na cheo lakini kaishia kwenye watoto wawili, watoto wawili hawa naona kawakuza na kuwasomesha...
Tukianza kujilinganisha na Ndugulile na Mafuru utaona watu wengi hawàna sifa ya kuwa háta na nusu mtoto!
Siyo kweli kwamba hao wawili wanawakilisha wenye hela wote kuwa nà watoto wawili wawili.

Hao ni uzembe wao tuu mbona husemi waziri Jafo mwenye wake wanne na watoto lukuki?

Nchengerwa, Awesu, Hafidh nk wana hela na wana wake zaidi ya mmoja?

Unadhani hawa hawamjui Ndugulile, au Mafuru?
 
Tahadhari kwa wazazi uzungu ukizidi sana ndio haya matokeo, ujasiri unaotoa wapi mtoto mdogo unamzika Baba yako uneongelea mziki wa Prof J, sisemi alie agalegale hapana ila sisi wa Africa wazazi tukipoteza ni pigo haijalishi wewe ni nani ila wenzetu naona mpaka tabia wanaiga za huko tuliona hata kwenye msiba wa Mafuru sijui labda ndio watoto wa kileo lakini mimi nilimzika mzazi wangu kwa uchungu hata kama sikulia hadharani lakini sura yangu sikuweza kuficha dhoruba.
 
Tukianza kujilinganisha na Ndugulile na Mafuru utaona watu wengi hawàna sifa ya kuwa háta na nusu mtoto!
Siyo kweli kwamba hao wawili wanawakilisha wenye hela wote kuwa nà watoto wawili wawili...
Kwahyo unawashauri maskini ambao hata Kula Yao NI ya shida waoe wake wanne na wazae kama jafo?? Au hujaelewa hata nimeandika nini, nmesema tuzae kulingana na uwezo wetu, kwahyo jafo nae wake alio nao na watoto NI kulingana na kipato chake
 
Back
Top Bottom