Tujadili faida na hasara ya kulipa kodi ya nyumba kwa kila mwezi na kwa miezi 6 au mwaka

Nadhani wabunge wanastahili kuelewa kuwa kila mtu ktk biashara ana malengo yake. Biashara ya kujenga nyumba na kupangisha ina malengo yake mhusika. Huwezi kunilazimisha nipokee kodi kwa mwezi kwasababu siyo mipango yangu ktk biashara yangu. Kama serekali inataka ijenge nyumba nyingi hata ikitaka kukodisha na kupokea kodi ya nusu mwezi ni hiari yake. Jamani wenzetu nchi nyingine wamepiga hatua zaidi. Na serekali zao zinawasaidia na siii kuwadidimiza. Nilipanga chumba kimoja pale Bangalo India. Nililipa kodi ya mwaka mmoja na fedha ya tahadhari $300 (fedha ya tahadhari hapa kwetu Hakuna) fedha hii inatumika pale mkataba wako utakapokwisha ilikupiga rangi na kurudishia vifaa ambavyo vimeharibika wakati wewe ukiwa mpangaji. Hapa kwetu hilo halipo. Biashara hururia iwe huria kweli. Wabunge wajadili hoja za maana zidi.
 
Nimeshampa notice mpangaji wangu leo. Sjui kausikia wapi uzushi huu ati ananiambia anataka kulipa kwa mwezi hata mwezi. Nikamwambia katafute vyumba tandale ndio wenye nyumba kila mwezi wanaweza kuja kukusanya kodi. Mi ni 6 au 12 months hapa.

Anyway, hii sheria isipoangaliwa wapangaji wataumia sana. Kila baada ya mwezi tutaandika mkataba mpya na hanizuii kupandisha kodi kila mwezi. Tofauti na sasa hivi ukishalipa kodi ya mwaka hautarajii kupata ongezeko la kodi kabla ya mwaka kuisha.
 
Kulipa kwa miezi mitatu tatu nadhani ni bora zaidi kuliko miezi sita na mwaka
 
Kulipa kwa miezi mitatu tatu nadhani ni bora zaidi kuliko miezi sita na mwaka
Wengine tulipangisha ili kujisogeza kimaisha. Uko chukua pangolin la mwaka nyumba mbili una nunua kiwanja. Sasa haya mafungu mafungu ya kila mwezi haya.
 
Mimi binafsi naona ni vizuri sana kwa sababu ilikuwa inafika wakati mpangaji anamaliza kodi yake alafu hana ela ya kulipa miezi.sita au mwaka akimwambia mwenyenyumba ampe kiasi alicho nacho mfano miezi mitatu mwenye nyumba hataki sasa anamwambia amuachie chuma/nyumba yake sasa inafaa sana kulipa mwezi mmoja ila kwa kuwa ni mkataba mnakubaliana kama.unayo zaidi ya mwezi mmoja mnakubaliana unampa hata miezi mitatu au zaid unaweza kumpa
 
Kwanza inakupasa ujue unafanya mjadala na nani.
Mwenye nyumba, mpangaji au wanaokaa bure kwenye nyumba za wazazi wao na walioachiwa waangalie ulinzi wa nyumba.

Ingependeza kila mchangiaji akisema yeye amepanga au ni mwenye nyumba au anaishi bure.
Naanza mimi.

Mimi ni mpangaji. Naona sheria ya mwezi mmoja ni nzuri kwakua haina hasara wala faida kwa wote. Kinachotokea ni kwamba hapa anapewa unafuu yule mpangaji ambaye ndiye mnyonge. Mpangaji anayepewa nafuu ni yule ambaye hawezi kuweka hela kidogo kidogo kwa muda wa miezi sita au mwaka ili azikabidhi kwa pamoja kwa mwenye nyumba. Mfano mdogo ni huu hapa. Mimi nimeajiriwa sehemu ambayo nalipwa mshahara. Kila mwezi huwa natenga kiasi cha kodi ambacho ukishaisha mkataba wangu wa nyumba, namlipa mama mwenye nyumba. Kwahiyo hata ikipitishwa sheria ya mwezi mmoja, haitanidhuru maana kodi ya mwezi ujao nakua nimeshaiweka kwenye bajeti kutoka kwenye mshahara wangu.

Pili hii sheria haitamkataza mlipa kodi kulipa kodi ya miezi sita au mwaka kwa mkupuo. Wenye uwezo watalipa na wasio na uwezo watalipa mwezi mmoja. Hiyo ndo tafsiri yangu.

Kwamba tufanye mkataba umeisha alafu mkononi una hela ya mwezi mmoja. Kama sheria hiyo haipo ni kwamba lazima uhame. Kama ipo basi utalipa mwezi huo wakati unafanya mipango mingine.

Wanaopinga hili ni wenye nyumba. Wanajua fika kuwa hela haiwekeki ndio maana wanalalamika. Kupokea hela ya mwezi mmoja mmoja kwa mwenye nyumba, anaona kama hapati kitu. Ndio maana wanataka wapangaji ndo wawawekee ili wao wazichukue kwa pamoja.
 
1.) Kudai kodi kuna gharama zake, sasa badala ya kudai kodi mara moja au mbili kwa mwaka, mwenye nyumba atalazimika kudai kodi hadi mara 12 kwa mwaka, je, nani atagharamia cost hizi za ziada? ( Kupiga simu, kuandaa na kusaini mikataba kila mwezi, kutenga muda wa kusainishana na kupokea kodi kila mwezi, na overheads nyingine kibao)

2.) Kiwango cha kodi kinachopangwa huwa in consideration kwamba kodi inalipwa mara moja au mbili kwa mwaka kwa mkupuo, sasa unapoongeza idadi ya installments ni lazima kodi itapandishwa, ni kama unaponunua soda moja moja na unaponunua kreti zima kwa mkupuo, mwenye duka atakuoa bei ndogo per unit kama ukinunua kreti kwa mkupuo, na atakupa bei kubwa ukinunua moja moja, je, wapangaji wako tayari kupandishiwa kodi ili tu walipe kwa awamu nyingi zaidi?
3.) Mkataba ni makubaliano baina ya mwenye nyumba na mpangaji, kama mwenye nyumba hataki basi hakuna makubaliano (mkataba), sasa utaenforce vipi kumpangia mtu jinsi ya kuuza huduma yake? Ni kama kuforce kununua kalamu kwa rejareja kwenye duka la jumla, mwenye duka anakuambia anauza kuanzia boksi 1 na kuendelea, wewe unataka uuziwe kalamu moja, utalazimisha?
 
Kwanza inakupasa ujue unafanya mjadala na nani.
Mwenye nyumba, mpangaji au wanaokaa bure kwenye nyumba za wazazi wao na walioachiwa waangalie ulinzi wa nyumba.

Ingependeza kila mchangiaji akisema yeye amepanga au ni mwenye nyumba au anaishi bure.
Naanza mimi.

Mimi ni mpangaji. Naona sheria ya mwezi mmoja ni nzuri kwakua haina hasara wala faida kwa wote. Kinachotokea ni kwamba hapa anapewa unafuu yule mpangaji ambaye ndiye mnyonge. Mpangaji anayepewa nafuu ni yule ambaye hawezi kuweka hela kidogo kidogo kwa muda wa miezi sita au mwaka ili azikabidhi kwa pamoja kwa mwenye nyumba. Mfano mdogo ni huu hapa. Mimi nimeajiriwa sehemu ambayo nalipwa mshahara. Kila mwezi huwa natenga kiasi cha kodi ambacho ukishaisha mkataba wangu wa nyumba, namlipa mama mwenye nyumba. Kwahiyo hata ikipitishwa sheria ya mwezi mmoja, haitanidhuru maana kodi ya mwezi ujao nakua nimeshaiweka kwenye bajeti kutoka kwenye mshahara wangu.

Pili hii sheria haitamkataza mlipa kodi kulipa kodi ya miezi sita au mwaka kwa mkupuo. Wenye uwezo watalipa na wasio na uwezo watalipa mwezi mmoja. Hiyo ndo tafsiri yangu.

Kwamba tufanye mkataba umeisha alafu mkononi una hela ya mwezi mmoja. Kama sheria hiyo haipo ni kwamba lazima uhame. Kama ipo basi utalipa mwezi huo wakati unafanya mipango mingine.

Wanaopinga hili ni wenye nyumba. Wanajua fika kuwa hela haiwekeki ndio maana wanalalamika. Kupokea hela ya mwezi mmoja mmoja kwa mwenye nyumba, anaona kama hapati kitu. Ndio maana wanataka wapangaji ndo wawawekee ili wao wazichukue kwa pamoja.
Umenena vyema sana. Ubinafsi wa wenye nyumba hautawaacha salama. Hii sheria ipite hata kesho.
 
Sio lazima wakupe ruzuku serikali lazima iregulate baadhi ya mambo.

Kwa mfano EWURA wanapanga bei ya mafuta je wametoa ruzuku ya ujenzi wa kituo husika?

Mabus yanapangiwa nauli je serikali imechangia nini?

Daladala nazo zinatumia bei elekezi.
Tofautisha bei elekezi na awamu za ulipaji elekezi, imagine wauza mafuta wangetakiwa kupokea pesa ya hadi mafuta ya sh.1
 
Sukari imewashinda mpaka leo bei juu!sasa mnakuja na mambo ya nyumba za watu mliwasaidia kuzijenga?Hii ni nchi yetu sote tusiwekeane sheria za ajabu ajabu.
 
Nimeshampa notice mpangaji wangu leo. Sjui kausikia wapi uzushi huu ati ananiambia anataka kulipa kwa mwezi hata mwezi. Nikamwambia katafute vyumba tandale ndio wenye nyumba kila mwezi wanaweza kuja kukusanya kodi. Mi ni 6 au 12 months hapa.

Anyway, hii sheria isipoangaliwa wapangaji wataumia sana. Kila baada ya mwezi tutaandika mkataba mpya na hanizuii kupandisha kodi kila mwezi. Tofauti na sasa hivi ukishalipa kodi ya mwaka hautarajii kupata ongezeko la kodi kabla ya mwaka kuisha.
Kila.mwezi kuwaongezea 30,000
 
Back
Top Bottom