Tujadili: Mtu kujitambulisha kama Mzanzibari ni halali, lakini kujitambulisha kama Mtanganyika ni haramu!!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,663
18,037
Hii ni kero namba moja ya muungano ya muda wote!! Kwa bahati mbaya haijaorozeshwa wala hakuna mpango wa kuiorodhesha miongoni mwa kero za muungano.

Juzi juzi tumefanya sherehe ya kumbukizi la miaka 60 ya uhuru wa "Tanzania", au wakiona aibu wanasema kumbukizi la uhuru wa "Tanzania bara"!! Lakini ukiwauliza Tanzania au Tanzania bara ilikuwa inatawaliwa na mkoloni gani?
hawana jibu!!!! watakuambia huo ni uchochezi.

Tumeamua kuificha historia yetu kwa kuifunika kwa kioo!!! Tumeifunika lakini inaonekana wazi.

Binafsi naukubali muungano, lakini hii kero ishughulikiwe.

Najivunia Utanganyika wangu kama wanavyojivunia Uzanzibari wao kabla ya wote kujivunia Utanzania wetu!!
 
Tatizo letu tunaachia wanasiasia watujengee mitazamo yetu, na wanasiasa wenyewe ambao pia wao wenyewe hawajitambui wanapelekeshwa na ari na viburi vya ushindani, muungano wa nchi na nchi ni muungano wa kisiasa kwa hio haupaswi hata kidogo kuua asili za watu na majivuno ya asili zao.

Kwa nini muungano huu unakimbilia sana kuua asili za watu na majivuno ya asili zao?
kama binadamu inabidi tukae tujitathmini kwa makini sana,Na tujujengee uwezo wa kujiamulia mambo yanayoingia akilini na sio kupelekeshwa na siasa tulizorithishwa na wakoloni.
 
Mpaka kiongozi mkuu wa Tanzania haoni haya kujitambulisha kama Mzanzibari, lakini ilipotokea kiongozi mkuu wa Tanzania alikuwa anatokea upande huu wa muungano, hutakaa umsikie anajitambulisha kama Mtanganyika!! Hii ni aibu kubwa ya muda wote!! Waswahili husema mkataa kwao ni mtumwa!!
 
Christopher Mtikila ndio mpinzani pekee aliyewahi kutokea nchini Tanganyika.
Tanganyika na Zanzibar ziliungana kupatikana Tanzania.

Sisi ni Watanganyika halisi.
RIP Mtikila.
 
Hii ni kero namba moja ya muungano ya muda wote!! Kwa bahati mbaya haijaorozeshwa wala hakuna mpango wa kuiorodhesha miongoni mwa kero za muungano.

Juzi juzi tumefanya sherehe ya kumbukizi la miaka 60 ya uhuru wa "Tanzania", au wakiona aibu wanasema kumbukizi la uhuru wa "Tanzania bara"!! Lakini ukiwauliza Tanzania au Tanzania bara ilikuwa inatawaliwa na mkoloni gani?
hawana jibu!!!! watakuambia huo ni uchochezi.

Tumeamua kuificha historia yetu kwa kuifunika kwa kioo!!! Tumeifunika lakini inaonekana wazi.

Binafsi naukubali muungano, lakini hii kero ishughulikiwe.

Najivunia Utanganyika wangu kama wanavyojivunia Uzanzibari wao kabla ya wote kujivunia Utanzania wetu!!
Wazanzibari wanajivunia uzanzibari wao kwa sababu wana harufu ya kiarabu( yaani baadhi yao ni warabu wa kuchovya sio original) Wewe jaribu kuangalia tu mtaani kwako kama kuna mwarabu then angalia watu anao interact nao( wenye access kwenda kwake mpaka ndani) huwa wanajiona nao ni waarabu kwa rafudhi ya kuongea hadi mavazi both women and men. HIZO NDO ATHARI ZA UKOLONI NDUGU YANGU
 
Hii ni kero namba moja ya muungano ya muda wote!! Kwa bahati mbaya haijaorozeshwa wala hakuna mpango wa kuiorodhesha miongoni mwa kero za muungano.

Juzi juzi tumefanya sherehe ya kumbukizi la miaka 60 ya uhuru wa "Tanzania", au wakiona aibu wanasema kumbukizi la uhuru wa "Tanzania bara"!! Lakini ukiwauliza Tanzania au Tanzania bara ilikuwa inatawaliwa na mkoloni gani?
hawana jibu!!!! watakuambia huo ni uchochezi.

Tumeamua kuificha historia yetu kwa kuifunika kwa kioo!!! Tumeifunika lakini inaonekana wazi.

Binafsi naukubali muungano, lakini hii kero ishughulikiwe.

Najivunia Utanganyika wangu kama wanavyojivunia Uzanzibari wao kabla ya wote kujivunia Utanzania wetu!!
Ziliunganjshwa nchi mbili Tanganyika na Zanzibar, ikapatikana nchi moja inaitwa TANZANIA
Halafu kukawa na Tanzania bara na Tanzania visiwani.....
Halafu kukawa na Tanzania na Zanzibar
Pole sana Tanganyika
 
Back
Top Bottom