Tujadili hili la mtu "kutuzwa" kwenye sherehe isiyo yake

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
1,686
3,992
Watanzania kuna vitu fulani tunaendekeza ambavyo havina mantiki kwakweli.

Siku hizi kuna kautaratibu kamepamba moto ambapo mtu sherehe si yake ila anakuja na watu wake wanampa zawadi akiwa amekaa mbele kabisa ukumbini.

Wiki iliyopita sisi wamama wa mtaa wetu tulienda kwenye sherehe harusi ya mdogo wa mwenzetu. Tumebeba zawadi mimi nategemea ni za maharusi ila cha kushangaza nasikia "wamama wa Mianzini wanamtunza mama Collins, tunaomba uje mbele mama Collins"

Wazazi wanatuzwa sawa, ingawa nayo sio fair wala. Ila jamani dada, wifi, shangazi, mamdogo ni vipi? Kwanini utafute umuhimu kwenye jambo lisilo lako?

Hili la wazazi pia kuna sherehe tumeenda wazazi wametuzwa masaa matatu. Hadi unabaki unajiuliza ni anniversary yao au harusi ya wenzao?

Tubadilike; mwache mwenye sherehe ang'are jamani!
 
Duuu inakera sana asee ilitokea hata kwenye shughuli yangu kuna watu waliitumia kama fursa. Kumbe kamekuwa ni kautaratibu ka mahali pengi!!
 
Acha wamtuze labda ndio nafasi yake ya kwanza na ya mwisho. Maana kama yeye mama Kolini hajawahi kuolewa hata besdei hajawahi kufanyiwa ni bora adandie kwenye shughuli ya mwenzake ili nayeye ajione mtu.

Vumilia tu mkuu yatapita na maisha yataendelea.

Wajinga ni wengi na mda hautoshi.
 
Duuu inakera sana asee ilitokea hata kwenye shughuli yangu kuna watu waliitumia kama fursa. Kumbe kamekuwa ni kautaratibu ka mahali pengi!!

Yani hivi sasa ndo mpango mzima. Unasikia "wafanyakazi wa Voda wanataka kumtuza mjomba wa bibi harusi"
 
Hapo huyo alotunzwa naye alitunza wenzie kama hivo ni kama anarudishiwa na hapo msemo wa kutoa ni kuweka ndio hutumika

Hata sio jambo baya huku kwetu kuna vikundi hasa ikitokea mwanakikundi akaozesha au kuoza anatunzwa na wenzie japo harusi s yake tena huku kwetu ikiwa ni mwanamke anaolewa bas hao wenye vikundi hutunzana vyombo vya ndani ikiwa n mwanaume anaoa wanatunza vitenge, kanga, madira,mitandio na vitu vingi tu

Na si lazima kutunzana ila ukiona wameamua kutunzana ujue mifuko yao inaruhusu.
 
Mambo ya hizo zawadi yamekaa ki revenge sana, mtu ametoa kwa wenzake kwa muda mrefu, akipata upenyo hata kama ni shuhuli ya binamu yake anaitumia nafasi ipasavyo!!
 
Hii inatokana na vikundi vyao. Unakuta huyo hana mtoto wa kuoa au kuolewa ikitokea hivyo wanaona bora wamtunze hapohapo kuepusha lawama.

Mambo yasiwe mengi, mengi yasiwe mambo
 
Hapo huyo alotunzwa naye alitunza wenzie kama hivo ni kama anarudishiwa na hapo msemo wa kutoa ni kuweka ndio hutumika

Hata sio jambo baya huku kwetu kuna vikundi hasa ikitokea mwanakikundi akaozesha au kuoza anatunzwa na wenzie japo harusi s yake tena huku kwetu ikiwa ni mwanamke anaolewa bas hao wenye vikundi hutunzana vyombo vya ndani ikiwa n mwanaume anaoa wanatunza vitenge, kanga, madira,mitandio na vitu vingi tu

Na si lazima kutunzana ila ukiona wameamua kutunzana ujue mifuko yao inaruhusu.

Suala si mifuko ila ni ile hali ya kuiba spotlight ya mwenzio. Mambo yafanyike mahala na wakati sahihi; si kutumia sherehe ya mwenzio kuwa eneo lako la mavuno!

Ulituza wenzio hatukatai, subiri sherehe yako au labda ya mwanao utuzwe nawe sio sherehe ya binamu, ya mpwa nawe unakaa kwenye kiti unafunikwa vitenge.

Kwanini usiandae sherehe yako mwenyewe hata ya kumshukuru Mungu kwa uhai?
 
Suala si mifuko ila ni ile hali ya kuiba spotlight ya mwenzio. Mambo yafanyike mahala na wakati sahihi; si kutumia sherehe ya mwenzio kuwa eneo lako la mavuno!

Ulituza wenzio hatukatai, subiri sherehe yako au labda ya mwanao utuzwe nawe sio sherehe ya binamu, ya mpwa nawe unakaa kwenye kiti unafunikwa vitenge.

Kwanini usiandae sherehe yako mwenyewe hata ya kumshukuru Mungu kwa uhai?
Kila sehem na utaratibu wake n kila mtu anayo jinsi anaishi anavyojua yeye,

Pengine ni kweli si vyema lakini ndio kaona nafaskatumia fursa
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom