Tuhuma za matumizi mabaya ya fedha: Wabunge wa CHADEMA waanza kuhojiwa TAKUKURU

Ukweli na Uwazi ni muhimu kwa mustakabali wa kesho ya taifa hili...TAKUKURU na wahojiwa watendee haki Watanzania.
 
Wabunge wa CHADEMA leo wameanza kuwasili katika ofisi za TAKUKURU jijini Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa. Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) amekuwa wa kwanza kufika

TAKUKURU ilisema itawahoji wabunge 69 wa chama hicho kufuatia malalamiko juu ya matumizi ya fedha za makato katika mishahara
Kati ya Taasisi ambazo zitafanyiwa reformation kubwa au kuvunjwa kabisa na kuundwa upya baada ya CCM kutoka Mahakamani hapo October namba
1. TISS
2. Takukuru
3. Polisi
4. Magereza

Naona JWTZ ndo taasisi pekee itakayoepuka mkono huu maana ndo taasisi pekee iliyofanikiwa kujitenga na siasa uchwara za CCM
 
Kati ya Taasisi ambazo zitafanyiwa reformation kubwa au kuvunjwa kabisa na kuundwa upya baada ya CCM kutoka Mahakamani hapo October namba
1. TISS
2. Takukuru
3. Polisi
4. Magereza

Naona JWTZ ndo taasisi pekee itakayoepuka mkono huu maana ndo taasisi pekee iliyofanikiwa kujitenga na siasa uchwara za CCM
Hii imejitahidi!
 
Wabunge wa CHADEMA leo wameanza kuwasili katika ofisi za TAKUKURU jijini Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa. Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) amekuwa wa kwanza kufika.

TAKUKURU ilisema itawahoji wabunge 69 wa chama hicho kufuatia malalamiko juu ya matumizi ya fedha za makato katika mishahara.
Atakayebainika kudanganya kwa maslahi ya Mbowe nae ashitakiwe kwa uongo!
 
Naiita "selective justice". Wanachagua nani wa kutupa na nani wa kubeba. Nassari aliwapa video ya Mnyeti akitoa rushwa kwa wabunge na madiwani wa CHADEMA, wakasema hakuna ushahidi. Mnyeti akapandishwa cheo na kuwa mkuu wa mkoa! CUF ya Lipumba ni mshirika wao.
Wakimaliza waende na CUF ya Lipumba, CAG alisema walivuta mil 300 wakaweka kwenye account binafsi kinyume na utaratibu.

JINSI TIMU LIPUMBA ILIVYOLAMBA MIL. 300/- | Mtanzania
 
Naam, wanahojiwa tu ingawa bado sijaelemewa kwanini wanahojiwa na chombo cha makosa ya rushwa wakati tuhuma ni matumizi mabaya ya fedha! Lakini pia tukumbuke kuwa kuna wakati zilitolewa tuhuma bungeni kuwa baadhi ya wabunge wetu wamepewa rushwa ya sh. 10m/= kila mmoja kipindi cha kuelekea kujadiliwa miswada ya sheria iliyokuwa na utata mkubwa. Kiti cha Spika kulizuia tuhuma hizi zisijibiwe bungeni. Baada ya muda Rais Magufuli alipokutana na vyombo vya habari kwa mara kwanza aliulizwa swali kuhusu tuhuma hizi hizi. Rais alijibu kuwa atakabidhi TAKUKURU. Hakuna mrejesho wowote uliotolewa kwa umma kuhusu tuhuma hizi nzito mno.
 
Hii ni wakati akiingia kuhojiwa kutokana na wito wa TAKUKURU wa kuwahoji wabunge wa Chadema kwa Tuhuma za kutengezwa na mamluki za matumizi ya fedha za michango ya wabunge wa chama hicho.
 

Attachments

  • Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi akiingia kuhojiwa katika Ofi ( 352 X 640 ).mp4
    3.8 MB
Hii ni wakati akiingia kuhojiwa kutokana na wito wa TAKUKURU wa kuwahoji wabunge wa Chadema kwa Tuhuma za kutengezwa na mamluki za matumizi ya fedha za michango ya wabunge wa chama hicho
Duh.... Mbowe ndio wanammaliza hivyo...... Sugu na mchungaji Msigwa siyo watu wa kuwaamini kabisa!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom