Mleta amani
Member
- Dec 6, 2019
- 25
- 117
Naandika malalamiko haya nikiwa ni mmoja wa wahanga wa hili.
Mimi ni daktari ambae nimemaliza mazoezi ya vitendo "internship" katika hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (Mbeya Zonal Referral Hospital).
Madaktari bingwa kutoka baadhi ya idara katika hospitali hii wamekua na tabia chafu ya kudai na kulazimisha rushwa ya ngono kutoka kwa madaktari wa kike wanaofanya mazoezi ya vitendo hospitalini hapo, ili waweze kuwapasisha wanapopita idarani kwao, na unapokataa kukubaliana nao, kinachofuata ni kufanya maisha yako kuwa magumu idarani kwao na hata saa zingine kukupa alama za kukufelisha.
Wanaofanya tabia hizi ni hawa wafuatao;
1.(Jina limehifadhiwa) wa idara ya medicine-Huyu binafsi alining'ang'aniza sana nimpe rushwa ya ngono, na alinihakikishia kuwa nisipompa penzi, alinihakikishia kuwa atanipa alama ya D kwenye idara yake.
Huyu daktari ni mshenzi sana na alifikia hatua ya kunifanyia sexual harrassment ofisini kwake kwa kunishika maeneo ya mwili wangu, lakini nilifanikiwa kumkimbia. Huyu daktari hii ni tabia yake, kwani kumekuwa na malalamiko ya aina hii juu yake hata kutoka kwa wanafunzi wa Chuo cha UDSM wa Medicine ambao hufanyia mazoezi ya vitendo hospitali hii.
2. (Jina limehifadhiwa) wa idara ya Upasuaji: Huyu amekuwa akiomba rushwa ya ngono na hata kufikia kulazimisha na kuwapa 'alama chafu' wale ambao wanamkatalia ushenzi wake huo.
3.(Jina limehifadhiwa) wa Idara ya Mifupa (Orthopedics): Huyu ni kinara mwingine wa kulazimisha rushwa ya ngono kwa interns wanaopita idarani kwake na aliwahi kusikika akisema kuwa idarani kwake bila kutoa uchi mtoto wa kike hawezi kukupa alama nzuri.
4.(Jina limehifadhiwa) wa medical: Huyu pia huwa anashirikiana mwenzake katika kuwanyanyasa kingono interns wanaopita idarani kwake, yeye mara nyingi hupenda kuita interns wa kike ofisini kwake na kuwafanyia sexual harrassment kwa kuanza kuwashika maungo yao huku akitumia maneno ya kutishia kwamba wakiripoti basi wasahau kupata alama nzuri idara ya medical.
Pamoja na hayo, mkurugenzi wa hospitali hii amekuwa akifumbia macho tuhuma hizi, hata watu wakilalamika vipi, kazi yake ni kuwatetea tu hawa madaktari wake bingwa, badala ya kufanya uchunguzi wa ndani na huru juu ya tuhuma hizi, yeye ndiye amekua akiwakingia kifua madaktari hawa wahuni na washenzi wa tabia, na hivyo hata wakiwa wanafanya ushenzi wao, wengine huwaambia kabisa wahanga kwamba huna pa kukimbilia hivyo ni bora tu ukubaliane na mimi.
Naomba sana Serikali kupitia wizara ya Afya ifanyie kazi tuhuma hizi kwa kufanya uchunguzi wa wazi na huru, kwani hawa madaktari wana nguvu sana kutokana na nafasi zao, ni rahisi kuingilia taratibu za uchunguzi.
========
Moderator: Haya malalamiko, Uongozi wa JamiiForums umeyafikisha kwenye Mamlaka ya Serikali. Habari njema ni kwamba yameshaanza kufanyiwa kazi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU).
Tutazidi kutoa mrejesho kwa kila hatua inayofikiwa.
Tuendelee kutoa taarifa za rushwa ya ngono popote nchini kupitia hii thread hapa chini, nasi tutazifikisha na kufuatilia katika Mamlaka husika.
Soma pia: JamiiTalks - Tutumie taarifa za Rushwa ya Ngono na Unyanyasaji sehemu ulipo, ili Mamlaka za Serikali zizifanyie kazi
Mimi ni daktari ambae nimemaliza mazoezi ya vitendo "internship" katika hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (Mbeya Zonal Referral Hospital).
Madaktari bingwa kutoka baadhi ya idara katika hospitali hii wamekua na tabia chafu ya kudai na kulazimisha rushwa ya ngono kutoka kwa madaktari wa kike wanaofanya mazoezi ya vitendo hospitalini hapo, ili waweze kuwapasisha wanapopita idarani kwao, na unapokataa kukubaliana nao, kinachofuata ni kufanya maisha yako kuwa magumu idarani kwao na hata saa zingine kukupa alama za kukufelisha.
Wanaofanya tabia hizi ni hawa wafuatao;
1.(Jina limehifadhiwa) wa idara ya medicine-Huyu binafsi alining'ang'aniza sana nimpe rushwa ya ngono, na alinihakikishia kuwa nisipompa penzi, alinihakikishia kuwa atanipa alama ya D kwenye idara yake.
Huyu daktari ni mshenzi sana na alifikia hatua ya kunifanyia sexual harrassment ofisini kwake kwa kunishika maeneo ya mwili wangu, lakini nilifanikiwa kumkimbia. Huyu daktari hii ni tabia yake, kwani kumekuwa na malalamiko ya aina hii juu yake hata kutoka kwa wanafunzi wa Chuo cha UDSM wa Medicine ambao hufanyia mazoezi ya vitendo hospitali hii.
2. (Jina limehifadhiwa) wa idara ya Upasuaji: Huyu amekuwa akiomba rushwa ya ngono na hata kufikia kulazimisha na kuwapa 'alama chafu' wale ambao wanamkatalia ushenzi wake huo.
3.(Jina limehifadhiwa) wa Idara ya Mifupa (Orthopedics): Huyu ni kinara mwingine wa kulazimisha rushwa ya ngono kwa interns wanaopita idarani kwake na aliwahi kusikika akisema kuwa idarani kwake bila kutoa uchi mtoto wa kike hawezi kukupa alama nzuri.
4.(Jina limehifadhiwa) wa medical: Huyu pia huwa anashirikiana mwenzake katika kuwanyanyasa kingono interns wanaopita idarani kwake, yeye mara nyingi hupenda kuita interns wa kike ofisini kwake na kuwafanyia sexual harrassment kwa kuanza kuwashika maungo yao huku akitumia maneno ya kutishia kwamba wakiripoti basi wasahau kupata alama nzuri idara ya medical.
Pamoja na hayo, mkurugenzi wa hospitali hii amekuwa akifumbia macho tuhuma hizi, hata watu wakilalamika vipi, kazi yake ni kuwatetea tu hawa madaktari wake bingwa, badala ya kufanya uchunguzi wa ndani na huru juu ya tuhuma hizi, yeye ndiye amekua akiwakingia kifua madaktari hawa wahuni na washenzi wa tabia, na hivyo hata wakiwa wanafanya ushenzi wao, wengine huwaambia kabisa wahanga kwamba huna pa kukimbilia hivyo ni bora tu ukubaliane na mimi.
Naomba sana Serikali kupitia wizara ya Afya ifanyie kazi tuhuma hizi kwa kufanya uchunguzi wa wazi na huru, kwani hawa madaktari wana nguvu sana kutokana na nafasi zao, ni rahisi kuingilia taratibu za uchunguzi.
========
Moderator: Haya malalamiko, Uongozi wa JamiiForums umeyafikisha kwenye Mamlaka ya Serikali. Habari njema ni kwamba yameshaanza kufanyiwa kazi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU).
Tutazidi kutoa mrejesho kwa kila hatua inayofikiwa.
Tuendelee kutoa taarifa za rushwa ya ngono popote nchini kupitia hii thread hapa chini, nasi tutazifikisha na kufuatilia katika Mamlaka husika.
Soma pia: JamiiTalks - Tutumie taarifa za Rushwa ya Ngono na Unyanyasaji sehemu ulipo, ili Mamlaka za Serikali zizifanyie kazi