Tuhuma za wizi wa kura ni nzito sana, zijibiwe kwa tafakuri ya kina

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Wimbi la tuhuma za wizi wa kura katika chaguzi mbalimbali nchini limetanda zaidi ya miongo miwili, sasa.

Tuhuma hizi ni nzito sana,tena zina hitaji tafakuri na majibu ya kina kuliko vitisho.

Tume ya uchaguzi imekuwa ikituhumiwa kama mhusika mkuu kwa kushirikiana na CCM, lakini majibu ya tuhuma hizi zinajibiwa kiwepesi kuliko tuhuma zenyewe.

Unapoiba kura za wananchi, umeiba demokrasia. Umeiba uhuru wa wananchi kumchagua kiongozi wamtakaye, lakini pia una vuruga uvumilivu wa wapiga kura kwa kuwanyang'anya haki yao ya kuchagua wamtakaye kwa mujibu wa sheria.

Uwizi ni maandalizi kwa maana ya connection, viashiria vya wizi vimeanza kuonekana wazi, tusipo chukua tahadhari tunaingiza Taifa kwenye majanga makubwa.

Bahati mbaya sana anayelalamika mara kwa mara kuibiwa amegoma safari hii kuibiwa tena na tena, akisema sasa basi inatosha. Maanake nini, hatokubali ghiliba,upendeleo, vitisho na kila aina ya dhuluma inayo fanywa kutengeneza mazingira ya wizi wa KURA.

Tume ya uchaguzi iliyo teuliwa na Mwenyekiti wa CCM, kwa kuwateua makada wenzake kwa mwamvuli wa urais kusimamia uchaguzi ambao yeye anagombea ni zaidi ya mbinu chafu za wazi zenye malengo ya kulazimisha ushindi.

Mkurugenzi wa uchaguzi, ambaye ndiye msimamizi mkuu wa uchaguzi ni kada wa CCM kama video clip iliyo trend kwenye mitandao ya kijamii inavyo jieleza, kuteuliwa kusimamia uchaguzi wa ushindani dhidi ya mtu aliye mteua ni kuto kuwatendea haki wagombea wengine na kuufanya uchaguzi kuwa wa kimkakati na mbinu chafu dhidi ya demokrasia inayo heshimu uhuru wa watu kuwachagua viongozi wawatakao.

Kulazimisha tume kuendelea kuteuliwa na rais mgombea, bila kuidhinishwa na bunge na tena bila kuwa na makamishana wa uchaguzi kutoka vyama vingine ni maandalizi rasmi ya ubakaji wa demokrasia nchini.

Tume kuwa biased kwa kushindwa kukemea makosa ya wazi yanayofanywa na mgombea urais wa CCM kwa mwamvuli wa urais, akipingana na sheria na kanuni za uchaguzi bila kukemewa na tume hiyo, lakini wapinzani wakitishiwa kwa taharuki ya kuzuia mianya ya wizi wa kura ni zaidi ya UDIKITEKTA unapaswa kupigiwa kelele kwa nguvu zote na waumini wa demokrasia nchini.

Kuzuiwa kwa matokeo ya urais kuhojiwa wala kuthibitishwa mahakamani, kinyume na matokeo ya ubunge na madiwani, hii ni maandalizi ya kuibadili sovereign state kuwa monarchy state, lakini pia inatoa mianya ya uporaji matokeo usihojiwe na mamlaka yeyote ile.

Ili viashiria hivi na tuhuma hizi zipatiwe majibu ya kina, tume inapaswa kuacha upendeleo wowote ule kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Sheria ichukue mkondo wake ili dhana nzima ya uchaguzi wa kidemokrasia iwe na tija.

Haitoshi kuvikemea vyama mbadala kwa kauli zao za kukataa kuibiwa kura, huku ukifumbia kanuni na sheria za uchaguzi zikivunjwa makusudi na CCM, kwa kuwa ndicho chama kinachoongoza serikali.

Sheria na kanuni za uchaguzi zinakataza rushwa, lakini mgombea urais wa CCM anatumia influence ya madaraka yake kukiuka sheria hiyo kwa kuagiza utekelezaji wa ahadi zake kwa mgongo wa urais kinyume na sheria ya uchaguzi.

Wakati sheria hiyo ina tafsiri utekelezaji wa maamuzi yeyote kwa mgongo wa madaraka uliyo nayo ukaagiza yafanyike kipindi hiki kwenye jukwaa la kampeni ni rushwa, lakini tume ya uchaguzi imeendelea kufumbia macho ukaidi huu wa makusudi unaofanywa na mgombea wa CCM.

Pamoja na mbeleko hii kwa kutumia dola vyama mbadala vimetoa angalizo,kuwa hiyo tarehe 28 October, havita kubali matokeo yeyote yenye sura ya wizi wa Kura.

Vile vile tume inapaswa kujua kuwa nchi hii ni yetu sote, heshima hujengwa kwa mkubwa na mdogo, vitisho havisaidi au kukuza demokrasia, uchaguzi huu ni baina ya watanzania kwa watanzania, tume isimamie maamuzi ya haki tu, vinginevyo Taifa linakwenda kuangamia kwa kukosa maarifa.
 
Umeandika kweli tupu..Nchi iliyojaa watu wasomi kwl kwl. Ni aibu kuikibali Tume hii,tume iliyojaa sio wataalam tu Bali iliyojaa watu walioteuliwa na wanasiasa wale wale walioshika dola..haiwezekani kabsa eti uchaguz ukawa na fair ground haiwezekani.

Inasikitisha kukuta eti kiongozi wa uchaguzi mchana kweupe kukikimbia wajibu wake wa kupokea form za wagombea. Eti kweli tuseme sisi na wao watuaminishe uchaguz ni wa haki katika misingi hii huku wakiwa nyuma ya dolali ambayo wananchi ndy kodi zao znawalpa mishahara na stahiki zao. Huu ni ujuha wa wazi wazi kabsa.

Inashangaza kuona wasomi wa sheria wakiwa kimya kwny sarakasi za kikundi cha watu katka nchi yetu. Wakiharibu umoja wetu ,ushirkiano wetu na undugu wetu uliodumu kwa miaka mingi sana.

Inashangaza wananchi kwa umoja wao wakiwa kimya katika mchezo hii ambayo inauaa mamlaka ya wananchi kuchagua ama kuweka mamlaka ya wananchi.

Wananchi tuseme mambo haya ya fedheha sana sasa basi. Mana yanaangamiza utu wetu. Vyombo vyote na taasisi zenye watu makini vikemee kweli na sio kujificha hapana Bali vitoke hadharani kukemea hali hii katka chaguzi zetu.

Tanzania ni yetu sote na si ya Kikundi cha watu. Wachache wanaotupeleka kusiko tuwpinge.
MUNGU BARIKI TANZANIA MPYA ITAKAYOJALI UTU WETU. AMENI!!!
 
Ukiona kura zimeibiwa ujue wakala wa Chama chako amehusika kwa asilimia kubwa. Kura zinahesabiwa kituoni mbele ya Mawakala wa vyama vyote wakimaliza kuhesabu wana sain kwenye kwenye fomu alafu matokeo yanabandikwa ukutani Mawakala wanapewa kopi ya matokeo.
 
Wimbi la tuhuma za wizi wa kura katika chaguzi mbalimbali nchini limetanda zaidi ya miongo miwili, sasa.

Tuhuma hizi ni nzito sana,tena zina hitaji tafakuri na majibu ya kina kuliko vitisho.

Tume ya uchaguzi imekuwa ikituhumiwa kama mhusika mkuu kwa kushirikiana na CCM, lakini majibu ya tuhuma hizi zinajibiwa kiwepesi kuliko tuhuma zenyewe.

Unapoiba kura za wananchi, umeiba demokrasia. Umeiba uhuru wa wananchi kumchagua kiongozi wamtakaye, lakini pia una vuruga uvumilivu wa wapiga kura kwa kuwanyang'anya haki yao ya kuchagua wamtakaye kwa mujibu wa sheria.

Uwizi ni maandalizi kwa maana ya connection, viashiria vya wizi vimeanza kuonekana wazi, tusipo chukua tahadhari tunaingiza Taifa kwenye majanga makubwa.

Bahati mbaya sana anayelalamika mara kwa mara kuibiwa amegoma safari hii kuibiwa tena na tena, akisema sasa basi inatosha. Maanake nini, hatokubali ghiliba,upendeleo, vitisho na kila aina ya dhuluma inayo fanywa kutengeneza mazingira ya wizi wa KURA.

Tume ya uchaguzi iliyo teuliwa na Mwenyekiti wa CCM, kwa kuwateua makada wenzake kwa mwamvuli wa urais kusimamia uchaguzi ambao yeye anagombea ni zaidi ya mbinu chafu za wazi zenye malengo ya kulazimisha ushindi.

Mkurugenzi wa uchaguzi, ambaye ndiye msimamizi mkuu wa uchaguzi ni kada wa CCM kama video clip iliyo trend kwenye mitandao ya kijamii inavyo jieleza, kuteuliwa kusimamia uchaguzi wa ushindani dhidi ya mtu aliye mteua ni kuto kuwatendea haki wagombea wengine na kuufanya uchaguzi kuwa wa kimkakati na mbinu chafu dhidi ya demokrasia inayo heshimu uhuru wa watu kuwachagua viongozi wawatakao.

Kulazimisha tume kuendelea kuteuliwa na rais mgombea, bila kuidhinishwa na bunge na tena bila kuwa na makamishana wa uchaguzi kutoka vyama vingine ni maandalizi rasmi ya ubakaji wa demokrasia nchini.

Tume kuwa biased kwa kushindwa kukemea makosa ya wazi yanayofanywa na mgombea urais wa CCM kwa mwamvuli wa urais, akipingana na sheria na kanuni za uchaguzi bila kukemewa na tume hiyo, lakini wapinzani wakitishiwa kwa taharuki ya kuzuia mianya ya wizi wa kura ni zaidi ya UDIKITEKTA unapaswa kupigiwa kelele kwa nguvu zote na waumini wa demokrasia nchini.

Kuzuiwa kwa matokeo ya urais kuhojiwa wala kuthibitishwa mahakamani, kinyume na matokeo ya ubunge na madiwani, hii ni maandalizi ya kuibadili sovereign state kuwa monarchy state, lakini pia inatoa mianya ya uporaji matokeo usihojiwe na mamlaka yeyote ile.

Ili viashiria hivi na tuhuma hizi zipatiwe majibu ya kina, tume inapaswa kuacha upendeleo wowote ule kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Sheria ichukue mkondo wake ili dhana nzima ya uchaguzi wa kidemokrasia iwe na tija.

Haitoshi kuvikemea vyama mbadala kwa kauli zao za kukataa kuibiwa kura, huku ukifumbia kanuni na sheria za uchaguzi zikivunjwa makusudi na CCM, kwa kuwa ndicho chama kinachoongoza serikali.

Sheria na kanuni za uchaguzi zinakataza rushwa, lakini mgombea urais wa CCM anatumia influence ya madaraka yake kukiuka sheria hiyo kwa kuagiza utekelezaji wa ahadi zake kwa mgongo wa urais kinyume na sheria ya uchaguzi.

Wakati sheria hiyo ina tafsiri utekelezaji wa maamuzi yeyote kwa mgongo wa madaraka uliyo nayo ukaagiza yafanyike kipindi hiki kwenye jukwaa la kampeni ni rushwa, lakini tume ya uchaguzi imeendelea kufumbia macho ukaidi huu wa makusudi unaofanywa na mgombea wa CCM.

Pamoja na mbeleko hii kwa kutumia dola vyama mbadala vimetoa angalizo,kuwa hiyo tarehe 28 October, havita kubali matokeo yeyote yenye sura ya wizi wa Kura.

Vile vile tume inapaswa kujua kuwa nchi hii ni yetu sote, heshima hujengwa kwa mkubwa na mdogo, vitisho havisaidi au kukuza demokrasia, uchaguzi huu ni baina ya watanzania kwa watanzania, tume isimamie maamuzi ya haki tu, vinginevyo Taifa linakwenda kuangamia kwa kukosa maarifa.
Bila bao la mkono ccm ilishashindwa tangu 1995.
 
Tume ni ccm umeona wanavyoenguwa wanachadema kwenye nafasi za ubunge na udiwani ni kwa sababu ya ukada tu
 
ccm haijawahi kushinda uchaguzi wanategemea mbereko ya nec wateule wa rais....

Nikuteue mimi nikulipe mshahara mzuri na kukupa gari alafu umtangaze mpinzani kuwa ameshinda....? MWISHO WA KUNUKUU
 
Ukiona kura zimeibiwa ujue wakala wa Chama chako amehusika kwa asilimia kubwa. Kura zinahesabiwa kituoni mbele ya Mawakala wa vyama vyote wakimaliza kuhesabu wana sain kwenye kwenye fomu alafu matokeo yanabandikwa ukutani Mawakala wanapewa kopi ya matokeo.

Siyo kweli hivi hao wasimamizi walioengua wagombea waupinzani kulikuwa na wakala hapo na Rais alipotangazia umma wa watanzania kuwa atamshangaa msimamizi wa uchaguzi atakayemtangaza mpinzani kuwa mshindi wakati yeye ndiye amemteua na kumpa gari zuri na mshahara alikuwa na maana gani kuifanya tume iwe huru. Haya ni mambo ya hovyo kabisa katika nchi ya kidemokrasia. Hata mtu unapotetea unakosa uzalendo kwa nchi yako
 
Ukiona kura zimeibiwa ujue wakala wa Chama chako amehusika kwa asilimia kubwa. Kura zinahesabiwa kituoni mbele ya Mawakala wa vyama vyote wakimaliza kuhesabu wana sain kwenye kwenye fomu alafu matokeo yanabandikwa ukutani Mawakala wanapewa kopi ya matokeo.

Hivyo ndio inavyotakiwa kwa mujibu wa sheria, lakini toka Magufuli ameingia imekuwa ni kinyume kabisa. Tumeshuhudia kwenye chaguzi za marudio mawakala wa upinzani wakipigwa, tena na polisi ili wasaini fomu fake za matokeo.
 
Samahani lakini, huwa najiuliza ikiwa Tume sio Huru na Haki, au inaiba kura, mbona maeneo mengine Wapinzani huwa Wanashinda? Kwa nini?

Nitatajie sehemu ambayo wapinzani wamewahi kushinda toka Magufuli ameingia madarakani. Ukisikia mama wa kambo anamyima mtoto wa kambo chakula, haimaanishi kuwa hampi kabisa maana atakufa, lakini huwa anampa kidogo ili asife na aendelee kumtesa. Ili mpinzani atangazwe inabidi wananchi wajitoe muhanga.
 
Ukiona kura zimeibiwa ujue wakala wa Chama chako amehusika kwa asilimia kubwa. Kura zinahesabiwa kituoni mbele ya Mawakala wa vyama vyote wakimaliza kuhesabu wana sain kwenye kwenye fomu alafu matokeo yanabandikwa ukutani Mawakala wanapewa kopi ya matokeo.
Na kauli - Mkurugenzi namlipa mshahara amtangaze mpinzani limekaaje na tangu ameingia Madaraka ni wapi mpinzani ametangazwa kurudisha fomu tu shida
 
Nitatajie sehemu ambayo wapinzani wamewahi kushinda toka Magufuli ameingia madarakani. Ukisikia mama wa kambo anamyima mtoto wa kambo chakula, haimaanishi kuwa hampi kabisa maana atakufa, lakini huwa anampa kidogo ili asife na aendelee kumtesa. Ili mpinzani atangazwe inabidi wananchi wajitoe muhanga.
2015 ndio kaingia lakini kilio cha wizi wa kura na tume huru hakijaanza leo kwa Wapinzani, kama ni kupewa japo kidogo basi si tume ingeangalia nani wa kumpa na nani wa kumnyima, mfano kuna Wapinzani ambao ni machachari na wanaibana sana serikali, kwa nini tume isiyohuru isingewatoa hao na kuwapoza Wapinzani kwa kuwaweka watu ambao sio machachari sana kama kina Zitto, Lema, Mdee na wengine? Na kama huwa inabidi mpaka wananchi walinde kura ndio wabunge wa upinzani watangazwe kwa nini huko kwingine pia wasilinde kura kama ambavyo maeneo mengine wanafanya?
 
2015 ndio kaingia lakini kilio cha wizi wa kura na tume huru hakijaanza leo kwa Wapinzani, kama ni kupewa japo kidogo basi si tume ingeangalia nani wa kumpa na nani wa kumnyima, mfano kuna Wapinzani ambao ni machachari na wanaibana sana serikali, kwa nini tume isiyohuru isingewatoa hao na kuwapoza Wapinzani kwa kuwaweka watu ambao sio machachari sana kama kina Zitto, Lema, Mdee na wengine? Na kama huwa inabidi mpaka wananchi walinde kura ndio wabunge wa upinzani watangazwe kwa nini huko kwingine pia wasilinde kura kama ambavyo maeneo mengine wanafanya?

Sio kila mtu anaweza kulinda haki yake kwa kuhatarisha maisha yake. Na ni kwanini mtu ahatarishe usalama kwa ajili ya uchaguzi? Huo ndio utaratibu wa kupata viongozi? Hebu kaa kimya ww muhuni maana huna hoja.
 
Yule mkurugenzi wa NEC hatakiwi kusikilizwa kwa lolote. Imedhihirika pasipo wazi kuwa ni kada wa CCM ambaye yupo kwa madlahibya CCM.

Vyama vya upinzani viangalie tu sheria na siyo zile kanuni za kijinga zinazotangazwa na NEC.

Mwaka huu hakuna upuuzi eti piga kura nenda nyumbani bali ni:

PIGA KURA, BAKI KITUONI, SHUHUDIA KURA ZINAVYOHESABIWA NA KUTANGAZWA. UMEJITIDHISHA KILA KITI KIMEENDA SAWA, NENDA NYUMBANI. UMEJIRIDHISHA PASIPO SHAKA KUNA WIZI, UDANGANYIFU AU KUTOTANGAZWA MSHINDI, YEYOTE ALIYEFANYA HIVYO AWAJIBISHWE HAPO HAPO NA UMMA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kila mtu anaweza kulinda haki yake kwa kuhatarisha maisha yake. Na ni kwanini mtu ahatarishe usalama kwa ajili ya uchaguzi? Huo ndio utaratibu wa kupata viongozi? Hebu kaa kimya ww muhuni maana huna hoja.
Usipanick basi mkuu, si tunaelimishana tu? Suluhisho ni katiba mpya na si kingine kwa sasa
 
Back
Top Bottom