Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
MUSWADA HUU WA SHERIA YA MATUMIZI YA FEDHA KWA AJILI YA UCHAGUZI UMEPINGWA NA NCCR-MAGEUZI KAMA ILIVYOELEZWA HAPA CHINI:
***************************************************************
CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimepinga muswaada wa marekebisho ya sheria za uchaguzi na ule wa Sheria ya Fedha za Uchaguzi kutokana na mapungufu yaliyomo waliyosema yanavikandamiza vyama vya upinzani.
Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa NCCR, Bw. Samuel Ruhuza kuwa endapo Bunge litapitisha muswaada huo chama chake kimejipanga kwenda mahakamani kuipinga na kuichongea serikali kwa wananchi kuhusiana na uozo wake.
"Suala la kubadili na kutunga sheria zinazohusiana na uchaguzi ni suala nyeti sana kwa maendeleo ya nchi, nchi yetu imefika mahali ambapo mabadiliko ni lazima yafanyike ili tuweze kusonga mbele, lakini mabadiliko katika zama zetu yataletwa kwa njia ya sanduku la kura," alisema Bw. Ruhuza
Bw. Ruhuza alisema kama miswaada hiyo ikipitishwa na kuwa sheria, haitaleta maendeleo bali itachangia kudidimiza demokrasia nchini na kuendelea kukipendelea chama tawala.
Alisema marekebisho ya miswaada hiyo yaliyofanywa yana lengo la kuwahadaa Watanzania na jamii ya wahisani na pia ni mpango wa Rais wa Awamu ya Nne, Rais Jakaya Kikwete kujitafutia umaarufu kisiasa.
"Pamoja na upungufu mkubwa uliopo katika miswada hii ni wazi kuwa serikali itatumia wingi wa wabunge wake bungeni ili kuipitisha, kama chama tawala kilitumia wingi wake kuruhusu takrima itumike katika uchaguzi hili litawezekana pia," alisema
Alisema sheria hiyo pia inawabana wapinzani katika matumizi ya uchaguzi ambapo alidai kuwa ruzuku zinazotolewa na vyama vya siasa ni zaidi bilioni mbili, ambazo hutokana na kodi za wananchi.
Kwa upande wa muswada wa Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi alisema mapungufu yaliyopo katika kifungu cha 4(1)ambacho kinampa msajili mamlaka ya kusimamia na kuhakiki matumizi ya uchaguzi kwa vyama vya siasa.
"Hiyo ni sheria ya kubana wapinzani katika uchaguzi, utajiri wako ndio utakaokupa ubunge na udiwani, kama wewe lofa ni bora uondoke,"
Alisema katika kifungu cha 12(1) na (3) cha muswaada huu kinazuia mtu, asasi, shirika au kampuni kuingiza nchini fedha kutoka nje ndani ya siku 90 kabla ya Uchaguzi Mkuu au ndani ya siku 30 kabla ya uchaguzi mdogo.
"Inasema fedha za kutoka nje zifike situ tisini kabla hata hujamjua mgombea wako, hiyo sio haki na ndio maana wao wameanza kuagiza magari mapema kwa kuwa walitambua wanachotaka kuanzisha," alisema.
NCCR imependekeza kufuta vifungu vyote vinavyokandamiza vyama vya upinzani na kuipa Tume ya Uchaguzi mamlaka ya kuteua maafisa na wafanyakazi wake kama inavyoona inafaa, na siyo kuwateua maafisa wa serikali kama ilivyo sasa.
SOURCE: http://www.majira.co.tz/index.php?o...-uchaguzi&catid=34:kitaifa-tanzania&Itemid=57
Je, madai ya NCCR-Mageuzi ni ya msingi, esp wanapozungumzia kuhusu kukandamizwa kwa vyama vya siasa vya upinzani (mambo ya siku 90 au 30)? Tujadili!
***************************************************************
CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimepinga muswaada wa marekebisho ya sheria za uchaguzi na ule wa Sheria ya Fedha za Uchaguzi kutokana na mapungufu yaliyomo waliyosema yanavikandamiza vyama vya upinzani.
Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa NCCR, Bw. Samuel Ruhuza kuwa endapo Bunge litapitisha muswaada huo chama chake kimejipanga kwenda mahakamani kuipinga na kuichongea serikali kwa wananchi kuhusiana na uozo wake.
"Suala la kubadili na kutunga sheria zinazohusiana na uchaguzi ni suala nyeti sana kwa maendeleo ya nchi, nchi yetu imefika mahali ambapo mabadiliko ni lazima yafanyike ili tuweze kusonga mbele, lakini mabadiliko katika zama zetu yataletwa kwa njia ya sanduku la kura," alisema Bw. Ruhuza
Bw. Ruhuza alisema kama miswaada hiyo ikipitishwa na kuwa sheria, haitaleta maendeleo bali itachangia kudidimiza demokrasia nchini na kuendelea kukipendelea chama tawala.
Alisema marekebisho ya miswaada hiyo yaliyofanywa yana lengo la kuwahadaa Watanzania na jamii ya wahisani na pia ni mpango wa Rais wa Awamu ya Nne, Rais Jakaya Kikwete kujitafutia umaarufu kisiasa.
"Pamoja na upungufu mkubwa uliopo katika miswada hii ni wazi kuwa serikali itatumia wingi wa wabunge wake bungeni ili kuipitisha, kama chama tawala kilitumia wingi wake kuruhusu takrima itumike katika uchaguzi hili litawezekana pia," alisema
Alisema sheria hiyo pia inawabana wapinzani katika matumizi ya uchaguzi ambapo alidai kuwa ruzuku zinazotolewa na vyama vya siasa ni zaidi bilioni mbili, ambazo hutokana na kodi za wananchi.
Kwa upande wa muswada wa Sheria ya Matumizi ya Uchaguzi alisema mapungufu yaliyopo katika kifungu cha 4(1)ambacho kinampa msajili mamlaka ya kusimamia na kuhakiki matumizi ya uchaguzi kwa vyama vya siasa.
"Hiyo ni sheria ya kubana wapinzani katika uchaguzi, utajiri wako ndio utakaokupa ubunge na udiwani, kama wewe lofa ni bora uondoke,"
Alisema katika kifungu cha 12(1) na (3) cha muswaada huu kinazuia mtu, asasi, shirika au kampuni kuingiza nchini fedha kutoka nje ndani ya siku 90 kabla ya Uchaguzi Mkuu au ndani ya siku 30 kabla ya uchaguzi mdogo.
"Inasema fedha za kutoka nje zifike situ tisini kabla hata hujamjua mgombea wako, hiyo sio haki na ndio maana wao wameanza kuagiza magari mapema kwa kuwa walitambua wanachotaka kuanzisha," alisema.
NCCR imependekeza kufuta vifungu vyote vinavyokandamiza vyama vya upinzani na kuipa Tume ya Uchaguzi mamlaka ya kuteua maafisa na wafanyakazi wake kama inavyoona inafaa, na siyo kuwateua maafisa wa serikali kama ilivyo sasa.
SOURCE: http://www.majira.co.tz/index.php?o...-uchaguzi&catid=34:kitaifa-tanzania&Itemid=57
Je, madai ya NCCR-Mageuzi ni ya msingi, esp wanapozungumzia kuhusu kukandamizwa kwa vyama vya siasa vya upinzani (mambo ya siku 90 au 30)? Tujadili!