Mkuu. kwenda na beat halafu asituudhi sidhani kama ita wezekana.Tatizo uliharibu,pale ulipogoma kutoa zile details za watu!!
Na ulikosea zaidi,ulipomfuta kazi informer Wao!!
Siku,hizi hawana Milango ya Kuingilia!!
Kwa,Ushauri
Jaribu kwenda na beats ila make sure
Hautuuzi!!!
Cc: Maxence Melo
Mkuu. kwenda na beat halafu asituudhi sidhani kama ita wezekana.
Yupo msukuma mmoja humu jf maarufu sana alitaka kufanya yote mawili kwa wakati mmoja, ila yamemshinda na amesha amua kwenda na beat tuu.
Tatizo uliharibu,pale ulipogoma kutoa zile details za watu!!
Na ulikosea zaidi,ulipomfuta kazi informer Wao!!
Siku,hizi hawana Milango ya Kuingilia!!
Kwa,Ushauri
Jaribu kwenda na beats ila make sure
Hautuuzi!!!
Cc: Maxence Melo
mkikaa kwenye vikao vyenu vya ndani mkumbushane kuwa huu mnaofanya ni upuuzi.Pole kwa yaliyotokea.
Hii paragraph hata mimi niliielewa sana!Kwa watanzania: Watu kama ndugu huyu wapo, tuzikatae kazi zao na wanaowatuma kwa nguvu zote; tusikubali kuletewa migawanyo inayokwepeka. Tuwakemee pale tunapoweza lakini tukibaini kuwa wana nguvu ya ziada, tumwombe Mungu akatende muujiza wake!
POLE MKUU!JEE ULIWAULIZA MUSIBA BINAFSI AMEFUNGUA KESI DHIDI YENU?MAANA TUHUMA ZA KUMUHUSU YEYE MUSIBA,POLISI HUSEMA HAKUNA KESI ILIYOFUNGULIWA.Ndugu wana JF na watanzania kwa ujumla,
Nachukua fursa hii kuwashukuru wote mlioguswa kusikia nimeitwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano baada ya magazeti mawili leo kunihusisha na linalodaiwa kuwa ‘Genge la Watu wanaopanga mikakati ya kumuua Cyprian Musiba”.
Genge hili lilihusisha wanasiasa, taasisi za serikali, watu binafsi (nikiwemo mimi) na hadi viongozi wa Taasisi za Serikali.
Si mara ya kwanza magazeti haya kufanya hivi kwangu na kwa watu wengi (ingawa kwangu imekuwa ikirudiwa kwa angle tofauti tofauti).
Naam, niliitwa saa 3 asubuhi (ingawa habari yenyewe ilitoka siku hiyo hiyo) na nikaambiwa nijitahidi niwe nimefika kabla ya saa 5; nikajitahidi kuitikia wito na kufika mnamo saa 4 na dk 30 asubuhi pale Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.
Nikiri, jopo la wachunguzi wa Jeshi la Polisi walioshiriki kwenye mahojiano nami walionyesha weledi katika kazi yao na hivyo kupelekea mimi na mwanasheria wangu kutoa maelezo yaliyohitajika katika sakata hili.
Nilihoji maswali ya msingi juu ya tuhuma ambazo zimekuwa zikitolewa na bwana huyu na nikahoji kinachopelekea mara zote vyombo vya dola kumwacha aendelee kuumiza watu. Aidha, nikiri pia kuwa maswali yote niliyouliza yalijibiwa kwa staha na undani wa mahojiano yetu nachelea kuuweka bayana kwani naweza kuvuruga uchunguzi.
Niseme: Nawashukuruni nyote mlioguswa na kunitafuta kwa njia mbalimbali kunitia moyo au kutaka kujua mnaweza kusaidiaje. Wengine mlijitoa kuwa tayari kwa dhamana kama ingehitajika, kitendo kilichonifariji kuwa watu wanaelewa tunasimamia nini na kwanini tunaendelea kukisimamia.
Kwa watanzania: Watu kama ndugu huyu wapo, tuzikatae kazi zao na wanaowatuma kwa nguvu zote; tusikubali kuletewa migawanyo inayokwepeka. Tuwakemee pale tunapoweza lakini tukibaini kuwa wana nguvu ya ziada, tumwombe Mungu akatende muujiza wake!
Once again, asanteni sana na Mungu asimame nasi katika kuijenga nchi yetu, Tanzania.
Maxence
Pole sana Max. Kinachonishangaza ni huyu Musiba kuachwa anaropoka ropoka hovyo kwa kuwatuhumu watu huku yeye wala hahojiwi.
Polisi walitakiwa wamuhoji huyo Musiba na ikiwezekana gazeti lake lifungiwe kabisa. Huwa anatuhumu watu bila ushahidi kabisa na anaachwa tu.
Musiba ni nani nchi hii ?
Kwa Kinachoendelea sasa Taifa linapita wakati mgumu na busara isipotumika nadhani tutasambalatika.Kuna uadui na chuki zisizo kifani na chanzo ni huyu ndugu yangu na wanaomtuma. Atokee mmoja tu mwenye Hekima amwambie Msiba tumechoka sana na tunahitaji kujikomboa na anachokiamini na kukitumikia...Pole sana mkuu ''
Kwa hii statement Watesi wetu lazima wanune na kufura kwa hasira. .maneno yako yamejaa Nguvu ya Ukombozi kwa wa tanzania ambao mioyo yao inalia machozi kutokana na kutokubaliana na kile kinacho endelea katika taifa hili 'Huku macho yao yakiwa haya amini kuona Wimbo wa Tanzania ni nchi ya Amani uliokuwa unaimbwa masikioni mwao ukianza kutoweka '
Taifa lime Pata viongozi wanao tugawa wa - tanzania Tumeanza kuwa maadui na ile dhana ya U-ndugu tuliyo nayo inazidi kutokomea Gizani ' mahala tulipofikia nadhani hata shetani ana tu-shangaa
Naomba mniruhusu ni Mtukane Musiba tafadhali
Fanya rejea kesi ya Melo iliyopo Mahakamani Kisutu ndiyo utaelewaHii hapa Sikuelewa chochote.. mkuu fafanua maana inaonekana unajua kinachoendelea...