Malisa Godlisten
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 201
- 1,534
Kuna habari inasambaa kwenye mitandao ya kijamii ikieleza kuwa mimi (Malisa), viongozi wa kitaifa wa Chadema na mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi tumekula njama (conspirancy) za kufanya upotoshaji kuhusu suala la mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini.
Baadhi ya viongozi waliotajwa kwenye andiko hilo ni Mhe.Freeman Mbowe (M/kiti taifa), Mhe.Vincent Mashinji (Katibu Mkuu), Ndg.Patrobas Katambi (M/kiti BAVICHA) na Ndg.Ben Saanane (Afisa wa chama). Mwandishi wa mwananchi ametajwa kwa jina la Tausi Mbowe.
Habari hiyo inadai mimi na mwandishi aitwae Tausi Mbowe tulikaa ofisi za Mwananchi na tukaandika taarifa potofu dhidi ya suala la utoaji wa mikopo ya elimu ya juu, kwa kushirikiana na viongozi wa juu wa Chadema. Taarifa hiyo inaongeza kuwa Computer iliyotumika ni ya kwangu.
[HASHTAG]#UKWELI[/HASHTAG]:
1. Simfahamu mwandishi wa Mwananchi aitwaye Tausi Mbowe. Mimi na yeye hatufahamiani na hatujawahi kuonana.
2. Sijafanya mawasiliano yoyote (ama ya simu, barua pepe, au ya ana kwa ana) na viongozi wangu wakuu wa chama kuhusiana na suala la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
3. Tarehe inayotajwa katika andiko hilo sikuwepo ofisi za gazeti la Mwananchi.
4. Wiki hii yote sikuwepo Dar es Salaam (nimekua Kahama, Geita, Ngara na Tabora kwa nyakati tofauti).
5. Computer yangu haijawahi kutumiwa na Tausi Mbowe wala mwandishi mwingine yeyote wa Mwananchi kwa shughuli za kikazi au binafsi.
Naomba umma wa watanzania uelewe kuwa habari hiyo ni ya uongo, ya kutunga na yenye nia ya ovu (malice aforethought), iliyoandikwa kwa malengo yafuatayo:
1. Kuwaondoa watu kwenye mjadala juu ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
2. Kumgombanisha mwandishi wa Mwananchi Tausi Mbowe na Mwajiri wake (ili ionekane anatumika kisiasa kinyume na maadili yake ya kazi).
3. Kugombanisha uongozi wa juu wa Chadema na gazeti la Mwananchi.
4. Kupunguza imani ya watanzania dhidi ya gazeti makini la Mwananchi, na kuwaaminisha uongo kuwa gazeti hilo linatumika kisiasa.
5. Kujenga chuki dhidi ya Chadema na viongozi wake wakuu.
Hivyo basi naomba taarifa hiyo ipuuzwe maana haina ukweli wowote. Tafadhali wajulishe na wengine.
NB: Serikali itoe fedha za mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na iache kutafuta visingizio visivyo na tija. Nguvu zinazotumika kutunga uongo dhidi yetu, zingetumika tutafuta fedha za mikopo kwa wanafunzi waliokosa.
Malisa GJ
Baadhi ya viongozi waliotajwa kwenye andiko hilo ni Mhe.Freeman Mbowe (M/kiti taifa), Mhe.Vincent Mashinji (Katibu Mkuu), Ndg.Patrobas Katambi (M/kiti BAVICHA) na Ndg.Ben Saanane (Afisa wa chama). Mwandishi wa mwananchi ametajwa kwa jina la Tausi Mbowe.
Habari hiyo inadai mimi na mwandishi aitwae Tausi Mbowe tulikaa ofisi za Mwananchi na tukaandika taarifa potofu dhidi ya suala la utoaji wa mikopo ya elimu ya juu, kwa kushirikiana na viongozi wa juu wa Chadema. Taarifa hiyo inaongeza kuwa Computer iliyotumika ni ya kwangu.
[HASHTAG]#UKWELI[/HASHTAG]:
1. Simfahamu mwandishi wa Mwananchi aitwaye Tausi Mbowe. Mimi na yeye hatufahamiani na hatujawahi kuonana.
2. Sijafanya mawasiliano yoyote (ama ya simu, barua pepe, au ya ana kwa ana) na viongozi wangu wakuu wa chama kuhusiana na suala la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
3. Tarehe inayotajwa katika andiko hilo sikuwepo ofisi za gazeti la Mwananchi.
4. Wiki hii yote sikuwepo Dar es Salaam (nimekua Kahama, Geita, Ngara na Tabora kwa nyakati tofauti).
5. Computer yangu haijawahi kutumiwa na Tausi Mbowe wala mwandishi mwingine yeyote wa Mwananchi kwa shughuli za kikazi au binafsi.
Naomba umma wa watanzania uelewe kuwa habari hiyo ni ya uongo, ya kutunga na yenye nia ya ovu (malice aforethought), iliyoandikwa kwa malengo yafuatayo:
1. Kuwaondoa watu kwenye mjadala juu ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.
2. Kumgombanisha mwandishi wa Mwananchi Tausi Mbowe na Mwajiri wake (ili ionekane anatumika kisiasa kinyume na maadili yake ya kazi).
3. Kugombanisha uongozi wa juu wa Chadema na gazeti la Mwananchi.
4. Kupunguza imani ya watanzania dhidi ya gazeti makini la Mwananchi, na kuwaaminisha uongo kuwa gazeti hilo linatumika kisiasa.
5. Kujenga chuki dhidi ya Chadema na viongozi wake wakuu.
Hivyo basi naomba taarifa hiyo ipuuzwe maana haina ukweli wowote. Tafadhali wajulishe na wengine.
NB: Serikali itoe fedha za mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na iache kutafuta visingizio visivyo na tija. Nguvu zinazotumika kutunga uongo dhidi yetu, zingetumika tutafuta fedha za mikopo kwa wanafunzi waliokosa.
Malisa GJ