Tuipigie chapuo bangi (marijuana) bunge likubali kuwa zao la biashara

TheDreamer Thebeliever

JF-Expert Member
Feb 26, 2018
2,490
3,534
Habari wadau..!
Najua humu ndani kuna greater thinkers wengi ,kama jambo tutalipitisha hapa basi bungeni watalitafakari kwa kina.

Nchi nyingi duniani zimehalalisha matumizi ya bange na wanatengeneza pesa ndefu sana .

Kwa kwetu pamba,korosho ,kahawa naona zinasuasua kwa nn basi tusipigie chapuo kilimo cha bangi kwa biashara (only export) nadhani great thinkers mmenielewa au mnaonaje?
 
Ukikuta polisi wanachoma bangi, tafsiri yake ni wanachoma mamilioni ya shilingi. Waache watu waitumie. Maana inauzwa kila kona ya hii nchi na kila mtaa ipo.

Polisi wenyewe wanavuta. Jw na wanavuta.

Hivi Mungu alipowaambia Adam na Hawa kuwa wayatumie majani ya kondeni alikuwa anazungumzia majani gani? Mchicha? Spinach? Au kit gani haswa?
Alimaanisha majani yanayofaa kwa matumizi. Kula au kuvuta.

Bange ina faida kubwa kuliko hasara. Kiuchumi na kiafya pia.
 
Hili zao ,serikali inachelewa Sana ,kulihalalisha ,soko lake ni Pana Sana duniani,Malawi Wana mwaka wa 3,Sasa wanapiga dola ndefu kwa hili zao,Kuna makampuni kule kabisa yananunua zao Hilo,pia serikali ya Malawi imeliorodhesha na kulitambua zao la marijuana Kama zao la kimkakati la biashara.
 
Tunacheleweshwa Sana ndugu zanguni
Wakiruhusu hii kitu nawaambia nitakua wa kwanza kuwekeza kwenye ka ekari kangu ka home nyumbanitu Njombe huku maana ni inakubali Sana na ka hali ka hewa huku

Nitakua nimejikwamua kufikia uchumi wa kati!
🖕
 
Biashara ya bangi inalipa sana,vijana wadogo tu wanatoboa ila kikwazo ni kwamba ukikutwa na ma afande ni msala
Serkali iangalie vizur hili suala vijana wajiajir na kilimo cha bangi watoboe maisha
 
Wababe wa kugeuza "adimu" kuwa fursa: pharmaceutical companies...walijaribu kuzalisha ingredients za bangi kwenye maabara ili watengeneze kidonge wauze kama dawa ya kutuliza mfadhaiko, kuleta hamu ya kula, hamu ya kufanya mapenzi, kutibu maumivu ya hedhi, kuleta uzingativu, nk ( maana kutaja faida za bangi itanichukua wiki naandika) walishindwa wakanyanyua mikono juu. Bangi haina mbadala wake!
 
Wababe wa kugeuza "adimu" kuwa fursa: pharmaceutical companies...walijaribu kuzalisha ingredients za bangi kwenye maabara ili watengeneze kidonge wauze kama dawa ya kutuliza mfadhaiko, kuleta hamu ya kula, hamu ya kufanya mapenzi, kutibu maumivu ya hedhi, kuleta uzingativu, nk ( maana kutaja faida za bangi itanichukua wiki naandika) walishindwa wakanyanyua mikono juu. Bangi haina mbadala wake!
unamaanisha haina mbadala?
 
Nina kishamba mlimani zinajioteaga 2-3, hiyo ni dalili zinastawi katika eneo hilo, ngoja tujadiliane na wife hapa, hichi kilimo. Tuuzie beberu.

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Mama aje na Kauli Mbiu ya

VIJANA RUDINI VIJIJINI.

mlioko karibu na mama mwambieni aturuhusu vijana turudi vijijini tukaitendee haki ardhi tuliyonayo. Na chukua hii kutoka kwangu, ikiruhusiwa tu hata uvutaji utapungua kwa kasi ya ajabu mpaka ushangae sababu siwezi acha dola 3000 niuze kijiti kwa 1000 ya madafu.
 
Wababe wa kugeuza "adimu" kuwa fursa: pharmaceutical companies...walijaribu kuzalisha ingredients za bangi kwenye maabara ili watengeneze kidonge wauze kama dawa ya kutuliza mfadhaiko, kuleta hamu ya kula, hamu ya kufanya mapenzi, kutibu maumivu ya hedhi, kuleta uzingativu, nk ( maana kutaja faida za bangi itanichukua wiki naandika) walishindwa wakanyanyua mikono juu. Bangi haina mbadala wake!

Mbona inauzwa sana kwenye pharmacists na maduka mengi duniani?
Nanunua sana Holland & Barrett nilinunua mafuta ya bangi kwa ajili ya maumivu ya mgongo
 
'Deep down inna di earth where me put di ganja
Babylon come and light it up on fire
Me a chant
Yes I'm a ganja planter
Call me di ganja farmer'

Marlon Asher
Ganja Farmer
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom