Tujifunze faida za kujenga Chato international Airport

Kamukhm

JF-Expert Member
Aug 30, 2015
2,799
4,192
Uwanja wa Ndege ... Unatofauti sana na Vituo vya usafiri Wa namna nyingine. Tujiulize kuna faida gani ya kimapato kumiliki uwanja wa ndege na inatoka wapi faida hii!

Uwanja wa ndege hasa unapokuwa wa kimataifa unategemea a complex web of factors ilikuufanya kuwa viable.. Katika factors hizi ni pamoja na Planning Air Routes, mwelekeo wa uchumi wa kikanda na Dunia, uelekeo wa watu nk...

Vitu hivi vinazingatiwa na wataalam ili kutetea maombi yao katika ujenzi Mpya wa uwanja ndege basi uwanja unakuwa na kushamiri.

Nairobi ilikuwa kwa kipindi kirefu a gateway to east Africa... Watu waliamini na mpaka leo wanaendelea kuamini ili kufika Tanzania au Uganda na Burundi/Rwanda basi pata tikiti yako ya nairobi kuanzia hapo unachukua regional Transport...

Hii ni kutokana na effective Route planning...by which wakenya walionesha nia yao ya kukidhi haja za wana afrika mashariki kufika katika maeneo wanayofika sasa...

Kwa sasa tunapanua JNIA pamoja na kuongeza miundombinu ili kuweza kuattract watu kuleta ndege zao.. Tumekawia ila tunaweza kama tutaanza na ndege yetu kubwa pindi ikifika...Insh'Allah! Wenzetu na wawekezeaji wengine duniani wataona walichelewa kiasi gani na hii itaongeza flow pale JNIA.

Katika Miradi ya upanuzi ..zabuni zilizotolewa na TAA nimeona upanuzi Songwe, Mwanza. Ukarabati na Upanuzi, Sumbawanga na Kigoma nadhani na Tabora... Hii designing Kama sikosei Arusha....

Hii yote inaenda hand in hand na Mpango tuliokuwa nao kabla; wa kuifungua nchi kwa uwekezaji Wa nje. Maeneo yote yenye fursa tulitaka yaunganishwe kwa ndege maana honestly ndio usafiri unaotumiwa na matajiri/wawekezaji... Otherwise itakuwa ngumu kuwapotezea muda na masafari mareefu ya gari.na muda wao ni Mali

Nirudi kwenye mapato ya uwanja wa ndege.. Air routes haziingizii pesa Uwanja..ila zinapelekea kuongeza mapato kama ..zitapelekea ongezeko katika mambo kama

1-ongezeko la Ndege zinazotua na kuruka.. Hii inamaana tozo la ndege kuruka na kutua litaongezeka ..na kama ndege zinazotua ni kubwa.. Tutapa parking kubwa zaidi, na tozo itakuwa kubwa kwani hutolewa kwa kuzingatia ukubwa na uzito. Na pia kuna gharama za wasafirishaji kutumia uwanja kama air control fees na parking assistance fees.

2-ongezeko la watu wanaotumia uwanja huo.. Hapa ndio mapato makubwa kabisa huwa yanapatikana kwa airport.. Busy airports na zinazovutia watu wengi pia zinamapato makubwa ..

Maana watu wote hulipa airport charges kupitia manunuzi ya Tikiti. Kwa mfano kwa Tanzania JNIA, KIA, Zanzibar na Mwanza ndio zenye mapato zaidi kwa kuwa zinatumiwa na watu wengi zaidi.

Lakini pia ongezeko LA watu linasaidia uwanja Wa ndege kupata mapato mengine kutoka kwenye vyanzo kama Concession fees zinazopatikana kwa wauzaji wa mikahawa na maduka ndani ya uwanja.

Viwanja vingi vikuwa havipangishi hizi nafasi ila unaendesha biashara kwa makubaliano maalum kwamba sehemu ya faida yako itakuwa ni mapato kwa Uwanja na hivyo kufanya wote kushiriki hasara na faida..

Maana mundeshaji anapaswa kuwa na huduma bora ili watu warudi au wapange kuitumia airport hiyo next time, na mwenye Uwanja awe na huduma nzuri kwa wasafiri na wasafirshaji ili waendelee kurudi hapo.. Mmoja akikosea wote mmekosa..

3- uelekeo wa watu ni kitu muhimu.. Kunakipindi nilikuwa Kahama na nikawa nataka kuwahi dsm kwa ndege ila ilibidi nije mwanza kwanza.. Kwa hiyo nilipata ndege ya jioni..

Niliondoka Kahama SAA NNE ..toochi wee nikafika mwanza SAA kumi na moja jioni.. Na nikafika dar usiku. Jamaa yangu aliyeondoka asubuhi Kahama na basi akaingia SAA 4 usiku pia.. I felt like a loser. hii ndio uelekeo..

Watu hawawezi kwenda kigoma ili wapande ndege ya kwenda Dar. Au wa Nzega Aende Tabora ili kuja Dar.. Wakati anayo cheap option.

Hivyo uelekeo ni kitu muhimu sana. Hii kwa takwimu za haraka Kahama ilikuwa ikigenerate asilimia 30 mpk 50 ya wateja wanaotumia uwanja Wa mwanza.. Wengi wakiwa wafanyabiashara wanaotoka Congo, Burundi na Rwanda

Kwa kifupi unahitaji kugenerate enough trips ili uwanja wa ndege uwe viable.. And often majiji na miji yenye watu wengi inao uwezo wa kuzalisha safari nyingi kutokana na economic complexity na mahitaji yao ya kila siku. Na pia miji yenye watu wengi ina uzalishaji mkubwa hence kuwa na bidhaa na huduma nyingi zinazohitaji kusafirishwa.

Gharama za Matunzo na Uendeshaji..
Kama ilivyo kwa mwili mkubwa maji mengi yatatumika kuuosha ndivyo hivyo kwa Uwanja mkubwa..

1-Gharama za utunzaji Wa miundombinu ya uwanja. Kwani taa za njia ya kuruka, Standby Source of electricity, Usafi wa Jengo LA abiria .. Katika huduma una watu Wa control tower, Usafi, wanasheria, Mafundi na wanamahesabu ya fedha.

Hivi vyote vinahitaji full time employees na pia kwa huduma za nje kunakuwa na contractors wenye mikataba ya muda mrefu.

2- Routine check na major rehabilitation whenever needed.. Itabidi kuwe na funds allocated for that.

Mwisho, Uwanja ukijengwa ni seed money..kuna hatua za kufanya ili kuufanya uwe viable.. Sasa kwa nadharia tu..inabidi tupange tuwe tunajua au hata tufanye testing.. Kisha ndio tufikirie kujenga..

Mfano mzuri narudi Kahama walifanya study.. Ikawa.positive..sasa Precision Air wanafanya safari ..(Phase ya Majaribio) still uwanja in wa Mchanga (Improved ofcoz) na kajengo kadogo ka Wasafiri. Baadae kama Kahama Airport itaprove kuwa an economically sound project naamini watajenga sasa a proper airport...

Chato Airport ...tafadhalini naombeni msaada kama kuna vitu naviruka...ila kwa upole mnieleweshe..

1- Uchumi wake ni Mdogo sana kama kata mbili tu pale Geita/Kahama au Mitaa miwili tu hapo Chanika

2. Predominantly inategemea uchumi Wa subsistence farming ..hakuna uwezo Wa kuzalisha au kuwa na kipato cha kutumia ndege ukitoa maybe a 5% of population ambayo ni affluent na sehemu kubwa ya wafanyakazi Wa serikali. Ambao pia safari zao sio nyingi..

3- Watalii kuelekea Rubondo.. Nadhani tunapokea watalii wachache tu Rubondo. Na Makampuni mengi wamesha establish Mwanza as the base na inayo airport na water way ambayo sidhani kama itakuwa muda mrefu saaana kufika Rubondo toka mwanza.

4. Soko la dhahabu... Hii jamani tuliona huko nyuma... Gesi.inachimbwa mtwara uchakataji.unafanyika dar.. Ng'ombe wanafugwa Shinyanga kiwanda cha ngozi Morogoro... Kwa Nn?! Solo.la dhahabu lisiwekwe kwenye Dhahabu?! Kama soko la Tanzanite lilivyo kwenye Tanzanite?!

Hii.itapelekea hata wachimbaji wa kati.na wadogo wafikiwe na wanunuzi.wakubwa na kupunguza ulanguzi..

Kama ni ghari na hatari.kusafirisha Dhahabu kwa njia ya Barabara Km 300 itakuwaje kwa migodi ya Kigoma, Tabora Nzega, Kahama na Singida?! Tutawapelekea Viwanja?!

Na kama Migodi Yote INA viwanja vidogo kulikuwa na umuhimu gani kuwa na uwanja mkubwa chato kama lengo ni kuleta dhahabu tu kuuza?!

5-Wanachato wanahitaji maendeleo.. Ila lazima yawe na uhalisia... Kiatu kina life span ya miaka 5kwa material iliyotumika... Regardless umekivaa au umetunza kabatini...

Strength yake kama kiatu itakuwa obsolete in 5years.. Halafu mkeo ana mimba tu unaamua kumnunulia mtt hiki kiatu akizaliwa akakua, akafikia muda Wa kwenda dara la kwanza akiwa na miaka 6 atakivaa ... Jamani... Huu uwanja mpaka chato iuhitaji utakuwa ni wakujengwa upya...

Kwanini tutupe hii fedha Leo katika ujenzi na baada ya hapo kwa kodi zetu tuukarabati na kuutunza kwa.muda wote ambao utakuwa haufanyi faida?!
 
Nissan nyeupe inakuhusu
Kaka na sisi wa huku kweye njeleli wanaleta nisani?! Hapana bwana.. Hawako hivyo..plus nina vimaswali vyangu ndio nipata ufumbuzi... Kujigunza tu.. Uwanja wenyewe ujengwe tu... Hata sipingi kabisa
 
Jibril beder... Matisho hayo.. Au na hujulikani pia
 
Tutapeleka hata midege mikubwa ya kubeba mizigo. Nimeona mang'ombe ya ankole kule Biharamulo yaliyotoka ng'ambo yakipigwa chapa za kwetu. Tuta force nyama ya darisalama itoke huko. Huoni wewe kwa sasa ila tutakapoongeza na muda wa kukaa ofisi ile zaidi, lazima tutaleteleza matumizi ya huo uwanja tu. Si bora amri??
 
Tutapeleka hata midege mikubwa ya kubeba mizigo. Nimeona mang'ombe ya ankole kule Biharamulo yaliyotoka ng'ambo yakipigwa chapa za kwetu. Tuta force nyama ya darisalama itoke huko. Huoni wewe kwa sasa ila tutakapoongeza na muda wa kukaa ofisi ile zaidi, lazima tutaleteleza matumizi ya huo uwanja tu. Si bora amri??
Hujasema kile nimeelewa ... Mbn unanitisha ... Kwani ukomo si upo?lkn
 
Uwanja wa Ndege ... Unatofauti sana na Vituo vya usafiri Wa namna nyingine. Tujiulize kuna faida gani ya kimapato kumiliki uwanja wa ndege na inatoka wapi faida hii!

Uwanja wa ndege hasa unapokuwa wa kimataifa unategemea a complex web of factors ilikuufanya kuwa viable.. Katika factors hizi ni pamoja na Planning Air Routes, mwelekeo wa uchumi wa kikanda na Dunia, uelekeo wa watu nk...

Vitu hivi vinazingatiwa na wataalam ili kutetea maombi yao katika ujenzi Mpya wa uwanja ndege basi uwanja unakuwa na kushamiri.

Nairobi ilikuwa kwa kipindi kirefu a gateway to east Africa... Watu waliamini na mpaka leo wanaendelea kuamini ili kufika Tanzania au Uganda na Burundi/Rwanda basi pata tikiti yako ya nairobi kuanzia hapo unachukua regional Transport...

Hii ni kutokana na effective Route planning...by which wakenya walionesha nia yao ya kukidhi haja za wana afrika mashariki kufika katika maeneo wanayofika sasa...

Kwa sasa tunapanua JNIA pamoja na kuongeza miundombinu ili kuweza kuattract watu kuleta ndege zao.. Tumekawia ila tunaweza kama tutaanza na ndege yetu kubwa pindi ikifika...Insh'Allah! Wenzetu na wawekezeaji wengine duniani wataona walichelewa kiasi gani na hii itaongeza flow pale JNIA.

Katika Miradi ya upanuzi ..zabuni zilizotolewa na TAA nimeona upanuzi Songwe, Mwanza. Ukarabati na Upanuzi, Sumbawanga na Kigoma nadhani na Tabora... Hii designing Kama sikosei Arusha....

Hii yote inaenda hand in hand na Mpango tuliokuwa nao kabla; wa kuifungua nchi kwa uwekezaji Wa nje. Maeneo yote yenye fursa tulitaka yaunganishwe kwa ndege maana honestly ndio usafiri unaotumiwa na matajiri/wawekezaji... Otherwise itakuwa ngumu kuwapotezea muda na masafari mareefu ya gari.na muda wao ni Mali

Nirudi kwenye mapato ya uwanja wa ndege.. Air routes haziingizii pesa Uwanja..ila zinapelekea kuongeza mapato kama ..zitapelekea ongezeko katika mambo kama

1-ongezeko la Ndege zinazotua na kuruka.. Hii inamaana tozo la ndege kuruka na kutua litaongezeka ..na kama ndege zinazotua ni kubwa.. Tutapa parking kubwa zaidi, na tozo itakuwa kubwa kwani hutolewa kwa kuzingatia ukubwa na uzito. Na pia kuna gharama za wasafirishaji kutumia uwanja kama air control fees na parking assistance fees.

2-ongezeko la watu wanaotumia uwanja huo.. Hapa ndio mapato makubwa kabisa huwa yanapatikana kwa airport.. Busy airports na zinazovutia watu wengi pia zinamapato makubwa ..

Maana watu wote hulipa airport charges kupitia manunuzi ya Tikiti. Kwa mfano kwa Tanzania JNIA, KIA, Zanzibar na Mwanza ndio zenye mapato zaidi kwa kuwa zinatumiwa na watu wengi zaidi.

Lakini pia ongezeko LA watu linasaidia uwanja Wa ndege kupata mapato mengine kutoka kwenye vyanzo kama Concession fees zinazopatikana kwa wauzaji wa mikahawa na maduka ndani ya uwanja.

Viwanja vingi vikuwa havipangishi hizi nafasi ila unaendesha biashara kwa makubaliano maalum kwamba sehemu ya faida yako itakuwa ni mapato kwa Uwanja na hivyo kufanya wote kushiriki hasara na faida..

Maana mundeshaji anapaswa kuwa na huduma bora ili watu warudi au wapange kuitumia airport hiyo next time, na mwenye Uwanja awe na huduma nzuri kwa wasafiri na wasafirshaji ili waendelee kurudi hapo.. Mmoja akikosea wote mmekosa..

3- uelekeo wa watu ni kitu muhimu.. Kunakipindi nilikuwa Kahama na nikawa nataka kuwahi dsm kwa ndege ila ilibidi nije mwanza kwanza.. Kwa hiyo nilipata ndege ya jioni..

Niliondoka Kahama SAA NNE ..toochi wee nikafika mwanza SAA kumi na moja jioni.. Na nikafika dar usiku. Jamaa yangu aliyeondoka asubuhi Kahama na basi akaingia SAA 4 usiku pia.. I felt like a loser. hii ndio uelekeo..

Watu hawawezi kwenda kigoma ili wapande ndege ya kwenda Dar. Au wa Nzega Aende Tabora ili kuja Dar.. Wakati anayo cheap option.

Hivyo uelekeo ni kitu muhimu sana. Hii kwa takwimu za haraka Kahama ilikuwa ikigenerate asilimia 30 mpk 50 ya wateja wanaotumia uwanja Wa mwanza.. Wengi wakiwa wafanyabiashara wanaotoka Congo, Burundi na Rwanda

Kwa kifupi unahitaji kugenerate enough trips ili uwanja wa ndege uwe viable.. And often majiji na miji yenye watu wengi inao uwezo wa kuzalisha safari nyingi kutokana na economic complexity na mahitaji yao ya kila siku. Na pia miji yenye watu wengi ina uzalishaji mkubwa hence kuwa na bidhaa na huduma nyingi zinazohitaji kusafirishwa.

Gharama za Matunzo na Uendeshaji..
Kama ilivyo kwa mwili mkubwa maji mengi yatatumika kuuosha ndivyo hivyo kwa Uwanja mkubwa..

1-Gharama za utunzaji Wa miundombinu ya uwanja. Kwani taa za njia ya kuruka, Standby Source of electricity, Usafi wa Jengo LA abiria .. Katika huduma una watu Wa control tower, Usafi, wanasheria, Mafundi na wanamahesabu ya fedha.

Hivi vyote vinahitaji full time employees na pia kwa huduma za nje kunakuwa na contractors wenye mikataba ya muda mrefu.

2- Routine check na major rehabilitation whenever needed.. Itabidi kuwe na funds allocated for that.

Mwisho, Uwanja ukijengwa ni seed money..kuna hatua za kufanya ili kuufanya uwe viable.. Sasa kwa nadharia tu..inabidi tupange tuwe tunajua au hata tufanye testing.. Kisha ndio tufikirie kujenga..

Mfano mzuri narudi Kahama walifanya study.. Ikawa.positive..sasa Precision Air wanafanya safari ..(Phase ya Majaribio) still uwanja in wa Mchanga (Improved ofcoz) na kajengo kadogo ka Wasafiri. Baadae kama Kahama Airport itaprove kuwa an economically sound project naamini watajenga sasa a proper airport...

Chato Airport ...tafadhalini naombeni msaada kama kuna vitu naviruka...ila kwa upole mnieleweshe..

1- Uchumi wake ni Mdogo sana kama kata mbili tu pale Geita/Kahama au Mitaa miwili tu hapo Chanika

2. Predominantly inategemea uchumi Wa subsistence farming ..hakuna uwezo Wa kuzalisha au kuwa na kipato cha kutumia ndege ukitoa maybe a 5% of population ambayo ni affluent na sehemu kubwa ya wafanyakazi Wa serikali. Ambao pia safari zao sio nyingi..

3- Watalii kuelekea Rubondo.. Nadhani tunapokea watalii wachache tu Rubondo. Na Makampuni mengi wamesha establish Mwanza as the base na inayo airport na water way ambayo sidhani kama itakuwa muda mrefu saaana kufika Rubondo toka mwanza.

4. Soko la dhahabu... Hii jamani tuliona huko nyuma... Gesi.inachimbwa mtwara uchakataji.unafanyika dar.. Ng'ombe wanafugwa Shinyanga kiwanda cha ngozi Morogoro... Kwa Nn?! Solo.la dhahabu lisiwekwe kwenye Dhahabu?! Kama soko la Tanzanite lilivyo kwenye Tanzanite?!

Hii.itapelekea hata wachimbaji wa kati.na wadogo wafikiwe na wanunuzi.wakubwa na kupunguza ulanguzi..

Kama ni ghari na hatari.kusafirisha Dhahabu kwa njia ya Barabara Km 300 itakuwaje kwa migodi ya Kigoma, Tabora Nzega, Kahama na Singida?! Tutawapelekea Viwanja?!

Na kama Migodi Yote INA viwanja vidogo kulikuwa na umuhimu gani kuwa na uwanja mkubwa chato kama lengo ni kuleta dhahabu tu kuuza?!

5-Wanachato wanahitaji maendeleo.. Ila lazima yawe na uhalisia... Kiatu kina life span ya miaka 5kwa material iliyotumika... Regardless umekivaa au umetunza kabatini...

Strength yake kama kiatu itakuwa obsolete in 5years.. Halafu mkeo ana mimba tu unaamua kumnunulia mtt hiki kiatu akizaliwa akakua, akafikia muda Wa kwenda dara la kwanza akiwa na miaka 6 atakivaa ... Jamani... Huu uwanja mpaka chato iuhitaji utakuwa ni wakujengwa upya...

Kwanini tutupe hii fedha Leo katika ujenzi na baada ya hapo kwa kodi zetu tuukarabati na kuutunza kwa.muda wote ambao utakuwa haufanyi faida?!
Pigeni kelele na kuchanganya kizungu kwa sanaa lakini mwisho wake mtatulia tu, na uwanja wa Chato utajengwa hadi umalizike. Poleni sana wajameni.
 
Mbona hujiulizi Kilimanjaro kuna viwanja viwili kwani chato kwa maana ya geita hawahitaji kiwanja ndege?
 
Pigeni kelele na kuchanganya kizungu kwa sanaa lakini mwisho wake mtatulia tu, na uwanja wa Chato utajengwa hadi umalizike. Poleni sana wajameni.
Habari yako kiongozi...za uchuvu?! Umeshinda salama?! Vipi umeshoma kile nimeandika au umeanza kusoma ukachoka ila ikabidi uchangie tu?!

Kama utasoma nadhani liko swala...na hilo ndio nataka nisaidiwe... Na Kwa upole tena.. Uwanja ujengwe... Ila na mie majibu yangu nipate.. Win win au sio..?!
 
Habari yako kiongozi...za uchuvu?! Umeshinda salama?! Vipi umeshoma kile nimeandika au umeanza kusoma ukachoka ila ikabidi uchangie tu?!

Kama utasoma nadhani liko swala...na hilo ndio nataka nisaidiwe... Na Kwa upole tena.. Uwanja ujengwe... Ila na mie majibu yangu nipate.. Win win au sio..?!
Aisee, nyinyi kwa nini mmekalia kujadili uwanja ambao karibu tayari unamalizika? Maji yameshamwagika lakini bado tu mnapoteza muda kutaka kuyazoa. Mtaweza kweli?
 
Mbona hujiulizi Kilimanjaro kuna viwanja viwili kwani chato kwa maana ya geita hawahitaji kiwanja ndege?
Chato wanataka uwanja wa ndege? Labda airstrip..uwanja Wa ndege sio Leo... Kilimanjaro ni mkoa ... Kuwa navyo hata sita kila wilaya pia ni saw a... Ila last time I checked kipo kimoja Kilimanjaro International Airport... Labda kama unasemea na kile cha arusha ambacho sio international... Njia za kurukia kama Kahama tu zipo 3 ila hakuna Airport... Njia za kurukia zinawekwa mpaka maporini katikati ya misitu...

Na ukinisoma vizuri utagundua sitaki kuvutana ujenzi nataka kuelewa nadharia ya kiuchumi/kuendelezaji miji iliyotumika
 
Uwanja wa chato ni mkoa wa geita kwa hiyo uwe na adabu sio kusema hawahitaji leo kwa zako za kinafiki
 
Aisee, nyinyi kwa nini mmekalia kujadili uwanja ambao karibu tayari unamalizika? Maji yameshamwagika lakini bado tu mnapoteza muda kutaka kuyazoa. Mtaweza kweli?
Kaka lazima tukubaliane... Kuwa kuna umuhimu wa kuitengeneza historia yetu... Tunayoonywa leo ndio makosa yaliypfanywa Jana...na tunaambiwa tufanye kwa bidii Leo..yalianzwa kufanywa Jana na yakawa na matunda...

Najua we we ni msomi..kuna ka dissertation umewahi andika... Tunafanya research ya vitu vilivyokwisha fanywa kwa lengo la kuelewa utendaji kazi wake..na kama Luna tweaking tunaweza fanya kuboresha outcome..au kuna mambo tunaweza avoid kwa ajili ya better outcome... Haya ndio malengo why am still questioning... Kama hilo ni kosa pia basi shule hainisaidii...
 
Mbona hujiulizi Kilimanjaro kuna viwanja viwili kwani chato kwa maana ya geita hawahitaji kiwanja ndege?
Alafu siku atakayokuja kusema chama mama kimepoteza dira ndo mtaanza kumwita majina yote...ooh mara mtu mwenyewe mbinafsi kajenga uwanja kwao..ooh sijui fisadi aliuza nyumbani bei chee....waafrika bwana....!!!!
 
Kaka lazima tukubaliane... Kuwa kuna umuhimu wa kuitengeneza historia yetu... Tunayoonywa leo ndio makosa yaliypfanywa Jana...na tunaambiwa tufanye kwa bidii Leo..yalianzwa kufanywa Jana na yakawa na matunda...

Najua we we ni msomi..kuna ka dissertation umewahi andika... Tunafanya research ya vitu vilivyokwisha fanywa kwa lengo la kuelewa utendaji kazi wake..na kama Luna tweaking tunaweza fanya kuboresha outcome..au kuna mambo tunaweza avoid kwa ajili ya better outcome... Haya ndio malengo why am still questioning... Kama hilo ni kosa pia basi shule hainisaidii...
Unafanya makosa makubwa sana kiuandishi kuchanganya lugha. Ni vyema ukajifunza kujieleza kwa ufasaha kwa lugha moja, iwe ni kwa Kiswahili au Kiingereza. Huu ni ushauri tu, unaweza kuukataa pia. Ujanani nilidhani huo ndio usomi wenyewe lakini kumbe nilikuwa ninajidanganya. Swala la ujenzi wa uwanja wa ndege wa Chato sioni matatizo yeyote yale, kwani nchi bado inaendelea ya huwezi kukadiria umuhimu wa upanuzi wa miundombinu kwa sasa. Piga picha mambo yatakavyokuwa miaka thelathini ijayo na kuendelea. Haya makelele ya wanasiasa yamejikita zaidi katika chuki za kikanda tu, na wengi wao wanafikiria kwa kipindi kifupi. Huu ni uchizi mtupu.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom