Zurie
JF-Expert Member
- Jul 6, 2014
- 1,686
- 3,992
Watanzania kuna vitu fulani tunaendekeza ambavyo havina mantiki kwakweli.
Siku hizi kuna kautaratibu kamepamba moto ambapo mtu sherehe si yake ila anakuja na watu wake wanampa zawadi akiwa amekaa mbele kabisa ukumbini.
Wiki iliyopita sisi wamama wa mtaa wetu tulienda kwenye sherehe harusi ya mdogo wa mwenzetu. Tumebeba zawadi mimi nategemea ni za maharusi ila cha kushangaza nasikia "wamama wa Mianzini wanamtunza mama Collins, tunaomba uje mbele mama Collins"
Wazazi wanatuzwa sawa, ingawa nayo sio fair wala. Ila jamani dada, wifi, shangazi, mamdogo ni vipi? Kwanini utafute umuhimu kwenye jambo lisilo lako?
Hili la wazazi pia kuna sherehe tumeenda wazazi wametuzwa masaa matatu. Hadi unabaki unajiuliza ni anniversary yao au harusi ya wenzao?
Tubadilike; mwache mwenye sherehe ang'are jamani!
Siku hizi kuna kautaratibu kamepamba moto ambapo mtu sherehe si yake ila anakuja na watu wake wanampa zawadi akiwa amekaa mbele kabisa ukumbini.
Wiki iliyopita sisi wamama wa mtaa wetu tulienda kwenye sherehe harusi ya mdogo wa mwenzetu. Tumebeba zawadi mimi nategemea ni za maharusi ila cha kushangaza nasikia "wamama wa Mianzini wanamtunza mama Collins, tunaomba uje mbele mama Collins"
Wazazi wanatuzwa sawa, ingawa nayo sio fair wala. Ila jamani dada, wifi, shangazi, mamdogo ni vipi? Kwanini utafute umuhimu kwenye jambo lisilo lako?
Hili la wazazi pia kuna sherehe tumeenda wazazi wametuzwa masaa matatu. Hadi unabaki unajiuliza ni anniversary yao au harusi ya wenzao?
Tubadilike; mwache mwenye sherehe ang'are jamani!