Tujadili Mgomo wa Waalimu

Mzee wa Gumzo

Senior Member
Apr 21, 2008
197
5
Jamani naona umuhimu mkubwa sana wa kuadili pamoja ishu ya mgomo wa waalimu unaoandaliwa.

Chama cha walimu Tanzania (CWT) kimeshaanza maandalizi ya mgomo kwa kusambaza fomu kwa walimu kusudi walimu wajaze kama ishara ya kuunga mkono mgomo huo.

Wakati mkakati huo ukiwa mbioni kutekelezwa imeibuka hoja ya ni lini mgomo huo uanze.Wapo wanaopendekeza kuwa mgomo huo uanze ama siku ya mitihani ya darasa la saba au siku ya kuanza mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka huu.

Hata hivyo kuna walimu huko Shinyanga wameanza kugwaya hasa wale waajiriwa wapya kwa madai kuwa bado hawaja onja utamu wa kazi.

Napenda kuweka hoja nzito zifuatazo:

Serikali inalichukuliaje suala la malimbikizo ya madeni ya waalimu?
Serilkali itaendelea kuwahadaa walimu na wafanyakazi wengine mpaka lini?
Hivi ni kweli kuwa serikali inatafuta fedha wakati kuna wengine wanazichota hukohuko serikalini na kujineemesha?
Serikali imeshajiuliza nini zitakuwa athari za mgomo wa walimu kitaifa?
Ni nini hatima ya elimu yetu na watoto wa Tanzania katika Jumuiya yaAfriaka Mashariki,SADEC,AU na dunia kijiji kwa ujumla?
Kama walimu watagoma je sisi wenye watoto mashuleni natuliopitia mikononi mwa haohao walimu tufanyeje?Tukae kimya? Tuandamane?

Mimi ni mdau wa ELIMU tena hasa.Najua madhila wayapatayo waalimu.Sijahadithiwa na mtu.Mimi ni Mtanzania, Nafahamu ahadi hewa ambazo serikali yetu imekuwa ikizitoa.Mimi nami ni MUATHIRIKA wa serikali iliyopo na zilizopita kwa kiasi.

Tusipoitazama ELIMU kwa umakini tunapoteza mwelekeo wa Taifa.Wanasiasa wetu wameingiza siasa kwenye masuala nyeti na mtambuka.Imekuwa rahisi sana kusimama Bungeni na kusema 'Serikali imeliona hilo na inalifanyia kazi pindi fedha zitakapopatikana'.Hata Rais katika hotuba ya mwisho wa mwezi alituambia kuwa'Uvumilivu ni sehemu ya kutatua tatizo'.Alimaanisha kuwa kama umekalia makaa ya moto uvumilie tu wakati utaratibu wa kuondoa huo mkaa unafanywa.Alikuwa anatuma salamu kwa walimu na vikongwe wastaafu wa iliyokuwa jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa hata wakiandamana na kulia siyo rahisi mambo yao yakatatuliwa mapema, wajifunze kuvumilia shida.

Hivi huko serikalini wanajua shida kweli?.Sijawahi kusikia wafanyakazi wa ofisi ya Bunge, wabunge,wafanyakazi wa Ikulu au Mahakama wanalalamika kucheleweshewa malimbikizo yao.Huko kwa wakubwa mshahara unaongezwa na wanalipwa kwa wakati bila kulimbiiza.Waalimu wanadai malimbikizo ya miezi 6 mpaka miaka miwili.Nchi moja, Raisi mmoja, chama dola kimoja.

Sitaki kuamini kuwa watanzania tumekubali kuwa wadanganyika kwa kiasi hiki lakini nataka kuamini kuwa tunaelekea kufumbuka macho na kuuona ukweli wa uongo wa wanasiasa wetu na watendaji tuliowapa dhamana.
Sipendi niendelee kuamini kuwa tumelishwa unga wa NDERE kama Mtolewa kwenye tamthiliya ya KIVULI KINAISHI.Kama kweli tumelishwa unga wa ndere tutaendelea kuamini kuwa uvumilivu wetu wa milele ni sehemu ya kutatua matatizo.

Mwaka 2010 tutaletewa Ilani ya uchaguzi mpya na somo la uvumilivu litaendelea...

Karibuni wadau.
 
walimu kusema ukweli ni watu muhimu katika jamii lakini pia ni watu wasio na maamuzi,ninasema ili kwa sababu haya malimbikizi kama wanavyoyaita sio ya jana wala leo;hawa walimu(wa serikali)walipanga kugoma mwezi wa tano lakini kilichotokea tulikiona wakakaa kimya wakakaliwa wakaendelea kula chaki zao,hv walimu mnajionaje,je nyie ni muhimu kuzidi madaktari mbona wanaamua kimoja wanagoma kama ni kufa watu wanakufa na maisha yanaendelea na inabidi walimu muelewe kuwa labour violence ni njia moja ya kutatua matatatizo yenu.
shida nyie walimu sijui mnaongozwa na nani ambaye anawafanyia maamuzi yasiyofaa nyie ni wasomi(isipokuwa wle wliopata walimu kwa kupendelewa) na sifa ya msomi lazima awe na maamuzi hata kama yatamdhuru mtu mwingine kama hao vijana watakao kuwa wanamaliza kidato cha nne na darasa la saba hamna jinsi mbona kongo, uganda walimu wamegoma miezi kadhaa,nyie watanzania ndo maana mnadumaza elimu kwa kuwa hamna maamuzi.
alafu nyie walimu mnaongozwa na viongozi wasiofaa ndo maana hamfanikiwa kama viongozi wenu sio woga basi ni wasisiemu au ni watu wa serikali kwa mfano magret sitta ambaye alitoka kwny cwt akawa waziri wa elimualiwasaidia nini pamoja na kujua matatatizo yenu?walimu mnafundisha democrasia na utawala bora lakini hamjui kuchagua..
walimu kama mnagoma gomeni eti mnasainisha petition vitu gani hiyo kama sio njama ya kuvuta muda ni nini?
Ila kweli walimu mmelishwa unga wa ndere hilo halina ubishi
 
Last edited:
As the group gets larger it loose cohesiveness! hicho ndicho kirusi cha CWT na zaidi viongozi wanaoweza kuhongeka kirahisi wa vyama vya wafanyakazi. Si waalimu tu waliowahi kutangaza mgomo halafu haukufanyika, TUCTA, TUICO wote hawawezi na hawataweza mpaka wawe na committed leadership, kwa viongozi walionao WASIPOTEZE MUDA ETI WATAGOMA!
 
Waalimu walio wengi kama ilivyo ada huko serikalini hawafanyi kazi tena siku hizi. Na pale wanapoingia madarasani huwa wanazuga tu siku ipite.

Mmoja wa waalimu walionifundisha sasa anamiliki kioski, na yeye ndiyo muuzaji. Nikauliza huyu aliacha lini kufundisha, nikaambiwa huyu teacher ameshaonywa lakini haijasaidia.

Ningetamani sana wagome, maana kwa kutofanya hivyo tafsiri yake ni moja kwamba watoto wenu hawataonja elimu bora. Sasa kama kuna mwenye kudhani kwamba hii issue ni ya waalimu peke yao, well, habari ndiyo hiyo!



.
 
Hivi huyu Hawa Vurugu mbona anavitisho sana? Au kwa sababu yeye ameshiba kama mashavu yake yanavyojionesha yalivyojaa? Acha vitisho vyako we mama, walimu mgomo kama kawa hadi kieleweke. Tena anzieni kwa kutofundisha kabisaaaa. Hawa watawala wetu sio viongozi hadi wapewe kashkash ndo wanawajibika.
 
Hivi huyu Hawa Vurugu mbona anavitisho sana? Au kwa sababu yeye ameshiba kama mashavu yake yanavyojionesha yalivyojaa? Acha vitisho vyako we mama, walimu mgomo kama kawa hadi kieleweke. Tena anzieni kwa kutofundisha kabisaaaa. Hawa watawala wetu sio viongozi hadi wapewe kashkash ndo wanawajibika.
Ndio wanasema wasomi walioko nje warudi wakutane na azma hii.....
 
Ndio wanasema wasomi walioko nje warudi wakutane na azma hii.....
"akataizile bwankya kaija bwaigolo"huu ni msemo wa kilugha cha kibantu na huu msemo uashilia kila mara kuwa makini mana hujui siku wala saa.

nasikia kwenye vyombo vya sisimu kuwa walimu walianza kulipwa mishahara mipya januari na pia malimbikizi mengine kwa ujumla wake kama kweli walilipwa na wakapanga mgomo basi ni "wenda wazimu" na km hawajalipwa wasipofanya mgomo wa kulitikisa taifa kama ilivyotangazwa basi wamelishwa "ndere".

chonde chonde walimu fanya kama kwanza "wasomi na simamia maamuzi yenu"
na pili fanya kama watu wanaofundisha jamii mana bila mwalimu jamii haitaelimika hivyo malengo ya millenium hayatatimia hivyo "walimu ni watu wanao sababisha vitu viende, maendeleo yaonekane na pia watu waweze kuongea na kusikika"hivyo walimu kama mtachezeshwa hivihivi kimbumbumbu basi mtkuwa mnajihaibisha mbele ya wanafunzi wenu.

"HAKUNA MTU HALIYE SOMA AMBAYE HAKUFUNDISHWA NA MWALIMU" kwaiyo umuhimu wa mwalimu uanzie hapo.

walimu mnataka nini?
mishahara minono.
teaching allowances
nyumba nzuri za kuishi

suruhisho:daini hayo yote"kwa njia yoyote ile"
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom