Tuhuma za mauaji: Nimehojiwa na Polisi, nimetimiza wajibu wangu

Ndugu wana JF na watanzania kwa ujumla,

Nachukua fursa hii kuwashukuru wote mlioguswa kusikia nimeitwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano baada ya magazeti mawili leo kunihusisha na linalodaiwa kuwa ‘Genge la Watu wanaopanga mikakati ya kumuua Cyprian Musiba”.

Genge hili lilihusisha wanasiasa, taasisi za serikali, watu binafsi (nikiwemo mimi) na hadi viongozi wa Taasisi za Serikali.

Si mara ya kwanza magazeti haya kufanya hivi kwangu na kwa watu wengi (ingawa kwangu imekuwa ikirudiwa kwa angle tofauti tofauti).

Naam, niliitwa saa 3 asubuhi (ingawa habari yenyewe ilitoka siku hiyo hiyo) na nikaambiwa nijitahidi niwe nimefika kabla ya saa 5; nikajitahidi kuitikia wito na kufika mnamo saa 4 na dk 30 asubuhi pale Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.

Nikiri, jopo la wachunguzi wa Jeshi la Polisi walioshiriki kwenye mahojiano nami walionyesha weledi katika kazi yao na hivyo kupelekea mimi na mwanasheria wangu kutoa maelezo yaliyohitajika katika sakata hili.

Nilihoji maswali ya msingi juu ya tuhuma ambazo zimekuwa zikitolewa na bwana huyu na nikahoji kinachopelekea mara zote vyombo vya dola kumwacha aendelee kuumiza watu. Aidha, nikiri pia kuwa maswali yote niliyouliza yalijibiwa kwa staha na undani wa mahojiano yetu nachelea kuuweka bayana kwani naweza kuvuruga uchunguzi.

Niseme: Nawashukuruni nyote mlioguswa na kunitafuta kwa njia mbalimbali kunitia moyo au kutaka kujua mnaweza kusaidiaje. Wengine mlijitoa kuwa tayari kwa dhamana kama ingehitajika, kitendo kilichonifariji kuwa watu wanaelewa tunasimamia nini na kwanini tunaendelea kukisimamia.

Kwa watanzania: Watu kama ndugu huyu wapo, tuzikatae kazi zao na wanaowatuma kwa nguvu zote; tusikubali kuletewa migawanyo inayokwepeka. Tuwakemee pale tunapoweza lakini tukibaini kuwa wana nguvu ya ziada, tumwombe Mungu akatende muujiza wake!

Once again, asanteni sana na Mungu asimame nasi katika kuijenga nchi yetu, Tanzania.

Maxence
pole sana Melo
 
Ndugu wana JF na watanzania kwa ujumla,

Nachukua fursa hii kuwashukuru wote mlioguswa kusikia nimeitwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano baada ya magazeti mawili leo kunihusisha na linalodaiwa kuwa ‘Genge la Watu wanaopanga mikakati ya kumuua Cyprian Musiba”.

Genge hili lilihusisha wanasiasa, taasisi za serikali, watu binafsi (nikiwemo mimi) na hadi viongozi wa Taasisi za Serikali.

Si mara ya kwanza magazeti haya kufanya hivi kwangu na kwa watu wengi (ingawa kwangu imekuwa ikirudiwa kwa angle tofauti tofauti).

Naam, niliitwa saa 3 asubuhi (ingawa habari yenyewe ilitoka siku hiyo hiyo) na nikaambiwa nijitahidi niwe nimefika kabla ya saa 5; nikajitahidi kuitikia wito na kufika mnamo saa 4 na dk 30 asubuhi pale Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.

Nikiri, jopo la wachunguzi wa Jeshi la Polisi walioshiriki kwenye mahojiano nami walionyesha weledi katika kazi yao na hivyo kupelekea mimi na mwanasheria wangu kutoa maelezo yaliyohitajika katika sakata hili.

Nilihoji maswali ya msingi juu ya tuhuma ambazo zimekuwa zikitolewa na bwana huyu na nikahoji kinachopelekea mara zote vyombo vya dola kumwacha aendelee kuumiza watu. Aidha, nikiri pia kuwa maswali yote niliyouliza yalijibiwa kwa staha na undani wa mahojiano yetu nachelea kuuweka bayana kwani naweza kuvuruga uchunguzi.

Niseme: Nawashukuruni nyote mlioguswa na kunitafuta kwa njia mbalimbali kunitia moyo au kutaka kujua mnaweza kusaidiaje. Wengine mlijitoa kuwa tayari kwa dhamana kama ingehitajika, kitendo kilichonifariji kuwa watu wanaelewa tunasimamia nini na kwanini tunaendelea kukisimamia.

Kwa watanzania: Watu kama ndugu huyu wapo, tuzikatae kazi zao na wanaowatuma kwa nguvu zote; tusikubali kuletewa migawanyo inayokwepeka. Tuwakemee pale tunapoweza lakini tukibaini kuwa wana nguvu ya ziada, tumwombe Mungu akatende muujiza wake!

Once again, asanteni sana na Mungu asimame nasi katika kuijenga nchi yetu, Tanzania.

Maxence
Pole sana Maxence...ni mapito tu na iko siku unafiki wa watu kama akina Msiba na genge lao utakufa in a natural death...!
 
Mimi naamini Musiba ana nguvu kubwa iliyo nyuma yake ila wajue tu hakuna nguvu kubwa ya kumzidi Mungu(Muumba).
 
Musiba kwanini anaruhusiwa kufanya haya?
Je kwa namna hii tunajenga Taifa gani?
Sidhani Kama Magufuli atastaafu nao wanaojipendekeza kwake,
Sina Hakika saana kama Polisi walipaswa kukuhoji wewe, maana nao ni watuhumiwa kama wewe kwa mjibu wa taarifa za Musiba,

Ningekuwa mimi ndo Mello Maelezo yangu yangekaa hivi,,
Ninaotuhumiwa kushirikiana nao kufanya njama kumuua Musiba wamenihoji,
Yaan nimemaliza maojiano na watuhumiwa wenzagu kwenye njama za kumuua Musiba"
Britannica

Hivi walikuwa wanamuhoji au walikuwa wanajadiliana? Inawezekanaje mtuhumiwa akamuhoji mtuhumiwa mwenzake wa tuhuma hiyo hiyo inayowakabili wote. Mimi nadhani walikuwa na kikao cha kujadili tuhuma yao. Kwasababu walio muhoji nao walipaswa wahojiwe. Labda iundwe tume huru kuwa hoji watuhumiwa ila sio polisi kwasababu nao ni watumiwa.
 
Haaaaaaa umenifurahisha namna unavyoutumia uhuru wako usikuwa na mipaka vizuri, lakin sijui kwa nini hutaki MSIBA atumie uhuru wake vizuri kama ulivyoutumia hapa tindo. Sijui unakwama wapi kwa Msiba kuheshimu Mawazo yake?

Nani kamzuia kutumia uhuru wake atakavyo? tunahoji polisi inakuwake wawe na double standard kwa wengine? Ww ulianza kuleta lugha za shombo ndio maana, nikaichomoa hiyo suruali yako iliyoingia kwenye makalio, nimeona umepiga kelele hivyo nimeamua kuirudishia ilipokuwa nashangaa unaleta mahubiri. Ukichangia kiungwana hata kama tunatofautiana utapata majibu stahiki, ukija na shombo tunakuchomekea harddisk mbovu.
 
pole sana kaka mkubwa. Binafsi nahofia sana uwezo mdogo wa kufikiri walio nao viongozi wetu kama huyu! Mtu kama Musiba hakuwa mtu wa kuropokaropoka ovyo. Yeye ni kiongozi na kioo cha jamii. Kwa umri alio nao ni mtoto pekee anayeweza kulinganishwa na akili yake. Amekua kimwili, hajakua kiakili. Ukiona mtu anapigapiga kelele ujue ni dalili ya uoga na hata walevi wapo hivyo. Musiba anatakiwa kujiuliza maswali haya 1.kwanini ni yeye tu? 2.Kwanini anapenda kugombana na watu mara kwa mara? 3.Anamiliki nini cha muhimu sana ambacho watu wanakitafuta wamnyang'anye? Kama kiongozi ni lazima utofautiane na watu. Wapo watakaokupenda wapo watakaokuchukia na wapo ambao watakuona wa kawaida. Muhimu asitake kila mtu amuabudu haiwezekani. Kama anawaza kwa uoga hivi je familia yake anaiendeshaje. Kwa ufupi aache drama za kutaka umaarufu. Afanye kazi ambayo aliyempa amemuamini.
 
Kwa kweli inachosha 'Mimi niltegemea kuona kwa kuwa bado imebaki mwaka mmoja tu kipindi cha kampeni ya uchaguzi mkuu kufanyika ' Basi matendo yao na maneno yangekuwa ya busara - lakini wapi

Hii hali wanayo ijenga sasa ni rahisi Kuja kuibua hasira za wapiga kura mwakani na hatimae nchi inaweza kuwa haikaliki kama jinsi ambavyo halishikiki bakuli la chuma lenye uji wa moto
Mi na we tushirikiane kumwangamiza msiba

Unaonaje

Nimesema msiba sio musiba , shaur yako
 
Kaka max ee achana na huyo mhuni msiba atakurabia siku yako tu bure

Sikia nikwambie naomba unisaidie namba ya moderator farida si unajua sisi wanaume hatudhurian kitu brother sisi wanaume wote ni ndugu tena ndugu ila tu kutoka kwa mama mwingine

Msiba ni wa kupuuza tu kaka achana naye
 
Max anatembea na mengi,kifuani!
Wame muandamaa sanaa!
Na ukiangalia,General Election imekaribia!!

Naposema,Aende na beats ana elewa!!
Anajua mengi hadi zengwe na kikao,kilichofanyika kwa ajili yake.

Lengo ni,kuipotezea Jf au akubaliane na masharti ambayo walimpa.
Na kuna donge nono,alitengewa!!

Akisema,Aende na beats. Malalamiko kuhusu moods yatakuwa mengi humu jukwaani!!

Ki,ufupi huyu jamaa,anapita kipindi kigumu sanaaaaaaaaaa
Mkuu. kwenda na beat halafu asituudhi sidhani kama ita wezekana.

Yupo msukuma mmoja humu jf maarufu sana alitaka kufanya yote mawili kwa wakati mmoja, ila yamemshinda na amesha amua kwenda na beat tuu.
 
Acha udini mkuu...binafsi naamini roho mbaya inatokana na makabila na sio dini...wakome wasabato
Bishana na UTAFITI mkuu; na kwanini useme niache udini na sio ukabila? Nimeona watu wa hizo kabila na wakiwa wasababto ni hatari kukaa nao, washirikina, wanafiki, watu wa kujipendekeza, wana chuki za ajabu, wana kuua kimya kimya hadi kwa boss, ukweli sitashangaa nikisikia msiba nae ni msabato, hilo siwezi kulishangaa!
 
Halafu kuna mtu anasema tulinde amani ya nchi yetu, huku akichochea na kuumba mifarakano ya kila namna ndani ya jamii. Kwa kuchagua, tunashindwa kuona madhara ya kinachofanyika hata kwa mifano hai kama watu kushangilia timu ya Taifa kufanya vibaya.
 
Back
Top Bottom