TUJADILI: Job Ndugai kuandika barua ya kujiuzulu kwa mtu asiyehusika ni bahati mbaya au makusudi?

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,663
18,036
Ni vigumu kuamini kuwa Mheshimiwa Ndugai hajui utaratibu wa kikatiba wa kujiuzulu nafasi ya uspika. Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania spika au naibu spika anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kuandika barua kwa BUNGE na kuisaini. Spika atahesabika kuwa amejiuzulu baada ya barua yake kupokelewa na Bunge.

Afisa wa bunge anayeshughulika na mambo ya utawala ni Katibu wa bunge. Lakini Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu wa CCM, mtu ambaye katiba haijamtaja katika mchakato wa spika kujiuzulu.

Kwa mantiki hiyo, kikatiba Ndugai bado hajajiuzulu, maana hajaandika barua ya kujiuzulu kwa mamlaka inayohusika!! Je hii imetokea kwa makusudi au kwa bahati mbaya? Sidhani kama angeamua kuchukua uamuzi mkubwa kiasi hicho bila ya kujiridhisha matakwa ya kikatiba kuhusu hatua hiyo au bila ya ushauri wa kisheria.

Ninaamini Ndugai amefanya hivyo kwa makusudì, huku akijua kuwa maadui zake amewapa mwanasesere badala ya mtoto!! Watakapogundua kuwa wamepewa mwanasesere atakuwa amejipanga kwa mapambano sawasawa!!

Kinachonishangaza zaidi ni katibu wa CCM kukubali kupokea barua hiyo ambayo kikatiba haikupaswa kuelekezwa kwake!! Nilidhani asingekubali kuipokea bali angemwelekeza mahali pa kuipeleka!! Hivi CCM makao makuu hawana mwanasheria wa chama?

Usikute huyo Katibu mkuu wa CCM naye akawa ni sehemu ya mchezo ili kuzuga huku akijua mchezo unakoelekea!! Mama shituka!! mhoji katibu wako kwa nini asingemwelekeza Ndugai utaratibu wa kikatiba wa kujiuzulu?

Mchezo umepangwa kuchezewa mahakamani na wachezaji wanajulikana!! mchezaji wa kiungo upande wa Ndugai ni MBATIA!! Ndugai atakuwa kimyaaa!!!! As if hajui kitakachoendelea!!
 
Ni vigumu kuamini kuwa Mh Ndugai hajui utaratibu wa kikatiba wa kujiuzulu nafasi ya uspika. Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania ibara ya 149, kifungu kidogo cha1-2...
Kwa kawaida utaratibu unakuwaje?
 
Mbatia tayari ameonesha nia ya kwenda mahakamani kuzuia mchakato wa kuchagua spika mpya, maana barua ya Ndugai ya kujiuzulu ni batili kwa kukosa kufuata utaratibu wa kisheria!!

Ukitaka kuchokoza nyuki muulize Ndugai kwa nini ameamua kuandika kwa katibu wa CCM badala ya kwa katibu wa bunge kama Katiba inavyoelekeza?
 
Kwani tunavyosemaga hapa kila siku kuwa MATAGA hayana akili hukuwahi kuelewa kuwa huwa tunamaanisha nini?
 
Job hajui Katiba inasemaje ,kama aliweza kulinajisi bunge kipindi cha mwendazake.

Hata sasa alikuwa na wabunge wasio na chama bungeni ,lakini aliendelea kuinajisi katiba kwa kuwakingia kifua.

Alikuwa spika wa hovyo kuwahi kutokea.
 
Mbatia tayari ameonexha nia ya kwenda mahakamani kuzuia mchakato wa kuchagua spika mpya, maana barua ya Ndugai ya kujiuzulu ni batili kwa kukosa kufuata utaratibu wa kisheria!!
Ukitaka kuchokoza nyuki mwulize Ndugai kwa nini ameamua kuandika kwa katibu wa ccm badala ya kwa katibu wa bunge kama Katiba inavyoelekeza?
Hata kama ukisema Chatle kwetu Bado no saw tu.
 
Job hajui Katiba inasemaje ,kama aliweza kulinajisi bunge kipindi cha mwendazake.
Hata sasa alikuwa na wabunge wasio na chama bungeni ,lakini aliendelea kuinajisi katiba kwa kuwakingia kifua.
Alikuwa spika wa hovyo kuwahi kutokea.
Kwa kuwa Sasa anamuda mzuri atakuwa anaweza kutafakari yote nakutambua alikokuwa anakosea.
 
Alikua anatetemeka kwa hofu na wasiwasi wa safari yake ijayo, maana hakuamini kilicho tokea
 
Job hajui Katiba inasemaje ,kama aliweza kulinajisi bunge kipindi cha mwendazake.
Hata sasa alikuwa na wabunge wasio na chama bungeni ,lakini aliendelea kuinajisi katiba kwa kuwakingia kifua.
Alikuwa spika wa hovyo kuwahi kutokea.
Hayo yote ni makusudi maana anaamini yuko juu ya sheria!!
 
Kwa hiyo kwa mujibu wa katiba Ndugai bado hajajiuzulu maana hajaandika barua ya kujiuzulu kwa wanaohusika! Na sioni mtu wa kumwambia aandike barua yake kunakohusika. Aliyepaswa kumwambia ni katibu mkuu wa ccm ambaye inaelekea ameshakula chenga ya mwili tayari au ameamua kufunga goli golini kwake!! Huu mchezo si wa kitoto!!
 
Ni vigumu kuamini kuwa Mheshimiwa Ndugai hajui utaratibu wa kikatiba wa kujiuzulu nafasi ya uspika. Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania spika au naibu spika anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kuandika barua kwa BUNGE na kuisaini...
Inasemekana barua alipelekewa Na "watoto wa mbwa" asaini tu. Ilikuwa imeshachapwa tayari Na hao wasiojulikana.
 
Ni vigumu kuamini kuwa Mheshimiwa Ndugai hajui utaratibu wa kikatiba wa kujiuzulu nafasi ya uspika. Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania spika au naibu spika anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kuandika barua kwa BUNGE na kuisaini. Spika atahesabika kuwa amejiuzulu baada ya barua yake kupokelewa na Bunge.

Afisa wa bunge anayeshughulika na mambo ya utawala ni Katibu wa bunge. Lakini Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu wa CCM, mtu ambaye katiba haijamtaja katika mchakato wa spika kujiuzulu.

Kwa mantiki hiyo, kikatiba Ndugai bado hajajiuzulu, maana hajaandika barua ya kujiuzulu kwa mamlaka inayohusika!! Je hii imetokea kwa makusudi au kwa bahati mbaya? Sidhani kama angeamua kuchukua uamuzi mkubwa kiasi hicho bila ya kujiridhisha matakwa ya kikatiba kuhusu hatua hiyo au bila ya ushauri wa kisheria. Ninaamini Ndugai amefanya hivyo kwa makusudì, huku akijua kuwa maadui zake amewapa mwanasesere badala ya mtoto!! Watakapogundua kuwa wamepewa mwanasesere atakuwa amejipanga kwa mapambano sawasawa!!

Kinachonishangaza zaidi ni katibu wa CCM kukubali kupokea barua hiyo ambayo kikatiba haikupaswa kuelekezwa kwake!! Nilidhani asingekubali kuipokea bali angemwelekeza mahali pa kuipeleka!! Hivi CCM makao makuu hawana mwanasheria wa chama?? Usikute huyo Katibu mkuu wa CCM naye akawa ni sehemu ya mchezo ili kuzuga huku akijua mchezo unakoelekea!! Mama shituka!! mhoji katibu wako kwa nini asingemwelekeza Ndugai utaratibu wa kikatiba wa kujiuzulu?
Mchezo umepangwa kuchezewa mahakamani na wachezaji wanajulikana!! mchezaji wa kiungo upande wa Ndugai ni MBATIA!! Ndugai atakuwa kimyaaa!!!! As if hajui kitakachoendelea!!
Yupo kizuizini.
 
Ili ndugai apate posho zake za kustaafu itatakiwa aprove kwamba kajiuzulu. The onus is on his side. Vinginevyo posho inaota mbawa mpaka atakapo thibitisha.
 
Hakuna cha kujadili hapa.
Job Ndugai aliandikiwa taarifa ya kujiuzulu.
Najulishwa aliwahi kufanya hivyo kwa kuandika barua kutoka kwa Mnyika kuwathibitisha Covid-19.
 
Tumeona leo Mahakama ikitupilia mbali pingamizi Mbatia juu ya utaratibu wa kujiuzulu kwa Mh Ndugai, ajabu Mahakama na Serikali wameonesha kutoitambua barua ambayo ilitolewa public twenye tovuti ya bunge pamoja na kurasa za Bunge za kijamii.
JamiiForums-1303604737.jpeg


Barua hii hapa juu Serikali wameikana leo Mahakamani licha ya kuwa ilithibitishwa na Katibu wa Bunge .

KT.PNG


Serikali imepeleka Mahakamani barua nyingine kuwa ndiyo iliandikwa na Mh Job Ndugai kwenda kwa Katibu wa Bunge.
20220128_133025.jpg

Hii juu ndiyo barua iliyopelekwa Mahamani kama kithibitisho kuwa Spika Ndugai alifuata utaratibu ijapokuwa Barua hii hatukuiona kabla.

Nani aliandika Barua ya mwanzo kabisa kwenda kwa katibu wa Chama? Ni ishara barua zotebili hazikuandikwa na Job Yustino Ndugai mwenyewe.
 
Tumeona leo Mahakama ikitupilia mbali pingamizi Mbatia juu ya utaratibu wa kujiuzulu kwa Mh Ndugai, ajabu Mahakama na Serikali wameonesha kutoitambua barua ambayo ilitolewa public twenye tovuti ya bunge pamoja na kurasa za Bunge za kijamii.View attachment 2098333

Barua hii hapa juu Serikali wameikana leo Mahakamani licha ya kuwa ilithibitishwa na Katibu wa Bunge .

View attachment 2098335

Serikali imepeleka Mahakamani barua nyingine kuwa ndiyo iliandikwa na Mh Job Ndugai kwenda kwa Katibu wa Bunge.View attachment 2098336
Hii juu ndiyo barua iliyopelekwa Mahamani kama kithibitisho kuwa Spika Ndugai alifuata utaratibu ijapokuwa Barua hii hatukuiona kabla.

Nani aliandika Barua ya mwanzo kabisa kwenda kwa katibu wa Chama? Ni ishara barua zotebili hazikuandikwa na Job Yustino Ndugai mwenyewe.
We bwanawe hawa watu watukuumizwa kichwa vibaya mnoo,, hii nchi ni hovyo
 
Back
Top Bottom