Tuijadili na Kuichambua Katiba Yetu

Safari_ni_Safari

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
23,273
17,096
Katiba yenyewe hii hapa http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf

Mimi naanzia kwenye utangulizi.

Hivi tuliamua lini haya na tuliamua vipi?Tulipiga kura au?Mimi sikumubki kushiriki

Halafu hapo nilipo underline mbona hapaeleweki

Sheria ya 1984
Na.15 ib.3
KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi
yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na
amani:
NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika
jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na
Bunge
lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha
wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu
wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo
kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na
kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu:
KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE
MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
,
kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii
kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania
inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia
na ujamaa.
 
Nimeipitia na sijaona mahala amabapo katiba ya Zanzibar imetajwa? Kisheria si ilipaswa iwe hivyo?
 
Haki ya kupiga
kura
Sheria ya 1984
Na.15 ib.6
Sheria ya 2000
Na.3 ib.4
5.-(1) Kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka
kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi
unaofaywa Tanzania na wananchi. Na haki hii itatumiwa kwa
kufuata masharti ya ibara ndogo ya (2) pamoja na masharti
mengineyo ya Katiba hii na ya Sheria inayotumika nchini
Tanzania kuhusu mambo ya uchaguzi.
(2) Bunge laweza kutunga sheria na kuweka masharti
yanayoweza kuzuia raia asitumie haki ya kupiga kura kutokana
na yoyote kati ya sababu zifuatazo, yaani raia huyo-
(a) kuwa na uraia wa nchi nyingine;
(b) kuwa na ugonjwa wa akili;
(c) kutiwa hatiani kwa makosa fulani ya jinai;
(d) kukosa au kushindwa kuthibitisha au kutoa
kitambulisho cha umri, uraia au uandikishwaji kama
mpiga kura,
mbali na sababu hizo hakuna sababu nyingine yoyote
inayoweza kumzuia raia asitumie haki ya kupiga kura.
(3) Bunge litatunga Sheria ya Uchaguzi na kuweka
masharti kuhusu mambo yafuatayo-
(a) kuanzisha Daftari la Kudumu la Wapiga kura na
kuweka utaratibu wa kurekebisha yaliyomo katika
Daftari hilo;
(b) kutaja sehemu na nyakati za kuandikisha wapiga
kura na kupiga kura;
(c) utaratibu wa kumwezesha mpiga kura
aliyejiandikisha sehemu moja kupiga kura sehemu
nyingine na kutaja masharti ya utekelezaji wa
utaratibu huo
;
(d) kutaja kazi na shughuli za Tume ya Uchaguzi na
utaratibu wa kila uchaguzi ambao utaendeshwa
chini ya uongozi na usimamizi wa Tume ya
Uchaguzi.
 
Mi nimevutiwa na hii:
(c)" utaratibu wa kumwezesha mpiga kura
aliyejiandikisha sehemu moja kupiga kura sehemu
nyingine na kutaja masharti ya utekelezaji wa
utaratibu huo
; "Kwa swala la uchaguzi naona tuanzie hapa
 
Nimeipitia na sijaona mahala amabapo katiba ya Zanzibar imetajwa? Kisheria si ilipaswa iwe hivyo?
Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.
 
Katiba yenyewe hii hapa http://www.tanzania.go.tz/images/katibamuungano.pdf

Mimi naanzia kwenye utangulizi.

Hivi tuliamua lini haya na tuliamua vipi?Tulipiga kura au?Mimi sikumubki kushiriki

Halafu hapo nilipo underline mbona hapaeleweki

Sheria ya 1984
Na.15 ib.3
KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi
yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na
amani:
NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika
jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na
Bunge
lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha
wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu
wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo
kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na
kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu:
KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE
MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
,
kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii
kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania
inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia
na ujamaa.

Katiba hii imepitwa na wakati na imejikita sana kwenye mfumo wa chama kimoja cha siasa kilichoshika hatamu.

Walisahau kuondoa maneno serikaliyenye kufuata misingi ya kijamaa, hiyo iliondolewa zamani wakati wa Azimio la Zanzibar lakini katiba yetu maneno bado yapo. Preamble ni misleading kabisa mahakama hazitendi haki, wabunge wengine hawakuchaguliwa ili mradi ni vurugu tu.

Tubadili katiba hii haitufai kabisa
 
Tatizo kubwa tulilo nalo ni yule mama waliyemuweka tena bila hata naibu, coz amri ikitoka kwake ndo imepita, hakuna mshauri. Dk. Slaa akisema Sitta ameshushiwa hadhi wa2 wanamshangaa, imagine Sitta angepewa wizara hii,kazi isingekuwa ngumu, nadhani tungefika mbali. Can u imagine keshaanza kujichanganya sa hivi eti kuandaa katiba mpya ni gharama, so ina maana inawezekana tatizo ni gharama siyo? Sasa sijui atawaambiaje wazee wa sisiem kama iko kwenye ilani ya chama au vipi. Sijui ataendelea kujikanyagakanyaga hadi lini.
 
Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.

Sasa kwa nini wamefanya mabadiliko ya kumu accomodate Sefu bila kuihusisha katiba ya muungano? ina maana CHADEMA walikuwa sahihi kumkatalia Sefu kuingia Bungeni?
 
Katiba imepitwa na wakati sana, ndiyo maana migogoro yatokanayo na katiba haitakwisha. Mfano mzuri ni ule wa kuweka diesel kwenye gari la petrol. Itafika wakati engine ita seize tu. Kwa mfano, katiba inasema Tanzania ni nchi inayofuata demokrasia ya vyama vingi, wakati hali halisi ni ya chama kimoja. Inasema serikali ni nchi ya kijamaa, wakati si ya kijamaa. Inasema serikali haina dini, wakati watu wengine wamekomalia serikali ianzishe mahakama ya kadhi etc. etc. Kuna haja ya kuwa na katiba mpya ambapo mambo haya yatajadiliwa na kuwekwa kwenye katiba jinsi ipasavyo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom