Tujadili faida na hasara ya kulipa kodi ya nyumba kwa kila mwezi na kwa miezi 6 au mwaka

kimarabucha

JF-Expert Member
Jul 29, 2017
791
621
WADAU naomba tujaribu kujikita kwenye mada tajwa hapo juu kwani nimemsikia Waziri Wa Ardhi Mh. Lukuvi sikuamini Bunge kuwa Wizara yake inatunga Sheria ya kuwataka wenye nyumba wachukue kodi ya kila mwezi badala ya miezi 6 au mwaka.

Rejea: Serikali kukataza wenye nyumba kukusanya kodi ya miezi 6, inaumiza wengi

Hoja yangu ni je ni faida gani au hasara atakayoipata mwenye nyumba na Mpangaji Kwa Sheria mpya ya upangaji?

Je ni faida/hasara gani Kwa Sheria ya Kulipa Kwa miezi 6/Mwaka anayoipata mpangaji/mwenye nyumba ?
 
Anza wewe basi kuchangiaa unaonaje???....

WADAU naomba tujaribu kujikita kwenye mada tajwa hapo juu kwani nimemsikia Waziri Wa Ardhi Mh.Lukuvi sikuamini Bunge kuwa Wizara yake inatunga Sheria ya kuwataka wenye nyumba wachukue kodi ya kila mwezi badala ya miezi 6 au mwaka.Hoja yangu ni je ni faida gani au hasara atakayoipata mwenye nyumba/Mpangaji Kwa Sheria mpya ya upangaji? Je ni faida/hasara gani Kwa Sheria ya Kulipa Kwa miezi 6/Mwaka anayoipata mpangaji/mwenye nyumba ?
 
Unakuta mwenyenyumba unamuomba kiuungwana kabisa,

Mzee/mama tafadhali Nina pesa ya miezi 2 au mitatu naomba upokee nyingine ntakupa, anakataa katakata na kukutaka uhame, ukileta ngumu anakuja kutoa vyombo nje na kukuadhirisha mbele ya hadhira

Huko utaenda kutafuta unakukana na hayo hayo, acha hiyo sheria ipite mkuu, wamejisahau sana hawa watu km alivyojisahau grace zibombo kwa dunia Mali yake na anaweza kufanya chochote kisa yupo kwenye daraja fulani
 
Hili haliwezekan kupanga sheria ya ulipaji wa kodi. Nakuomba mtoa mada upuuze kama ulivyo puuza matamko ya fuaatayo
1. Kubomoa nyumba zilizojengwa viwanja visivyo pimwa
2.Ada elekezi
 
Makubaliano/Mktaba ya mpangaji na mwenye nyumba huwa ni baina yao serikali inawezaje kuingilia. Hawa mawaziri watafakari kabla hawajatoa sheria zisizoeleweka.
Kwa sheria ikipita tutegemee wapangaji wengi watapewa notice.
 
sheria itafanya biashara ya ujenzi wa nyumba za kupanga kutokuwa na faida.
haiwezekani kujenga nyumba kwa milioni 30 halafu upokee kodi ya laki 2 kila mwezi.. lini fedha itarudi.

lakini italeta unafuu kwa wapangaji ule mzigo wa kulipa 3.6m stress zake hazikuwa za kawaida
 
Makubaliano/Mktaba ya mpangaji na mwenye nyumba huwa ni baina yao serikali inawezaje kuingilia. Hawa mawaziri watafakari kabla hawajatoa sheria zisizoeleweka.
Kwa sheria ikipita tutegemee wapangaji wengi watapewa notice.
Kwanini isiingilie?
 
sheria itafanya biashara ya ujenzi wa nyumba za kupanga kutokuwa na faida.
haiwezekani kujenga nyumba kwa milioni 30 halafu upokee kodi ya laki 2 kila mwezi.. lini fedha itarudi.

lakini italeta unafuu kwa wapangaji ule mzigo wa kulipa 3.6m stress zake hazikuwa za kawaida
Nyumba za kupangisha siku hizi ni biashara, kwa hiyo hata ile kodi ya "property tax" inazingatia hilo. Tatizo la wanasiasa ni "kiki" wengi wao wana miradi mikubwa ambayo inawawezesha kufanya mambo mbalimbali ikiwemo kulipa ada za vyuo vikuu wanao, kufanya matengenezo ya nyumba zao bila wasiwasi kwani wanapokea fedha mamilioni, Je huyu mwenye nyumba anayepokea shilingi laki 2 kwa mwezi,anahitaji kusubiri miezi mitatu kukusanya fedha ili aweze kufanya jambo kubwa, wakati huo huo anahitaji kula, matibabu na mengine mengi. Sheria hii naifananisha na ile ya Mafao ya kujitoa katika mifuko ya kijamii. Ni wakati sasa kuwa na viongozi wanaosaidia wananchi kupata maendeleo na sio kutafuta njia ya kupata kura kama ile aliyotumia mugabe ya kupora mashamba ya wazungu kwa ajili ya kupata kiki ya kisiasa, madhara yake yanaonekana. Mimi nasema hivi kama NSSF na PPF wanaweza kujenga maghorofa, basi wajenge na nyumba za kupangisha kwa kodi ya kila mwezi, lakini serikali kuwapangia wanye nyumba kupokea kodi kwa mwezi ni adhabu kubwa sana kwa wenye nyumba. Nitashangaa endapo umoja wa wamiliki wa nyumba za kupanga hawatapinga sheria hii mahakamani.
 
Hii sheria imekuja wakati ndiyo ninaanza hii biashara. Mahesabu yalikuwa nikusanye kodi ya mwaka ili ijenge nyumba nyingine
 
Kulipa kwa mwezi ni vizuri pia kama Mpangaji ana uhakika wa kulipa hivyo. Ila itakuwa kila mwezi aweke bajeti ya kulipa - hivyo kuna ususmbufu fulani hivi kwa mpangaji na mwenye nyumba - na tatizo ni pale ukipata wapangaji watata ambao wanaweza kuwa wanapiga chenga kulipa. Hivyo mwenye nyumba atalazimika kuacha kazi zake na kufuatilia kodi kila wakati. Uzuri wa miezi mitatu/sita/mwaka ni kuwa baada ya kulipana - mpangaji na mwenye nyumba hamkutani tena - mpaka miezi mitatu/sita/ mwaka upite; ndio mnatafutana.
 
Wakati wamejenga nyumba zao walipata Ruzuku kutoka serikalini?
Sio lazima wakupe ruzuku serikali lazima iregulate baadhi ya mambo.

Kwa mfano EWURA wanapanga bei ya mafuta je wametoa ruzuku ya ujenzi wa kituo husika?

Mabus yanapangiwa nauli je serikali imechangia nini?

Daladala nazo zinatumia bei elekezi.
 
Kuchukua kodi ya mwezi ni kama hela ya mafungu usipoangalia unaishia kubadilisha mboga tu
 
Nyumba za kupangisha siku hizi ni biashara, kwa hiyo hata ile kodi ya "property tax" inazingatia hilo. Tatizo la wanasiasa ni "kiki" wengi wao wana miradi mikubwa ambayo inawawezesha kufanya mambo mbalimbali ikiwemo kulipa ada za vyuo vikuu wanao, kufanya matengenezo ya nyumba zao bila wasiwasi kwani wanapokea fedha mamilioni, Je huyu mwenye nyumba anayepokea shilingi laki 2 kwa mwezi,anahitaji kusubiri miezi mitatu kukusanya fedha ili aweze kufanya jambo kubwa, wakati huo huo anahitaji kula, matibabu na mengine mengi. Sheria hii naifananisha na ile ya Mafao ya kujitoa katika mifuko ya kijamii. Ni wakati sasa kuwa na viongozi wanaosaidia wananchi kupata maendeleo na sio kutafuta njia ya kupata kura kama ile aliyotumia mugabe ya kupora mashamba ya wazungu kwa ajili ya kupata kiki ya kisiasa, madhara yake yanaonekana. Mimi nasema hivi kama NSSF na PPF wanaweza kujenga maghorofa, basi wajenge na nyumba za kupangisha kwa kodi ya kila mwezi, lakini serikali kuwapangia wanye nyumba kupokea kodi kwa mwezi ni adhabu kubwa sana kwa wenye nyumba. Nitashangaa endapo umoja wa wamiliki wa nyumba za kupanga hawatapinga sheria hii mahakamani.
 
Rais Magufuli akitaka kupiga hatua za maendeleo aachie kuteua viongozi kama mawaziri kwa kufuata ukada wa chama.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom