Tuhuma za kutisha za Dr. Munga Askofu KKKT -DKMS

Wapendwa Wana DKMS - KKKT, Salaam katika Kristo Yesu Mkombozi wa wanadamu = Redemptor Hominis!

SABABU ZA KUFANYA MATENGENEZO DKMS - KKKT.

"Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua"
Mithali 29:2.

Inawezekana wengi wenu hamjui kwanini kunahitajika kufanyika matengenezo ya haraka DKMS - KKKT; ni kwamba zipo sababu nyingi sana zilizopelekea jambo hilo:

1. Kuinusuru Dayosisi isiendelee kuongewa madeni.
Kwamba; Uongozi uliopo sasa ambao hauamini kuwa muda wao Kikatiba umemalizika unaendelea kulimbikiza madeni, na hawawezi kufanya muujiza wowote. Deni la SEKOMU tu ni kizungumkuti. Tumshukuru Mungu Ripoti ya Kamati ya Reweta imeshapatikana yote mtayaona kwa uso na macho; hamtaamini jinsi Chuo Kikuu Cha Kumbukumbu cha Sebastian Kolowa kilivyohujumiwa na kuleta adha kwa Wafanyakazi na Washarika.

2. Kwamba pia Watumishi wengi wa DKMS - KKKT, wanaishi maisha ya dhiki sana, Mishahara na posho zao hawajapata kwa muda mrefu sasa, sijui na janga hili la Corona wataishije maskini ya Mungu. Watumishi hawa wanaogopa kupaza sauti zao; lakini Jipeni moyo Mtetezi wenu yu hai: Msiogope!

3. Kwamba Vituo vingi vya Dayosisi viko hoi(ICU). Vuga Press imefungwa, Bangala Seminary hoi, Lwandai hoi, Hospitali ya Kilindi yachechemea, Bumbuli Hospital nayo ni tia maji tia maji. Hali ni mbaya, kama husadiki tembelea Vituo hivyo utajionea mwenyewe.

4. Kuvuruga uhusiano wa DKMS na marafiki wa Ujerumani.

Hayati Baba Askofu Dkt Sebastian Ignatius Kolowa, ThD, alianzisha Urafiki baina DKMS na Makanisa ya Ujerumani, na mashirika mbalimbali ya Kitume ya Ulaya. Urafiki ulikuwa na manufaa makubwa sana katika Dayosisi hii. Marafiki hao walisaidia sana katika uwanja wa? huduma za kijamii; kama vile, Lutindi Mental Hospital, Irente School for the blind, Irente Children's Home, Usambara Technology Center, ATIFA, Irente, Irente Rehabilitation Center, Rainbow School. Vituo hivyo vilisaidiwa sana kutokana na Urafiki huo. Baada ya Kifo cha Mzee Askofu Kolowa, Dayosisi ikaongozwa na Mt Petro Baba Askofu Joseph Jally, tunamuita Mtume Petro kwakuwa hana makuu, ni? mpole, mnyenyekevu, mwenye upendo, ni mtu wa sala na maombi, alizifuata nyayo za Mtangulizi wake. Akaicha Dayosisi katika hali njema.

Sasa huyu baada ya Askofu Jally, ndio kaiweka Dayosisi kitanzini.

5. Mahusiano ya DKMS na Serikali.

Tokea enzi ya Askofu Dkt Sebastian Kolowa, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ilikuwa na mahusiano mazuri na Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wala hakukutokea chokochoko yoyote. Ushirikiano ulijengwa katika huduma za kijamii, kutembeleana, kushauriana na kuombeana kwa amani. Hata Mzee Askofu Jally, alidumisha mahusiano mazuri.

Sasa kiyangayanga ni kwa huyu Mwanaharakati Askofu wa DKMS asiyetaka kustaafu, kosoa weee Serikali, mapovu yakimtoka, huko yeye mwenyewe akiwa na boriti limemzinga, (Mathayo 7:5). Ukiishi kwenye nyumba ya vioo usiwarushie wengine mawe: Ona sasa kwa matumizi yako mabaya ya madaraka (Mr Mkuu wa Chuo SEKOMU, Mrs Makamu Mkuu wa Chuo, na huku Katibu Mkuu wa DKMS ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha SEKOMU, aah majanga): umeleta janga la kutolipa Kodi ambayo Dayosisi inadaiwa, mamilioni na mamilioni, ujanja wako uko wapi?. Ubadhilifu ndio ulioifikisha DKMS hapa, TRA, WFC, NSSF kote wanadai.

Usijidanye kulipa Kodi ni Amri halali tena ni agizo la Mungu: Soma Injili ya Luka 20:21 - 26.

6. Kuvuruga uhusiano wetu na Madayosisi mengine.

Kama hujui Askofu, DKMS imekuwa na mahusiano ya kihistoria na kindugu; nikuingize darasani kidogo pamoja na hiyo PhD yako, kwa kukupa mfano wa Madayosisi ya Kanda ya tu: Tumekuwa ndugu, udugu wetu ulijengwa na Mababa Askofu Moshi, Askofu Kolowa, Askofu Kweka na Askofu Mshana wa Pare, Askofu Jally na Askofu Msangi. Jamii yetu imechanganyika mno, tunaoshirikiana mno. Uliza siku mwili wa Mzee Askofu Kolowa, uliposafirishwa toka KCMC kwenda Lushoto, mji mzima wa Moshi na Pare ulisimamisha shughuli zao kwa kumuenzi Mzee Askofu Kolowa, walimwona kuwa ni Baba yao. Sisi Waumini wa DKMS hakuelewi kwanini unamshambulia Mkuu wetu wa Kanisa? Halafu unawaeleza washarika Kanisani ili iweje?

Ukome kabisa na uache tabia hiyo. Tena Baba Askofu Charles Mjema wa Dayosisi usimfuate Askofu Munga atakuingiza chaka.

7. Kuwafukuza na Kuwasimamisha Uchungaji baadhi ya Watumishi.

Kama Baba Askofu Kolowa asingemsihi Mkuu wa Chuo cha Makumira Mch Dkt Hans Mwakabana asikufukuze Chuo cha Uchungaji kutokana na uliyoyatenda ukiwa usingefikia hapo ulipofikia (kisa chenyewe tunakitunza).
Umefukuza Mch Dkt Kopwe, Dean Mch Mwamboza, Mch Crispus Kanju, umewasimamisha Mch Peter Zakaria na Mch Dickson, bila sababu za msingi . Aliyekuwa na Katibu Mkuu Mch Godrey Hermann umemfanyia figisu figusu, akaamua kukuachia ofisi. Ulishamsimamisha Mch Shekifu na Dean Mmaka pia. Wote hao umewaumiza, tunajiuliza ni jiroho gani lililokukamata.

8. Kutowathamini Watumishi Wastaafu.

Hivi Askofu Dkt Stephen, unapata muda wa kuwajulia hali Wastaafu pamoja na wajane!. Huna muda huo uko bize. Pension pia huwapi, wakati unataka maslahi makubwa.

9. Mafao ya Askofu Munga atakapostaafu.

Ulipeleka madai ya mafao ya kustaafu kwako kuwa:

a.Ujengewe Nyumba kubwa ya kuishi,

b.Ujengewe Nyumba ya vyumba vitatu (3), kwa ajili ya Watumishi.

c.Uwekewe Watumishi wataolipwa na Dayosisi yaani Dereva, walinzi, wapishi na mfanyakazi wa bustani.

d. Ununuliwe gari kubwa la kifahari V8 au VX

e. Ujengewe bwawa kubwa la samaki, ili uepuke kula RED MEAT(nyama nyekundu), aloo rahaa utamu!

f. Alipwe mshahara unaotosheleza, na kutunzwa hadi ukamilifu wa dahari.

Je, watangulizi wako walifanyiwa hivyo? Wafanyie kwanza halafu wewe ndio ufuate.

Mwisho Wachungaji, Watumishi na Washarika wote wa DKMS msidanganyike; Muda wa kipindi cha Uaskofu wa Munga umemalizika, hana mamlaka ya kuongoza Mkutano Mkuu wala Kikao chochote kabisa.

Bado anaendelea kutumia Gari la Kanisa na Posho, yuko DSM na Wasaidizi wanapanga mkakati wa kujinasua.

FAHAMUNI KANUNI YA 6 ya Katiba ya DKMS - KKKT ya Mwaka 2000:

E.
1. Askofu
c. Askofu atatakiwa kustaafu Kikatiba akiwa na umri wa miaka sitini na tano (65) ya kuzaliwa, lakini anaweza kustaafu kwa hiari yake akiwa na miaka sitini (60).

Habari ndiyo hiyo.

Tena Kanuni hiyohiyo ya 6:

F. Ukomo wa Uongozi.

Kiongozi anaweza kuacha kazi, kuachishwa, kujiuzulu ama kufukuzwa ikiwa;

1. Hatatimiza wajibu wake au akivunja Kanuni na Sheria za Dayosisi.
4.Kustaafu akitimiza umri wa kustaafu kisheria.
5. Kujiuzulu kwa hiari yake mwenyewe.
6. Kujiuzulu kwa kuwajibika.

Jiulize anatokaje hapo?

Ni jukumu lake kutafakari na kuchukua hatua kwani Neno la Mungu lasema:

"Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha;
Bali wajinga huendelea mbele wakaumia.
Mithali 22:3

Wakatabahu,

+++ Sauti ya Kijito Kedroni.

Jr
Mazito sana haya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ASKOFU DKT STEPHEN ISMAIL MUNGA JIUZULU UINUSURU DAYOSISI.

Askofu Dr Stephen Ismail Munga, Salaam katika Kristo Yesu Mfufuka!

Muda wako wa Uaskofu wako DKMS - KKKT umemalizika, Ila hujaamini kuwa uko nje ya muda.

Tunajua umeagiza kwa Wasaidizi wako Dean na Katibu Mkuu waitishe Kikao cha Wachungaji ili uwatishe, wakutetee: Nakwambia hivi hii sio habari ya kitoto, huu muziki ni munene, tunazo taarifa nyingi, huwezi chomoka. Hivi zile milioni 200 alizozitoa Katibu Mkuu DKMS na kumpa Shemeji yake kwaajili ya wa uanzishwaji wa Utume Radio na Television ziko wapi?. Ile Tume ya Wakuu wa Dinari iliyoundwa na Halmashauri Kuu kufuatilia hilo umefikia wapi?

Usiitishe Kikao cha Wachungaji huna mamlaka, muda wako umekwisha.

Kaidi Mahakama itatafsiri.

Jr
 
d. Ununuliwe gari kubwa la kifahari V8 au VX
Hii issue ya Munga kupatiwa gari kubwa aina ya V8 au VX ina trend sana.. kwa waumini.. ha ha ha nafikiri itatokana na MFUKO MPANA...😂😂😂 niliipata kwenye jumuiya yangu.... tulicheka sana.... bro Munga.... tengeneza mazingira uondoke kwa heshima... wala usiwe na wazo la kuweka mtu wako.... Nakukumbusha... Mwinuka... Kingazi.... kuwa nao makini. Bwana Apewe Sifa.
 
Sijaielewa hii ya gari.. Yaani apewe V8 ili astaafu?
d. Ununuliwe gari kubwa la kifahari V8 au VX
Hii issue ya Munga kupatiwa gari kubwa aina ya V8 au VX ina trend sana.. kwa waumini.. ha ha ha nafikiri itatokana na MFUKO MPANA... niliipata kwenye jumuiya yangu.... tulicheka sana.... bro Munga.... tengeneza mazingira uondoke kwa heshima... wala usiwe na wazo la kuweka mtu wako.... Nakukumbusha... Mwinuka... Kingazi.... kuwa nao makini. Bwana Apewe Sifa.

Jr
 
ASKOFU MSTAAFU DKT STEPHEN ISMAIL MUNGA KUJIFICHA KWAKO HAKUTAKUSAIDIA KITU.

"Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko".
Zaburi 139:7 -8.

Askofu Mstaafu wa DKMS - KKKT, Dkt Stephen Munga, ninakusalimu katika Jina la Yesu Kristo Mwokozi wa kweli.

Mimi niliye mjumbe wa Mungu, nimeagizwa kukuletea ujumbe huu kwamba "KUJIFICHA KWAKO HAKUTAKUSAIDIA LOLOTE".

Darubini za Kimbingu na zile za Intelejensia Takatifu (Holy Intelligence), zinaonyesha
kuwa umejificha katika Hostel ya DKMS, iliyoko Songe Wilayani Kilindi, Mkoani Tanga; na unahudumiwa na Parish Worker aitwaye Dorothy Baka. Huyu Dorothy Baka ni mwenyeji wa Lewa - Korogwe, alikuwa Mwanglikana, baadaye alihamia Lutheran.

Hivi sasa Askofu Mstaafu Munga umeacha kutumia Gari lako la Ofisi ya Askofu, unatumia gari la Ofisi ya Katibu Mkuu wa DKMS; na Dereva wa Katibu Mkuu ndiye anayeendesha gari.

Mipango yote uliyopanga nimeinasa tayari, kama ifuatavyo:

1. Staili ya maisha yako itakuwa ya kujifichaficha na kuhamahama maeneo, unafanya hivyo ili kusubiri muda wa Mkutano Mkuu wa Dayosisi.

2. Umepanga kwamba utaitisha Mkutano Mkuu wa kustukiza Siku ya Alhamis ya Agosti 6, 2020. Mkutano huo Mkutano Mkuu wa DKMS umepanga kuwa utakuwa Maalum, na ajenda itakuwa moja tu ya Uchaguzi.

3. Umepanga pia kwamba baada ya Uchaguzi huo, wa kumpata aliye chaguo lako ili akufichie majanga yako, utaondoka nchini mara moja na kwenda kuishi katika makazi yako.

Askofu Mstaafu Dkt Munga, kumbuka ya kwamba Mungu yuko kila mahali na huwezi kumkimbia wala kujificha.

Kwanini unafanya shingo yako kuwa ngumu?.
Kwanini umejaza kiburi moyoni mwako?.
Kwanini unashindana na Mungu???.
Kwanini unalitesa Kanisa la Mungu alilolikomboa kwa damu yake ya thamani?.

Askofu Mstaafu Munga, nikueleze wazi, na kama hutaelewa vipimo vya Afya ya Akili vinakuhusu, kwamba;

(a) Wewe ni Askofu Mstaafu, huna Locus standi yoyote ya kuitisha Mkutano Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ya KKKT. Si hilo la Mkutano Mkuu tu, bali hurusiwi pia kuiwakilisha DKMS mahali popote, elewa hivyo. Huruhusiwi kuitisha Kikao chochote kiwe cha Wachungaji, Wakuu wa Majimbo, Wakuu wa Idara na Taasisi za DKMS; Mamlaka yako imekoma.

(b) Nakufundisha tena ingawa Mimi sina PhD kama wewe, nikurudishe katika KANUNI YA VII, ya Katiba ya DKMS ya Mwaka 2000: Sehemu hii inahusu "Wajibu wa Halmashauri Kuu ya Dayosisi

Kanuni ya VII:
D: 14 inasomeka hivi: "Kuandaa agenda za Mkutano Mkuu wa Dayosisi".

Hiyo ni moja kati ya wajibu wa Halmashauri Kuu ya Dayosisi. Hebu toka huko mafichoni uuelezee umma wa Wana DKMS ni lini kilifanyika Kikao cha Halmashauri Kuu ya Dayosisi kupanga na kuamua hayo?.

Askofu Mstaafu Munga usiivuruge amani ya DKMS na ya Wananchi pia, Kanisa hili ni sehemu ya Wanajamii wa Mkoa wa Tanga; unapoivuruga DKMS elewa umeivuruga Jamii katika Mkoa wa Tanga kwani yako mahusiano ya karibu sana na mashirikiano mema Kati ya Waumini na Jamii pamoja na Madhehebu mbalimbali, hata yale yasiyo ya Kikristo pia.

Ujumbe wa Mungu Mwenyezi kwako Askofu Mstaafu Dkt Stephen Ismail Munga ni huu:

(I) Uache mara moja kuivuruga DKMS.

(II) Kwakuwa umestaafu toka huko mafichoni ukaikabidhi Dayosisi kwa Mkuu wa KKKT; jambo hilo lifanyike ndani ya Kanisa Kuu la Dayosisi - Utondolo Cathedral. Awepo Baba Askofu Mstaafu Joseph Mathayo Jally, Chaplain wa Kanisa Kuu, Mwanasheria wa Dayosisi, Afisa Utumishi, wazee wa Kanisa wawili(ke na me), Vijana wawili (ke na me) pamoja na watoto wawili wa Sunday School (ke na me), hao wote wataiwakilisha DKMS; hakuna haja ya kuwepo na Washarika wengine.

Kama unaona aibu kufanya hivyo mbele ya hao watu, nenda kimyakimya Kanisa Kuu Utondolo Lushoto kailaze Fimbo ya Uaskofu juu ya Madhabahu; hapo utakuwa umetimiza agizo la Mungu la kuachia madaraka ambalo pia ni takwa la Kikatiba.

(III) Kristo Yesu anakushauri Utubu na Kumrudia Mungu ili upate rehema. Omba msamaha kwa Dayosisi na kwa wote uliowaumiza na kuwaumiza. Hilo hulazimishwi umeshauriwa tu.

Angalizo limfikie pia Katibu Mkuu wa DKMS kuwa Ofisi Kuu ya DKMS isigharimie kwa namna yoyote ile safari za Askofu Mstaafu Munga, hata fedha mliyompa kwenda mafichoni Songe Kilindi ni kinyume na utaratibu.

Mwinjilisti William Mahonge msimsumbue hahusiki na lolote katika ujumbe huu. Yupo Mjumbe mmoja Maalum aliyetumwa na Mungu kuwafikishia ujumbe huo wa kuikomboa DKMS toka katika mikono dhalimu. Mjumbe huyo hana Kamati wala nini, mtafuteni yeye msiwasumbue wengine kwani;

"Roho ya Bwana yu juu yangu,
Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema.
Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao,
Na vipofu kupata kuona tena,
Kuwaacha waliosetwa,
Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa".
Luka 4:18 - 19.

Kuna baadhi yenu mnauliza kama Wanafunzi wa Yesu kwa mambo haya yatatukia lini?

"Je! Bwana, ni wakati huu ndipo utakapowarudishia Israeli ufalme?"
(Matendo 1:6)

Wana NED mnaouliza hivyo jibu ni hili kwamba;

"Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika yake mwenyewe."
Mdo 1:7.

Niwatie moyo msihofu ukombozi umekaribia: Uko mlangoni, anzeni kumshangilia na Kumtukuza Mungu kuanzia Tanga Mbuyukenda ilipoanzia Injili 1890 hadi Hohen Mlalo 1891, na baadaye katika maeneo mengine katika Dayosisi hii.

Kwaya Kuu Lushoto anzeni kuimba ule wimbo wenu:

"Jubilate Jubilate
Jubilate Jubilate
Jubilate Domino

Ooh Mwalimu Semkiwa na akagone (RIP)
Tunayamisi maimbo na mashangilizi yako.

+++Sauti ya Musa Jangwani.

Jr
 
WAUMINI DKMS - KKKT
S.L.P 10
LUSHOTO

03/04/2020


MKUU WA KKKT
S.L.P 3033
ARUSHA
TANZANIA

Salaam katika Jina la Bwana na Mwokozi wetu Kristo!

MALALAMIKO YETU DHIDI YA HUJUMA NA UBADHILIFU WA ASKOFU STEPHEN ISMAIL MUNGA WA DKMS - KKKT

"Kama si BWANA aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa," Zaburi 124:1.

Mh. Mkuu wa Kanila la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, tunatambua kuwa unayo majukumu mengi ya kuliongoza Kanisa letu la KKKT, pamoja na majukumu haya tunaomba uweke uzito stahiki katika waraka huu tunaokuandikia ili uweze kuinusuru Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ya KKKT.

Sisi Waumini wa DKMS - KKKT; ambao majina yet una saini zetu zimo katika barua hii tunapowakilisha wana Dayosisi wengi kwa kuzingatia Kanuni zifuatazo za Katiba ya KKKT - Toleo la Mwaka 2015:
Kanuni ya VII: G:3,
Kanuni ya VIII: C:2 na 3
Kanuni ya XII:A:1,4,5,7 na
Kanuni ya XIV:A:1,2,3,4,
tumeona ni vema kuleta malalamiko yetu kwenye Ofisi yako, kama kichwa cha habari hapo juu kinavyosomeka.

Mh. Mkuu wa Kanisa, DKMS - KKKT, ina hali ngumu mno kutokana na Uongozi usiofaa wa Askofu Dkt. Stephen Munga, ambaye, bado anang'ang'ania madaraka licha ya muda wake wa kuiongoza DKMS - KKKT kumalizika tokea Mwezi Machi 2020 ( Taz. Katiba ya DKMS - KKKT ya Mwaka 2000: Articles 6: 1c ambayo tumeiambatanisha katika barua hii kiambatisho namba 5), na kuendelea kuingiza Dayosisi ya Kaskazini Mashariki katika mazingira magumu.

Bila ya kumung'ung'unya maneno malalamiko yetu dhidi ya Askofu Stephen Ismail Munga, ni haya yafuatayo;

1. Kuisigina Katiba ya DKMS - KKKT ya Mwaka 2000: articles 6:1c, inayomlazimu Askofu wa DKMS - KKKT kustaafu afikiapo umri wa miaka 65; na hakuna kuongeza ama kuongezewa muda. Hata katika Katiba ya KKKT Toleo la Mwaka 2015 Kanuni ya XIV: A3, inatoa mwongozo. Askofu Stephen Munga amegoma kustaafu na hivyo amejiongezea muda kinyemela bila kupitishwa na kikao chochote cha Kikatiba.

2. Askofu Stephen Munga amesababisha anguko la SEKOMU.

A.Tarehe 20/10/2009, ilitolewa Ripoti ya Ukaguzi wa Fedha za SEKOMU; Bw. Yohana Mnkanda ndiye aliyetoa Ripoti hiyo ambayo tumeimbatanisha kama kiambatanisho namba 6. Ripoti hiyo ilionesha ubadhilifu mkubwa wa Fedha za Chuo, na yeye akiwa kiongozi wa Dayosisi aliifumbia macho kwani Mke wake (Mch. Dkt. Aneth Munga) alihusika katika ubadhilifu huo akiwa Provost wa Chuo hicho.

Dean wa DKMS wa wakati huo Mch. Jonathan Mwamboza aliingilia kati swala la ripoti hiyo, kwamba ifanyiwe kazi, lakini juhudi zake hazikuzaa matunda kwani zilizimwa kwa maelekezo ya Memo toka kwa Askofu Munga ya tarehe 8/10/2009, akitaka jambo hilo liachwe. Memo hiyo tumeiambatanisha kama kiambatanisho namba 7.

Jambo hilo la Dean kutaka kuchukua hatua kutokana na Ripoti hiyo kuligharimu Huduma yake, na kupelekea kuvuliwa Uchungaji kwa barua ya tarehe 24/08/2010, ambayo tumeimbatanisha kama kiambatanisho namba 8.

B. Tarehe 14.12. 2018 Halmashauri Kuu ya DKMS - KKKT, iliunda Tume Maalum, ambayo ilipewa jukumu la kuchunguza matatizo yanayoikabili SEKOMU hata kupelekea Chuo hicho kufikia hali mbaya na hivyo kusitishiwa usajili hadi sasa. Tume hii iliapishwa rasmi na Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu Askofu Dkt. Stephen Munga na kuanza kazi rasmi tarehe 17.12.2018 ikizingatia hadidu za rejea ilizopewa na Halmashauri Kuu.

Tume hiyo iligundua ubadhilifu mkubwa mno wa Fedha, na ilitoa mapendekezo kwa Halmashauri Kuu ya DKMS, kuwa wote waliohusika wawajibike, akiwemo Askofu Stephen Munga, Mch. Dkt. Aneth Munga, Msaidizi wa Askofu Mch. Dkt. Eberhart Ngugi, Katibu Mkuu Mch. James Mwinuka ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha ya SEKOMU, na Bw. Geofrey Kingazi ambaye ni Mkurugenzi wa Fedha SEKOMU.

Ripoti hiyo ya Tume Maalum yenye ya kurasa zipatazo 85 ilizimwa na Askofu Munga na wala haikufanyiwa kazi yoyote mpaka sasa.

C. Madeni Makubwa ya SEKOMU
Chuo cha SEKOMU kimeingia kwenye madeni makubwa na kuiweka Dayosisi mahali pabaya sana kutokana na sababu mbalimbali:

i) Udhibiti mbovu wa Fedha.
- Kwa kuwa Chuo hiki kimeongozwa kwa misingi ya kindugu hakuna kuwajibishana katika maswala nyeti ya Fedha. Mf. Vice Chancellor ni mke wa Askofu hivyo japo alionekana kuwa hana uwezo hapakuwa na yeyote wa kumkemea kwa sababu ya masilahi ya kifamilia.

- Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha ya Chuo, Mch. James Mwinuka ni mtu wa karibu sana wa Familia ya Askofu.

- Mkurugenzi wa Fedha wa Chuo Bw. Geofrey Kingazi ambaye ni ndugu wa Askofu Munga ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha ya Dayosisi. Kwa mtindo huu Mwenyekiti wa Kamati ya Chuo, ambaye ni Katibu Mkuu hawezi kumuwajibisha Mkurugenzi wa Fedha wa Chuo kwa kuwa naye atawajibishwa na mtu huyo huyo kwenye vikao vya Kidayosisi. Kilichopo hap ani kwamba ukiniwajibisha leo nami nitakuwajibisha kesho nitakapokalia kiti. Kwa maneno mepesi ni kwamba tutunziane siri na kulindana. Hapo ndipo shimo kubwa lililopokea fedha za SEKOMU lilipoanzia.

ii) Askofu Stephen Munga, mara kwa mara alidharau ushauri wa TCU kuhusu namna nzuri ya kuendesha Chuo cha SEKOMU, kwa kufuata Miongozo na Kanuni, za TCU akiendelea kung’ang’ania mke aendelee kuwa Vice Chancellor hata kama hana sifa zitoshazo. Haya yote yalipelekea Chuo hicho kutokidhi vigezo vya udahili, na kuibuka kwa madeni makubwa yanayoikabili Taasisi hiyo na Dayosisi kwa ujumla.

iii) Kuna Deni la CRDB la Sh. 1,300,000,000 (Bilioni Moja na Milioni Mia Tatu) ambalo mpaka sasa halijalipwa. Mwaka 2018 hadi 2019 Uongozi wa DKMS chini ya Askofu Dkt. Stephen Munga, Deni hili liligawanywa kwenye Dinari na Vituo vya Dayosisi kwa viwango kama ifuatavyo:

a) Dinari ya Pwani - Sh. 400,000,000/=
b) Dinari ya Tambarare - Sh. 400,000,000/=
c) Dinari ya Kusini - Sh. 200,000,000/=
d) Dinari ya Kaskazini – Sh. 100,000,000/=
e) Ofisi Kuu ya Dayosisi Sh. 100,000,000/=
f) Vituo vya Dayosisi - Sh. 100,000,000/=
Jumla Sh. 1,300,000,000.

Waumini wa DKMS kupitia Sharika zao na vituo walijitoa kwa moyo kuchangia kuliondosha deni hilo, na kwa asilimia kubwa fedha hiyo ilipatikana; cha ajabu ukisoma katika Ripoti ya TCU kwa SEKOMU; SEKOMU 6 MONTH REPORT, utaona deni hilo lipo na halijalipwa. Swali kubwa letu sisi Washarika wa DKMs ni kwamba je fedha zote tulizochanga zimekwenda wapi?

Mwanzoni mwa mwaka 2019 Askofu Dkt. Stephen Munga na Katibu Mkuu waliitisha harambee maalum ya kuinusuru SEKOMU huko Dar es Salaam. Walioalikwa kwenye Harambee hiyo walikuwa Dkt. Reginald Mengi (Marehemu), Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa, Wabunge na viongozi mbalimbali. Haijulikani hadi sasa kuwa fedha zilizopatikana kupitia Harambee hiyo zimeelekezwa wapi.

Ripoti ya TCU imeonyesha kwa uchache madeni yanayokikabili Chuo, yakiwemo yale ya TRA, NSSF, WCF, Mishahara ya Watumishi wa Chuo, ambapo Deni hilo linaoneshwa kuwa ni zaidi ya Tsh. Bilioni 2.

Kutokana na madeni hayo, baadhi ya Watumishi wa Chuo hicho wamefungua kesi Mahakamani kudai haki zao ambazo ni fedha nyingi mno kuliko tunavyofikiri. Kwa kuwa kesi hizi ziko Mahakamani hatutapenda kuzungumza mengi hapa.

Miongoni mwa Madeni haya yamepelekea Basi aina ya Coaster lenye namba za usajili T 114 CDT mali ya SEKOMU kupigwa mnada na kuuzwa kwa Sh. 24,000,000/= , baada ya Mtumishi mmoja kushinda kesi dhidi ya Dayosisi. Bado mtumishi huyu anadai fedha nyingi kwa kuwa kiasi cha fedha zilizopatikana kwa mnada wa Coaster hii hakikutosha. Picha ya Coaster hii inaambatanishwa kama kielelezo, (kiambatanisho namba 9)

Tunaambatanisha Ripoti ya TCU kama kiambatisho namba 10; kwani Wana DKMS pamoja na Wachungaji wao wanaaminishwa kuwa hakuna deni lolote.

3. Kuuzwa kwa Kituo cha Mafuta BP Mombo.

Askofu Dkt. Stephen Munga amekiuza Kituo cha Mafuta Mombo kwa Bw. Mziray kwa Sh. 300,000,000/= bila ya idhini ya Halmashauri Kuu ya Dayosisi, na haijulikani Fedha hizo amepeleka wapi. Bw Mziray kwanza alilipa Tsh. 210,000,000/=, na pale atakapokabidhiwa Hati ya eneo hilo angemalizia kiasi kilichobaki. Baada ya kutopewa Hati aliamua kufungua Kesi Mahakama Kuu Tanga, na upo uwezekano wa DKMS - KKKT kuingia hasara ya kumlipa mamilioni ya fedha.

4. Uvunaji wa Misitu ya Dayosisi bila kibali cha Halmashauri Kuu ya DKMS.
Misitu mingi ya Dayosisi imevunwa kwa agizo la Askofu wa DKMS, bila ya Utaratibu bila H/Kuu kuridhia. Misitu hiyo ni ya Magamba, Chatlon, VBS, Bangala na Mponde. Hali ya maeneo hayo ni ya kutisha, na wala haijulikani fedha zilizopatikana katika uvunaji wa Misitu hiyo, Askofu Munga na timu yake wamezipeleka wapi. Shamba la Magundi Korogwe linatakiwa kukaguliwa kama bado linamilikiwa na DKMS.

5. Hali ngumu ya Watumishi katika Dayosisi.

Watumishi wengi katika Vituo vya Dayosisi, mf. Ofisi Kuu ya Dayosisi, Lwandai Sekondari, Bangala Seminari, Vuga Press, Tumaini Hostel, Radio Utume nk wako katika hali ngumu mno. Hawalipwi mishahara yao kwa miezi mingi sasa, hawana tumaini, wanateseka, hawana pa kusemea maana Askofu Munga yu juu ya Halmashauri Kuu ya DKMS, anawaburuza anavyotaka.

Wachungaji walio wengi wanapata maumivu makubwa kwa kukosa posho zao kwa ajili ya michango mikubwa ya fedha ili kuinusuru SEKOMU lakini hawathubutu kusema lolote kwa kuwa Askofu ameshatamka kuwa yeyote atakayenyanyua mdomo kinyume na Askofu atafukuzwa kazi mara moja. Watumishi wa Dayosisi wakihojiwa wataeleza maumivu yao.

6. Hali mbaya ya Vituo katika Dayosisi.

Vituo kama Vuga Press, Lwandai Sekondari, Bangala Seminari, Mbuyukenda, Tumaini, Duka la Vitabu Lushoto, vinapita katika bonde la uvuli wa mauti; na viko hatarini ya kufungwa kama UTC na Gereji ya Lushoto zilivyofungwa kutokana na Uongozi mbovu wa Askofu Munga.

7. Uanaharakati na mapambano.

Askofu Dk Stephen Ismail Munga amepoteza sifa za Kichungaji, huduma yake ameielekeza zaidi katika uanaharakati na mapambano ya kuwaumiza wengine wakati kwake kumemshinda. Tokea alipoingia madarakani alianza kuvuruga Umoja wa Kanisa, aliibadilisha Katiba, KKKT - DKMS, na kuwa DKMS - KKKT, Majimbo kuwa Dinari, na Wakuu wa Majimbo kuitwa Wakuu wa Dinari, ili mradi ajiweke kinyume na Madayosisi mengine ya KKKT. Haya aliyafanya mara tu baada ya kushindwa kwenye kinyang’anyiro cha Ukuu wa Kanisa alipochaguliwa Askofu Dkt. Alex Malasusa. Hivi karibuni pia tumeshuhudia akihamasisha na kushiriki vikao visivyo rasmi vya kuivuruga KKKT kama kile alichokifanya Dodoma Machi 18, 2020. Dayosisi ya Kaskazini Mashariki haijamtuma kufanya hivyo, na hatujui mamlaka hiyo ameitoa wapi na pia ijulikane kuwa gharama za safari hizo anagharimiwa na Dayosisi kinyume cha utaratibu.

8. Kuwasimamisha/ kuwafukuza Uchungaji/ na Utumishi katika Dayosisi. Tokea Askofu Munga aingie madarakani tumeshuhudia akiwasimamisha baadhi ya Wachungaji na Watumishi wa DKMS: mfano:

- Mch. Godfrey Hermann aliyekuwa Dean na Katibu Mkuu, aliyeitumikia DKMS kwa weledi na uaminifu mkubwa, alimfanyia hujuma mpaka Baba huyu akaondoka kwa haraka katika huduma.

- Mch. Jonathan Mwamboza aliyekuwa Dean wa Dayosisi alimfukuza kazi kwa chuki binafsi kwa kuwa tu alikuwa anasimamia ukweli.

- Mch. Dkt. William Kopwe aliyesomeshwa kwa gharama kubwa naye alimfukuza kwa chuki binafsi.

- Mch. Dickson Kihiyo naye amemsimamisha Uchungaji tokea Mwaka 2017, sasa ana miaka 3 anahangaika na familia yake, na wala halipwi stahiki zake kama Kanuni ya ajira na mahusiano kazini inavyoagiza. Baraza la Wachungaji chini ya Uenyekiti wa Askofu Munga lilishakubaliana kuwa Mch. Kihiyo arudishwe kazini, lakini mpaka sasa hajarudishwa.

Tunaambatanisha barua ya kusimamishwa Utumishi kwa Mchungaji Kihiyo kiambatanisho namba 11.
- Bw. Richard Shembilu aliyekuwa Mhazini wa DKMS naye pia alifukuzwa kazi bila ya kufuata kanuni; aliishitaki Dayosisi, ameshinda wakalazimika kumlipa pesa nyingi ambazo bado hawajamaliza.

9. Kuvunja Urafiki wa Kihistoria na Ujerumani
Askofu Dkt. Stephen Munga kwa sababu zake binafsi zikiwemo za kutopenda kukaguliwa na kufuatiliwa juu ya matumizi ya fedha ameamua kuvuruga urafiki uliokuwepo wa miaka mingi na Makanisa ya Ujerumani. Sasa anashinikiza kuiingiza Dasyosisi ihusiane na Dayosisi ya Lund Sweden ambayo inakubali mambo ya Ushoga.

10. Safari binafsi za Dar es Salaam kila wiki
Askofu Dkt. Stephen Munga tangu alipochaguliwa amekuwa na tabia ya kutokukaa ofisini na hivyo kila Jumatatu amekuwa akiondoka kuelekea Dar es Salaam na kukaa huko hadi Alhamisi au Ijumaa. Safari hizi zimekuwa mzigo mkubwa kwa Dayosisi yetu na hatuna mashaka kusema kuwa zimechangia kuiweka Dayosisi yetu pabaya sana kifedha. Ukaguzi wa kina ukifanyika utabaini ni kiasi gani cha fedha alichokitumia katika safari zake hizi binafsi kwa kipindi cha miaka hii 19 ya uongozi wake. Hata pale ambapo watumishi wamekuwa hawana mishahara Ofisi Kuu yeye hajawahi kukosa fedha za kuweka gari mafuta na posho za safari kwa siku hizo. Tunajiuliza maswali magumu kuwa hivi huko Dar es Salaam anakwenda kufanya nini kila wiki?

Mh. Mkuu wa Kanisa, yapo mambo mengi yanayoivuruga DKMS - KKKT chini ya Uongozi wa Askofu Dkt. Stephen Ismail Munga, tumeyaleta hayo machache ili Kanisa litafute njia ya kuikoa DKMS - KKKT toka katika mikono dhalimu.

Nasi tunapendekeza yafuatayo:

I) Askofu Dkt. Stephen Ismail Munga, kwakuwa muda wake wa Uaskofu DKMS umemaliza ajiuzulu mara moja bila ya masharti yoyote.

II) Kwa kuwa muda kwa Askofu umeshapita, asiruhusiwe kufanya kazi yoyote kama Askofu wa DKMS - KKKT, na wala asiwe msemaji wa Dayosisi, na asiruhusiwe kushiriki katika Vikao vya KKKT, viwe ni vya Halmashauri Kuu ama vya Maaskofu kwani hayuko kazini, atambuliwe kuwa ni Askofu mstaafu kama Katiba ya DKMS na ile ya KKKT ilivyoonesha.
III) Iundwe Tume Maalum ya KKKT ichunguze na kukagua fedha na madeni ya SEKOMU, Ofisi Kuu na Vituo vyote vya Dayosisi. Akaunti zote za Dayosisi zikaguliwe ikiwemo ile ya Fedha za Kigeni.

IIII) Akaunti za Askofu Dkt. Stephen Ismail Munga pamoja za Mch. Dkt. Aneth Munga, nazo zikaguliwe.

Mwisho, tumalizie kwa kusema kwamba tumelileta jambo hili mikononi mwako, kwa unyenyekevu mkubwa, ili liweze kushughulikiwa kwa dharura ili kuepusha vurugu ndani ya Dayosisi.

Iwapo Askofu Dkt. Stephen Ismail Munga, atakaidi, tuko tayari kumpeleka Mahakamani.

"Watu wa kusitasita nawachukia, Lakini sheria yako naipenda." Zab 119:113.

Tunawasilisha,

Ni sisi Waumini wa DKMS - KKKT

1.
2.


Nakala kwa:
- Maaskofu wote wa KKKT
- Katibu Mkuu KKKT
- Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya KKKT
- Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani (TZ)
- Msajili wa Taasisi za Dini Tanzania

Jr
Mmekuwa wavumilivu kwa mda mrefu sana..poleni sn
 
Tatizo Ni muundo wa
KKKT nadhani ni dhehebu linaloongoza nchini kwenye migogoro ambayo chimbuko lake ni pesa!

Swali la kujiuliza kwa nini linaongoza kwenye migogoro ya pesa?

Je, viongozi wa kutoka maeneo gani ambao wanakumbwa na migogoro ambayo chimbuko lake ni pesa?

Je, viongozi wake hawa wanajua sana umuhimu wa pesa kuliko wengine?
Tatizo Ni muundo wa uongozi wa dhehebu letu unaowafanya maaskofu wa Dayosisi Kama Munga kuwa na ukuu yaani suprimancy
Kwa mujibu wa katiba ya KKKT huyo Dr shoo aliye andikiwa barua bado Ni Celebrity tuu dhidi ya Askofu Munga
 
Ktk mambo ambayo baba munga amechemsha ni kukiondoa chuo tumaini kwa lengo la kulimit council ya tuma kujua kinachoendelea sekomu yaani mapato maTumizi na ubora huduma.
Hili ndo lililopekekea sekomu kuingia kwenye matatizo makubwa ya kifedha kiuongozi kimaadili na hatimaye serikali kukifunga baada ya migomo kadhaa ya wanafunzi na waadhili.
Tatizo la pili kanisa ni taasisi km angekua anajenga mfumo mzuri tuhuma zisinge kuwa zake ..alikua anajenga legacy yake hivyo tuhuma zikija zinamgusa yeye na mkewe tu km viongozi wa sakata kwa upande wa kwanza na wahidhinishaji na watoa pesa kwa upande wa pili ambao hauna nguvu kwa kuwa wale ni waamrishwa na wakitoa lazima wapewe asante na bwana mkubwa.
Cha tatu uvumulivu...km walivyo viongozi wengine baba yetu hana uvumilivu sasa kanisani hakuna kuhoji ila yanapotokea tofauti baina ya viongozi wa usharika na wazee wa kanisa hasa wanapoambiwa watafute mbinu za kuongeza mapato....wanapohoji baba ana taka kujua nani kohoji nin na ikiwezekana aondolewe uongozi ndani ya sharika...mifano hai ipo.hii inakutia doa kaka.

Cha nne uwazi..kizazi kimebadilika kwa kweli watu wanapenda waone matokeo chanya hata km wanaibiwa hii ndo imepelekea makanisa ya kilokole kushika hatamu...michakato mifano michache kwenye mijadala ilotangulia...huduma za radio upendo ,uanzishwaji wake,tenda zake,matumizi .yake na mifumo yake ya ajira haikuwa wazi ila kilichokuwa wazi ni lengo la makusanyo...hapa waumini wana mengi ya kuhoji ila hakuna pa kusemea
Cha tano...uwajibikaji...yaani hata ulipatwa na changamoto hukuweza kuwawajibisha walio chini yako au ww kujiwajibisha. Mfano
Kwa madeni yanayo ikabili dayosisi mpaka sasa hakuna update zimechangwa ngapi bado ngapi na wala hakuna kamati maalumu ya wana dayosisi kusimamia mchakato...hii pia imeshusha uaminifu wenu kwao.
Cha sita...visasi na malengo ya muda mfupi.baada ya madeni kuwa makubwa na hakuna uwazi ukaamua kumkimbilia marehemu mengi pia na mzee mkapa ukamsahau prof kihiyo alipokuvusha .km baba ulipaswa kujua kuwa ulipaswa kumpatanisha prof na mkeo kabla ya kumfuata marehemu mengi na mzee mkapa...hakuna namna bora ya kusafisha kidonda km hutokwangua uchafu uliopo iwe usahaa au seheemu ya ngozi ilioanza kuharibika ili utibu tatizo. Na ktk kutoa uchafu lazima maumibu yawepo.

Cha saba uaminifu. Baba nasikitika wenzako hawakuamini hii imejidhihilisha ulipokua unaomba uwe askofu mkuu...unakumbuka mara ngapi umeshindwa?hukukata tamaa ila km unapata muda wa kutafakari wenzako hawakuamini na hawakuamini kwa sababu nyingi mm ntakukumbusha mbili tu. kwanza za kiteolojia(katika dayosisi yako umetunga kitabu chako kitumike zaidi kwenye mafunzo ya kipaimara kuliko kile cha kkkt hili ni tatizo tena kubwa na km uliona kile kimepitwa na wakati ungekaa na wenzako mngetoa toleo jipya sio kujitenga kwa namna hiyo.... na ya pili uongozi ...kitendo cha kubadili katiba ya dayosisi na mkazo ukaweka kwenye mizizi ya supremacy ya kiti hilo ni tatizo kwe wenzako..unasahau .kuwa watu wa tambalale na bondeni nao walipaswa kushiriki kwa kifupi maridhiano hayakuako.wewe ulishirikisha wale unao wamudu na wachumia tumbo. Na wakati mwingine unajisahau unakua unatoa tamko km unawasemea kkkt makao makuu wakt hauna wajibu huo.
Cha nane matumizi ....baba umekuwa na matumizi yasiyo na ulazima hasa wakati huu ambapo unawatumishi hawajalipwa mishahara miezi mitatu sita hadi mwaka. Kwa kisingizio cha dayosisi haina pesa..mfano ulipokwenda mapumziko nje ya nchi...ulipkwenda kwenye sherehe ya kuapishwa yule mchungaji marekani unajua umetumia milioni ngapi...wale wamama wanao ombea kanisa ambao unawapa laki na 30 kwa mwezi ungekua umewapunguzia kiasi gani cha deni wanalokudai.?
Cha tisa...hukumu...baba unakumbuka yule mwl ulomdai mamilion ya pesa hebu kumbuka ulimdai milioni mia mbili au bilioni mbili...kwa kosa la kukuandikia waraka na kuwaomba wale uliwashugulikia msamaha kwa niaba ya kanisa unadhani ile hukumu washarika wameichukuluaje?cheo cha askofu ni cheo cha ubaba maamuzi yoyote yapaswa kuwa ya kibaba si km ya kijana asiejua majukum.

Kumi.baba pole na maandishi yetu...wachungaji wako hujawapa nafasi kukushauri mfano aliekuwa Rev wa cathedral maarufu km msocha ulipomchukua kumuamishia pale .wananchi walijua labda utamwita akushauri au labda ameogopa kukushauri yule baba tangu yupo Tanga korogwe Magamba na kokote alipotoa huduma alipohama watu walilia...hata ulipompeleka lushoto mjini waumini wa lushoto walifurahi...unajua kwa sababu gani...ni mwema ;rahimu na muadilifu hata sasa unaweza mtafuta kwa kuwa unajua ulipompeleka ...umewachagua wale wanaonufaika na pesa unazokula hivyo hawawezi kukushauri zaidi ya kukupigia makofi.
Kristo akupe macho uone...
Ni mimi
Muumini kutoka bonde
(Safarini kuelekea mlalo)

Jr
 
Namshukuru mungu nimefika Lushoto salama kuanza likizo yanvu ya siki 30.lushotoni makao makuu ya dayosisi ya kaskazini mashariki (kkkt).....wenyeji ni wakalimu haswa.
Baadhi ya mambo niliyasikia sijaamini baadhi ya hayo mambo ni km ifuatavyo
Kuna wajane wa watumishi wa kanisa wanadai haki za waume zao miaka kadhaa . Kuna watumishi wanadai mishahara miezi kadhaa ili hali baba askofu anajilipa mamilioni kwenda likizo ulaya
Kuna mifugo inafugwa kwa gharama za kanisa kwenye shamba la kanisa ila mazao ya mifugo hiyo ni personal propety ya askofu munga.(yaani mfano maziwa yakiuzwa pesa inapelekwa /inaingizwa kwenye akaunti binafsi ya baba askofu )
Baba askofu karudi nimepishana nae njiani akiwa kwenye gari la katibu mkuu.nadhani amekuja kujipanga vema na watendaji wake.

Mengine yatavyojiri nitawahabarisha. Km anasingiziwa maana nitajionea kwa macho uhalisia.
Jioni njema
 
Namshukuru mungu nimefika Lushoto salama kuanza likizo yanvu ya siki 30.lushotoni makao makuu ya dayosisi ya kaskazini mashariki (kkkt).....wenyeji ni wakalimu haswa.
Baadhi ya mambo niliyasikia sijaamini baadhi ya hayo mambo ni km ifuatavyo
Kuna wajane wa watumishi wa kanisa wanadai haki za waume zao miaka kadhaa . Kuna watumishi wanadai mishahara miezi kadhaa ili hali baba askofu anajilipa mamilioni kwenda likizo ulaya
Kuna mifugo inafugwa kwa gharama za kanisa kwenye shamba la kanisa ila mazao ya mifugo hiyo ni personal propety ya askofu munga.(yaani mfano maziwa yakiuzwa pesa inapelekwa /inaingizwa kwenye akaunti binafsi ya baba askofu )
Baba askofu karudi nimepishana nae njiani akiwa kwenye gari la katibu mkuu.nadhani amekuja kujipanga vema na watendaji wake.

Mengine yatavyojiri nitawahabarisha. Km anasingiziwa maana nitajionea kwa macho uhalisia.
Jioni njema
[4/29, 21:39] Gasto m. zn: ASKOFU MSTAAFU DKMS DKMS - KKKT MLIPENI HAKI ZAKE MJANE WA MAREHEMU MWINJILISTI MSTAAFU MICHAEL GOMBE.

Zaburi:11.1
Bwana ndiye niliyemkimbilia. Mbona mnaiambia nafsi yangu, Kimbia kama ndege mlimani kwenu?
Zaburi:11.2
Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
Zaburi:11.3
Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?
Zaburi:11.4
Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.
Zaburi:11.7
Kwa kuwa Bwana ndiye mwenye haki, Apenda matendo ya haki, Wanyofu wa moyo watamwona uso wake.

Askofu Mstaafu Dkt Stephen Ismail, ambaye huamini kuwa umstaafu, leo ulikwenda katika maziko ya Mwinjilisti Mstaafu Michael Gombe wa Karoyo Duga Usharika wa Bethelehemu unaoongozwa na Mchungaji Msumari. Na mmekuwa na Kikao hapo Mbuyukenda ambacho kimehudhuriwa na Dean Kiongozi, Katibu Mkuu wa DKMS Mch James Mwinuka, Mch Msumari wa Usharika wa Bethelehemu, na Mchungaji Ndimbo wa Usharika wa Makorora ambaye mara kwa mara anakupa rushwa ya samaki ili uepukane na Red meat, ili naye pia asihamishwe hapo Usharikani hapo.

Yote yatakuwa wazi kwani Mkuu wa Dinari ya Pwani atatujuza mara kwakuwa yuko karibu nasi.

Mlipeni haki zake huyo Mama mjane kwani mumewe anadai zaidi ya miaka miwili pensheni yake.

Askofu Munga endelea kushindana na BWANA; kwakuwa unajiona Kidume ndago.

+++Sauti ya Kijito Utofu.
[4/29, 21:39] Gasto m. zn: WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU DKMS - KKKT WAJIBIKENI PAMOJA NA ASKOFU MSTAAFU STEPHEN ISMAIL MUNGA

Kutoka:15.2
Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu ; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.
Kutoka:15.3
Bwana ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lake.
Kutoka:15.4
Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.
Kutoka:15.5
Vilindi vimewafunikiza, Walizama vilindini kama jiwe.
Kutoka:15.6
Bwana, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, Bwana, mkono wako wa kuume wawaseta-seta adui.
Kutoka:15.7
Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.

Wajumbe Wastaafu wa Halmashauri Kuu ya DKMS - KKKT, Salaam!

Ninyi mnapaswa kulaumiwa kwa kuleta msiba na majonzi katika Dayosisi hii. Ninyi mmekasimiwa na Mkutano Mkuu kuisimamia DKMS katika mambo kadha wa kadha, tena yaliyo makuu. Moyo wa Dayosisi mlikabidhiwa ninyi, lakini hamkuona thamani hiyo; ninyi ni wapumbavu na muitwe wapumbavu bila chenga, kama isemavyo Zaburi ya 53.

Mliuona mwenendo mzima wa mwana wa uasi Stephen Munga, mkamuabudu kwa PhD yake, msijue kichwa chake kimejaa upumbavu na ugonjwa wa akili; na sasa kaitumbukiza Dayosisi shimoni. Mfuko mpana mkauridhia, na kweli ukawa mpaaaanaaa, Maana Kaimu Katibu Mkuu Mch James Mwinuka, kajichotea cash Milioni 200 za Radio Utume na kumpa Shemeji yake aitwaye Munisi, Wapumbavu wakubwa, mnaangalia tu.

Mali zinauzwa mnaangalia, yaani mnatia huruma, pengine mna fedha ya aibu mnayopata.

Mungu ametuma Mjumbe wake kuikomboa hii DKMS lakini hamwonyeshi ushirikiano. Eti unataka upewe pesa, uhongwe ili utoe ushirikiano, pumbavu. wewe mdowe mjumbe wa Halmashauri Kuu, unaishi Korogwe, ni mjumbe wa muda mrefu sana, ulijaribu kuwazuia Waumini wa Korogwe wasitie saini kuwasilisha maoni ya kuukataa Uongozi dhalimu wa Askofu Mstaafu Munga, pumbavu.

Inaonesha mmepewa mlungula.

Kumbukeni muda wenu umeisha wa kuwa wajumbe wa Halmashauri Kuu: Askofu Munga muda wake wa Uaskofu umeisha, Dean pia, Kaimu Katibu Mkuu pia.

Hivi huyu mnayemwita Katibu Mkuu wa DKMS, mlimwidhinisha lini? Wekeni barua ya kumthibitisha tuione.

Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya DKMS hamna haja ya kujiuzulu kwakuwa muda wa ujumbe wenu umekwisha; ila mnatia huruma kwa kujifanya hamnazo; pumbavu.

Tubuni enyi wajumbe.
Kaeni pembeni, hatuhitaji chochote toka kwenu.

Wana DKMS tusonge mbele ukombozi uko mlangoni.

+++Sauti ya Masa Jangwani.

Jr
 
Back
Top Bottom